Jeshi la Polisi: Hatujapiga marufuku mikutano ya kisiasa ambayo iko kwa mujibu wa katiba za vyama

sly boy

JF-Expert Member
May 29, 2016
346
156
Jeshi la polisi nchini limetoa ufafanuzi kuwa halijazuia mikutano ya vyama vya siasa nchini walicho zuia wao ni mikutano ya hadhara ambayo walihisi hali ya usalama haikuwa nzuri.jeshi la polisi nchini limewataka wananchi kupuuza taarifa kuwa wao walizuia mikutano ya kisiasa.

==============

June 2 2016, Jeshi la polisi nchini lilitoa tamko lililolenga kuzuia mikutano, maandamano ya kisiasa nchini kutokana hali za kiusalama kutokuwa sawa.

Leo July 09 2016, Jeshi la polisi nchini limetoa ufafanuzi kuhusu tamko la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama vya kisiasa kuwa tamko hilo lililenga kuzuia maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na tamko hilo halikupiga marufuku mikutano ya kiutendaji na kiutawala ya vyama vya siasa inayofanywa kwa mujibu wa katiba na kanuni za vyama husika.

Hivyo jeshi la polisi linawataka watu wasipotoshe watu kuhusu tamko hilo na pale hali ya kiusalama itakapotengemaa, mikutano na maandamano ya vyama vya siasa itaruhusiwa kufanyika.
 
Kwani nani alikuwa hajui hilo!!
Tatizo wengi walikosa hoja ya maana
Sasa wakaona njia ya kuponea kisiasa ni hiyo
Hahaha,
Sasa wale wanaojiamini
Waende Dodoma.

HAPA TULIA
KULE MAGUFULI!!!
 
Jeshi la polisi nchini limetoa ufafanuzi kuwa halijazuia mikutano ya vyama vya siasa nchini walicho zuia wao ni mikutano ya hadhara ambayo walihisi hali ya usalama haikuwa nzuri.jeshi la polisi nchini limewataka wananchi kupuuza taarifa kuwa wao walizuia mikutano ya kisiasa.
Anhaaa,so Zitto alitaka kufanya mkutano wa siasa pale Millenium Towers?????/
 
Zitto alikuwa anafanya mkutano wa siasa Millennium Tower?.

Chaso kwenye mahafali Dodoma na Moshi,Iringa,Morogoro ilikuwa ni mikutano ya kisiasa?.

Mwiguru jimboni kwake alikuwa anafanya mikutano ya nini?.

Kweli Tz nchi yangu kuna baadhi ya majawabu ya viongozi na police inafaa yawe vivutio vya watalii.
 
Kwani nani alikuwa hajui hilo!!
Tatizo wengi walikosa hoja ya maana
Sasa wakaona njia ya kuponea kisiasa NI hiyo
Hahaha,
Sasa wale wenye ubongo WaMende
Waende Dodoma.

HAPA TULIA
KULE MAGUFULI!!!
Naona unatamani kila mtu angekuwa na ubongo kama wako, eti?

Lile kongamano la ACT Wazalendo lilikuwa hadharani au ukumbini...hebu nikumbushe genius.
 
Kwa taarifa hii
IMG-20160709-WA0035.jpg
Jeshi la Polisi linatakiwa kuwaeleza watanzania ile nguvu ya kuzuia mahafali ya vijana wa CHASO walitoa wapi?
 
June 2 2016 Jeshi la polisi nchini lilitoa tamko lililolenga kuzuia mikutano, maandamano ya kisiasa nchini kutokana hali za kiusalama kutokuwa sawa.

Leo July 09 2019 Jeshi la polisi nchini limetoa ufafanuzi kuhusu tamko la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama vya kisiasa kuwa tamko hilo lililenga kuzuia maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na tamko hilo halikupiga marufuku mikutano ya kiutendaji na kiutawala ya vyama vya siasa inayofanywa kwa mujibu wa katiba na kanuni za vyama husika.

Hivyo jeshi la polisi linawataka watu wasipotoshe watu kuhusu tamko hilo na pale hali ya kiusalama itakapotengemaa, mikutano na maandamano ya vyama vya siasa itaruhusiwa kufanyika.
 
Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake leo wamesema walichozuia ni mikutano ya hadhara na sio mikutano ya kiutendaji....

Lakini jeshi hilihili lilizuia mkutano wa ndani wa ACT....

Sasa sijui tushike lipi?
 
Kongamano la ACT lilikuwa ni mkutano wa hadhara?Hawa watu hata aibu hawana!

Ndio maana nilianzisha uzi jana wa kumpongeza na kumtakia maisha marefu aliebuni wazo la vijana wa BAVICHA kwenda Dodoma.Ni wazi bila kuwepo mpango huu wa vijana hawa kwenda Dodoma Polisi wasingesema haya wanayoyasema leo.

Huu ni ushahidi kwamba bila kukomaa hakuna kitakachoendelea.
 
Kuna wakati fulani bavicha walitaka kufanya mkutano .....polisi wakawazuia kwa kisingizio Kuna mlipuko wa kipindupindu.....

Ova
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom