Jeshi la Polisi linakipendelea chama tawala

cantonna

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
1,120
439
BY, ZITTO KABWE;

Jeshi la Polisi wametoa kauli kufafanua uzuiwaji wa mikutano ya hadhara ya vyama vya Siasa.

Polisi wanasema kuwa ' WAMEZUIA' mikutano ya hadhara na sio mikutano ya KIKATIBA ya Vyama vya Siasa.

Hata hivyo Kamishna wa Polisi Nsato Mssanzya hakunukuu kifungu chochote cha Katiba kinachompa yeye au jeshi la Polisi mamlaka ya kuruhusu au kutoruhusu mikutano ya vyama.

Pia Polisi sio mamlaka ya kutafsiri Sheria ya Vyama vya Siasa na kujua Vikao vya kikatiba ni vipi.

Polisi wametoa ufafanuzi wao kwa sababu ya Mkutano Mkuu wa CCM. Wanasahau kuwa mkutano waliozuia wa Act Wazalendo Kongamano la Bajeti ni kwa mujibu taratibu za Chama chetu kupitia Mfumo wa kuendesha Chama kupitia Kamati za Kitaifa.

Kongamano lilikuwa ni shughuli ya kitendaji ya Kamati ya Fedha na Miradi ya ACT Wazalendo.

Pia naamini kuwa mahafali ya CHASO ni sehemu ya kanuni za Chama chao. Ufafanuzi wa Polisi unaonyesha dhahiri kuwa Jeshi hilo linaipendelea CCM.

Tutaona maajabu zaidi baada ya Mkutano Mkuu wa CCM. Chama hicho kina utaratibu wa kuzungusha Viongozi wao wapya kwenye miji mikubwa.

Magufuli anaenda kuwa anointed kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Chama ambacho yeye hajawahi kuwa hata Balozi wa Shina.

CCM wataacha utaratibu wao wa miaka yote kutambulisha Viongozi wao? Polisi watakuja tena na ufafanuzi mwingine? Tusubiri tuone. Somo?

Viongozi wajifunze kufikiri kabla ya kutamka. Matamko ya MwendoKasi haya yataleta madhara makubwa kwa Nchi.
 
Angetaja hayo madhara na sio kuishia.....blah blah blah. Maneno hayo tunashinda tunayasikia...ayaseme yapi tumchambue kwanza...
 
Polisi ya tanzania haitend haki

Inasahau kuwa kodi zetu ndio zinazowalipa wao mishahara!!!

Polisi acheni kupendelea ccm
 
Kufuaatia sintofaham inayoendelea nchini juu ya polisi kuuawa kizembe na majambazi huku wenyewe wakijiandaa kuua raia wanaodhamiria kutimiza takwa la kikatiba kuhusu maandamano na mikutano sept 1 kwa jina la ukuta; Haya ndio maoni yangu binafsi juu ya swala hili..

Na kwa kuanzia; nimejielekeza kumweleza kiongozi wa mapolisi kwa kuwa; kiongozi ndie dira ya chombo hiki..

Hii wizara inaongozwa na mmoja Wa mawaziri Vijana kabisa na anatajwa kuwa genius..

First class economist toka UDSM..

Anatajwa kuwa mmoja Wa warithi Wa JPM ndani ya CCM mwaka 2025..

Bila shaka; nilitegemea weledi Mkubwa sana Wa kuliendesha jeshi letu la polisi kwa usasa Zaidi; kisomi Zaidi; kiteknolojia Zaidi..

Sikutegemea angetumia njia zile zile za kugeuza polisi kuwa Adui Wa watu..
Polisi kutumia nguvu na silaha dhidi ya raia wema wasio na silaha na wasioasi..

Sikutegemea polisi wetu chini yake watumie intimidation techniques..

Nilitegemea kuona polisi huru wasiofungamanishwa na siasa uchwara zinazogawa watu (wao wapinxani na ss watawala)..

Kwa kinachoendelea juu ya UKUTA na matukio ya kihalifu Kila uchao (with reference ya Moshi juzi na jana dsm) ni dhahiri uendeshwaji wa jeshi letu ni business as usual..

Inaweza pia kuwa kielelezo cha kushindwa kwa waziri tunayeamini ni mahiri; msomi na kijana..

Inasikitisha sana Mtu Mwenye maono ya kuwa Amiri jeshi mkuu wetu anaendesha jeshi letu kisiasa na kuacha wakifa kizembe huku nguvu ikielekezwa UKUTA..

