Subira the princess
JF-Expert Member
- Mar 3, 2018
- 2,424
- 2,587
Wasalaam, kwa mujibu wa katiba ya JMT police wana jukumu la kumlinda mwananchi na Mali zake, inamaana jeshi la police linapaswa kumtumikia mwananchi kwani ndio boss. Kwa siku za hivi karibuni jeshi letu LA police limejigeuza kuwa jeshi LA ccm na kuwaonea viongozi was upinzani kwa kuwakata hovyo na kuwafungulia kesi za kipuuzi zinazoitwa za uchochezi. Police wanapokea na kutekeleza maagizo kutoka kwa makada wa ccm wakiwamo maDC na maRC. ukitafakari kwa kina utagundua wananchi asilimia kubwa wamepoteza imani kwa jeshi la police kwani inatia ukakasi na tunajiuliza hawa police wanamtumikia mwananchi au chama cha mapinduzi? Hili ni jeshi la police au green guard ya ccm?
Ni nini hasa tafsiri ya neno uchochezi? Uchochezi maana yake nini?
Ni nini hasa tafsiri ya neno uchochezi? Uchochezi maana yake nini?