Jeshi la Polisi: Hatujapiga marufuku mikutano ya kisiasa ambayo iko kwa mujibu wa katiba za vyama

before judging them lets first check on their entry point to national service..,,,ndo maana wanafundishwa fundishwa each and everything to do.....nilihisi tyu kwamba lazima tamko lao waliolisema wao wenyewe lazima walitengue maana CHIMWAGA inakuja hiyo so wanaandaa mazingira
 
before judging them lets first check on their entry point to national service..,,,ndo maana wanafundishwa fundishwa each and everything to do.....nilihisi tyu kwamba lazima tamko lao waliolisema wao wenyewe lazima walitengue maana CHIMWAGA inakuja hiyo so wanaandaa mazingira
Can you tell us your entry point to this thread?
 
Hawajapiga Marufuku bali bali wamezuia,sifa pekee ya mtu yeyote ni kuwa mkwel,hawa Polisi wanatumiwa kisiasa hivyo hata kazi zao zimekuwa za kimiongozo miongozo tu (kisiasa)
 
Kama Polisi wanazuia Watu wasikusanyike kumzika mpendwa wao kisa tu aliyefariki na waliokusanyika kumzika mpendwa huyo ni Wapinzani,kwa sababu zisizo na mashiko eti kuna mlipuko wa Kipindu pindu,nikashangazwa sana na kauli hiyo na baadaye nikajiuliza kwanini? hawakutangaza mapema liwe Tangazo la Dharura katika eneo husika kama walikuwa na nia njema.Nikagundua siasa ndiyo inaliongoza Jeshi la Polisi,hii ni hatari sana
 
Ndg, spade4spade najua we ni miongoni mwa wale vijana 46 waliotajwa kwenye maazimisho ya chama kule singida vipi hujaukwaa tu uheshimiwa maana chairperson alimwomba jamaa asiwasahau kwa kazi yenu nzuri Mtandaoni. Tuyaache hayo hebu niambie vizuri labda mie sijaelewa Msingi wa katazo la polisi ilikuwa si kupiga marufuku ya kuikosoa serikali. Bali hali ya usalama, kwa hoja ya kuwepo viashiria vya uvunjifu wa amani. Ndio sababu ya kuzuia mikutano ya hadhara kwasababu inahusisha halaiki ya watu udhibiti wa hali ya utulivu ni mdogo. Mikutano ya ukumbini na mahafali hata kama ni ya chama Fulani havikuwa kwenye misingi ya katazo kwahiyo hoja yako kuwa mkutano wa zitto pale ukumbini ulikuwa na nia kuisema serikali vibaya haina mashiko kwani suala la kuikosoa serikali ni la muda wowote na ni haki ya kila mwananchi bila kujali chama. Hivyo kutokana na ufafanuzi uliotolewa na polisi, zuio la mkutano wa zito pamoja na mahafali ya CHASO ni batili kwani haviendani na misingi ya katazo. Polisi walibugi na we pia unazidi kubugi
Bhikalamba!
Mimi siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa na huenda katika maisha yangu sintobahatika kuwa mwanachama! Kejeli zako za kunibandika kuwemo kwenye kundi la vijana 46 ambalo hata sijawahi kulisikia kabla yako pia ni njema.

Mtu neutral kama mimi atauona ukweli wa nilichoandika na mtu shabiki wa aina yako lazima awe mwamba ngoma! Nilichoandika nimeandika na ulichotafsiri umetafsiri, hakuna shida; lakini kama sikosei nafikiri hata mzee wako mamvi amekigusia kule Arusha kwenye sherehe za kujipongeza kwa ushindi wa madiwani wake.

Nchi hii hatutafuti uhuru bali tunapigania mkate! Mkate wetu itakuwa rahisi kuupata tukiwa na afya nzuri, barabara nzuri, mawasiliano mazuri, n.k.

Chama cha siasa nia yake ni kuongoza dola, hivyo ni kutafuta kila penye kasoro na kuwaeleza wananchi kwa ufasaha na kwa ustaarabu ili waelewe na kukipa sapoti katika uchaguzi.

Siyo kutumia nguvu ya maandamano ya mateja na madogo wenye mihemko ya kukosa ajila za Serikali.

Hatupati dola kwa kumkashifu, kumbeza na kumkejeli Rais, NS na viongozi wengine. Na wala siyo kwa kuwalazimisha watu wawaunge mkono kwa utaratibu unaofanana na Jihad hata kama machoni petu mnatenda dhambi na kusema uongo zaidi ya Shetani.

Hatuendi Ikulu kwa kubadilisha uhalisia wa sentensi wanazotoa viongozi na kuzitafsiri katika namna ya vichekesho mnavyopenda msikie na kuwaaminisha wengine! Na wala hatuendi kwa kunyoosha madole yetu ya kati, tukiwavua baraghashia zao watu wengine kwa nguvu na kutengeneza mabango na fulana zenye maandishi makubwa yenye kejeli na kashfa au ushawishi wa vurugu na viashiria vya kutuletea timbwili la kuuana sisi na vizazi vyetu hadi kufikia vya nane mpaka kumi.

Kutafuta kuingia Ikulu hakuletwi na kwenda Dodoma kwa kuwalipa vijana mihemko ili wakafanye shughuli za watu waliopewa kazi hiyo kwa mafunzo, wakatambuliwa na sheria na wakalipwa kodi zetu. Na hakuletwi kwa kwenda kaburi la baba wa taifa na kufanya maigizo ya kunuiza na kujirekodi kisha ukarudi kwetu kututangazia eti ulienda kushitaki.
 
Wamesema hawakuzuia, wewe unawaomba wazuie mkutano wa CCM Dodoma, mnajichanganya mkuu. Kama walizuia mikutano, mbona mlifanya mkutano Butiama mkoani Mara na mpaka mkaweka azimio la kwenda Dodoma kuisaidia police kuzuia ccm, na wala hamkutawanywa? Mlienda mbali mpaka mkaandikisha vijana 300 waliofuzu mafunzo yao huko Mara. Jmn amani yetu ni kitu muhimu sana.


Mkuu.
Jitahidini sana kumuosha maiti lakini, haosheki jamani. Hapa ni mpaka mwenye kuitoa ile kauli aamue kuifuta kama akitaka. Angalieni, waweza hadaa watu lakini ni kwa muda tu. Mnataka kukutana kwa nguvu zote!!! mbona mnampinga rais?? Amesema, mikutana yoote ya siasa ni mpaka 2020. Tiini amri bila shurutiiiiiiiii
 
Mimi Nina swala LA kisiasa linanishangaza sana kama sio kustaajabu Kwa nini jeshi LA polisi wanachama wa chama Au vyama pinzani wakitaka kufikisha ujumbe wao kunakohusika Kwa njia ya maandamano hupigwa sana na polisi. mi nionavyo kazi ya jeshi LA polisi ni kulinda amani na sio kuivunja walitakiwa kama ni maandamano walindwe hadi mwisho wao Nilitaraji kua hayo ndo maadili ya polisi.
 
Wenzio swali hilo tumeanza kujiuliza tangu mwaka 1995 enzi za ngangari na ngunguri mpk leo majibu hatujapata. Usituchoshe
 
Back
Top Bottom