Jeshi la Polisi linajifedhehesha kwa kuzuia mikutano ya kisiasa ya wapinzani

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Akizungumza wakati wa kupokea ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Rais John Magufuli alisema siasa kwa sasa hazina nafasi hadi baada ya miaka mitano.

Kwa maneno yake bila kushurutishwa, Magufuli alisikika akisema, “niwaombe wanasiasa wenzangu, tufanye siasa za ushindani kwa nguvu zote baada ya miaka mitano ili wananchi watuhoji tuliyoyaahidi, tuliyotekeleza au ambayo hatukutekeleza.”

Kujifedhehesha kunakotajwa kwa jeshi hilo kunatokana kitendo cha kumzuia Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe kufanya mikutano ya ndani na kufungua matawi Jijini Mwanza.

“Kama ilikuwa haramu kwa Mbowe kufanya mikutano ya ndani kwenye matawi ya Chadema mkoani Mwanza na haramu pia kwa Zitto kufanya mkutano wa ndani Dar es Salaam kujadili bajeti, inakuwaje halali kwa CCM kufanya mkutano utakaokuwa na watu zaidi ya 3,000 mjini Dodoma.” Amesema Shaban Selema, mkazi wa Makiungu mkoani Singida

Aliongeza kuwa Polisi wanaonekana wana hila, wanasababisha fujo nchini, wanakandamiza demokrasia na katika mvutano huu, jeshi linaweza kuwa chanzo cha machafuko ya kisiasa.

Inashangaza mwishoni mwa wiki jeshi hilo likaibuka na kutoa taarifa kwamba halijazuia mikutano ya kiutedaji ya chama, lakini hatua hiyo ni ‘janja’ ya kukipendelea chama tawala, CCM.

Kama ilikuwa marufuku huko ndani watu kukaa kwenye mahafali, CCM wanapate uhalali wa kukusanyika tena wengi kuliko wa Chaso, bado jeshi la polisi liseme mkusanyiko huu ni halali kinyume na agizo la rais?

Jeshi hili kwa sasa limedhihirisha kuwa ni mdau wa shaka kabisa kulea demokrasia na haki nchini. Limejiweka wazi kuwa linamilikiwa na chama cha siasa na linafanya kazi za chama.
 
Wewe uwenyekiti wa maasimu wako unakuhusu nini? Nenda domdom ushuhudie vijiti vinavyokabidhiwa tu
 
Akizungumza wakati wa kupokea ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Rais John Magufuli alisema siasa kwa sasa hazina nafasi hadi baada ya miaka mitano.

Kwa maneno yake bila kushurutishwa, Magufuli alisikika akisema, “niwaombe wanasiasa wenzangu, tufanye siasa za ushindani kwa nguvu zote baada ya miaka mitano ili wananchi watuhoji tuliyoyaahidi, tuliyotekeleza au ambayo hatukutekeleza.”

Kujifedhehesha kunakotajwa kwa jeshi hilo kunatokana kitendo cha kumzuia Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe kufanya mikutano ya ndani na kufungua matawi Jijini Mwanza.

“Kama ilikuwa haramu kwa Mbowe kufanya mikutano ya ndani kwenye matawi ya Chadema mkoani Mwanza na haramu pia kwa Zitto kufanya mkutano wa ndani Dar es Salaam kujadili bajeti, inakuwaje halali kwa CCM kufanya mkutano utakaokuwa na watu zaidi ya 3,000 mjini Dodoma.” Amesema Shaban Selema, mkazi wa Makiungu mkoani Singida

Aliongeza kuwa Polisi wanaonekana wana hila, wanasababisha fujo nchini, wanakandamiza demokrasia na katika mvutano huu, jeshi linaweza kuwa chanzo cha machafuko ya kisiasa.

Inashangaza mwishoni mwa wiki jeshi hilo likaibuka na kutoa taarifa kwamba halijazuia mikutano ya kiutedaji ya chama, lakini hatua hiyo ni ‘janja’ ya kukipendelea chama tawala, CCM.

Kama ilikuwa marufuku huko ndani watu kukaa kwenye mahafali, CCM wanapate uhalali wa kukusanyika tena wengi kuliko wa Chaso, bado jeshi la polisi liseme mkusanyiko huu ni halali kinyume na agizo la rais?

Jeshi hili kwa sasa limedhihirisha kuwa ni mdau wa shaka kabisa kulea demokrasia na haki nchini. Limejiweka wazi kuwa linamilikiwa na chama cha siasa na linafanya kazi za chama.
nadhani wakuu wa polisi wanaotoa amri ambazo zinakanganya na kuleta uwezekano wa kusababisha mtafaruku katika jamii hawajui kuwa ICC itakapoanza kuchakatua mambo yake huko mbeleni, hawatapata protection ya mtu awaye yote - si CCM wala serekali yake!

kwa maana nyingine, kama wanafanya haya wakiwa wanajua athari zake huko mbeleni, basi watakuwa tu wameamua kujitoa kama mbuzi wa kafara kwa ajili ya hao wanaowatumikia.
 
Chadema wajanja sana wametuma vijana kuwachachafya polisi ili wajichanganye kauli zao na kweli polis wamejaa kingi then mwenyekiti ndio anasimama kutoa feedbak na kuwatuliza vijana kuwa kazi ishakamilika udhaifu wa polis ushaonekana
 
Ifike mahali jeshi la polisi liache kuunda na kutengeneza intelijensia za uongo kwa nia ya kuwatisha wananchi.
Wasikwepe lawama hizi kwani wapo nje ya mstari wa utendaji kazi.
Kama wameamua kuwa sehemu ya ccm basi wavue magwanda wavae sare za chama. Nalisema hili kwa uhakika kwa jinsi wanavyojitokeza kukilinda chama hicho kwa nguvu kubwa kuliko ile wanayotakiwa kwenye majukumu yao ya kisheria. Yapo wazi na kila mpenda demokrasia anayaona. Ni kwanini huyo mchafua amani hakamatwi na wanaintelijensia waliotoa taarifa ili mikusanyiko na maandamano ya kisiasa yafanywe kwa amani. Au ni mchafua amani hewa na hakamatiki? Waache kutengeneza matukio na watimize wajibu wao.
 
Back
Top Bottom