Inaonekana UKUTA wasio na silaha ni tishio kubwa kuliko MAJAMBAZI; wauza unga na wakwepa kodi..

Lazima Mwigulu kakaangu ajitafakari..

Akipitia mitandao ya kijamii; ataona jinsi RAIA waalivyokosa Upendo kwa polisi wao..

Vijana wanashabikia polisi kuuawa kinyama na maajambazi..
Ni ukatili kwa kiwango cha unyama..

Ila hii haijaja makisudi..
Ni zao la uendeshwaji mbovu Wa jeshi letu la polisi kwa mbinu za kikoloni..

Tuna polisi ambayo ipo integrated na watawala (CCM)..

Wamebebeshwa agenda ya kisiasa na wanatumikishwa kisiasa..

Adui Wa ccm ni adui Wa polisi..
Hii si Sawa..

Tusibadilika; si ajabu ya Tandahimba 2012 yatajitokeza tena mwaka huu..

Tandahimba polisi waliwindwa km kuku na RAIA..
Wakalazimika wahamishwe wote na kuletwa wapya 200 kufuatia mgogoro Wa polisi na RAIA..

Ni disaster..
We must change before the change finish us..

Na Ally Rama..
 
Kufuaatia sintofaham inayoendelea nchini juu ya polisi kuuawa kizembe na majambazi huku wenyewe wakijiandaa kuua raia wanaodhamiria kutimiza takwa la kikatiba kuhusu maandamano na mikutano sept 1 kwa jina la ukuta; Haya ndio maoni yangu binafsi juu ya swala hili..

Na kwa kuanzia; nimejielekeza kumweleza kiongozi wa mapolisi kwa kuwa; kiongozi ndie dira ya chombo hiki..

Hii wizara inaongozwa na mmoja Wa mawaziri Vijana kabisa na anatajwa kuwa genius..

First class economist toka UDSM..

Anatajwa kuwa mmoja Wa warithi Wa JPM ndani ya CCM mwaka 2025..

Bila shaka; nilitegemea weledi Mkubwa sana Wa kuliendesha jeshi letu la polisi kwa usasa Zaidi; kisomi Zaidi; kiteknolojia Zaidi..

Sikutegemea angetumia njia zile zile za kugeuza polisi kuwa Adui Wa watu..
Polisi kutumia nguvu na silaha dhidi ya raia wema wasio na silaha na wasioasi..

Sikutegemea polisi wetu chini yake watumie intimidation techniques..

Nilitegemea kuona polisi huru wasiofungamanishwa na siasa uchwara zinazogawa watu (wao wapinxani na ss watawala)..

Kwa kinachoendelea juu ya UKUTA na matukio ya kihalifu Kila uchao (with reference ya Moshi juzi na jana dsm) ni dhahiri uendeshwaji wa jeshi letu ni business as usual..

Inaweza pia kuwa kielelezo cha kushindwa kwa waziri tunayeamini ni mahiri; msomi na kijana..

Inasikitisha sana Mtu Mwenye maono ya kuwa Amiri jeshi mkuu wetu anaendesha jeshi letu kisiasa na kuacha wakifa kizembe huku nguvu ikielekezwa UKUTA..

Inaonekana UKUTA wasio na silaha ni tishio kubwa kuliko MAJAMBAZI; wauza unga na wakwepa kodi..

Lazima Mwigulu kakaangu ajitafakari..

Akipitia mitandao ya kijamii; ataona jinsi RAIA waalivyokosa Upendo kwa polisi wao..

Vijana wanashabikia polisi kuuawa kinyama na maajambazi..
Ni ukatili kwa kiwango cha unyama..

Ila hii haijaja makisudi..
Ni zao la uendeshwaji mbovu Wa jeshi letu la polisi kwa mbinu za kikoloni..

Tuna polisi ambayo ipo integrated na watawala (CCM)..

Wamebebeshwa agenda ya kisiasa na wanatumikishwa kisiasa..

Adui Wa ccm ni adui Wa polisi..
Hii si Sawa..

Tusibadilika; si ajabu ya Tandahimba 2012 yatajitokeza tena mwaka huu..

Tandahimba polisi waliwindwa km kuku na RAIA..
Wakalazimika wahamishwe wote na kuletwa wapya 200 kufuatia mgogoro Wa polisi na RAIA..

Ni disaster..
We must change before the change finish us..

Na Ally Rama..
bila marekebisho ya katiba ya kupunguza madaraka ya raisi watatumika sana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom