dubu
JF-Expert Member
- Oct 18, 2011
- 3,495
- 3,458
Heshima kwenu wakuu,
Kwanza niwapongeze TAKUKURU na taasisi ya Kupambana na dawa za kulevya kwa kuweza kutenda kazi zao bila kujali chama cha mtu wala cheo chake.
Japo TAKUKURU wamekuwa wakipokea Maagizo kutoka juu, lakini wanaonesha japo nia ya kifanya kazi wasipoingiliwa. Mfano Wapokea waliokuwa wanahusika na kununua Madiwani, Nasssri alipeleka ushahidi lakini ukaharibiwa. Tunaelewa.
Taasisi ya kupambana na dawa za kulevya hadi sasa sina la kuwalaumu kwani wanafanya kazi nzuri kabisa.
Ila jeshi la Polisi wameshindwa kujipambanua kwenye ukada wa chama tawala. Hii ni changamoto kwao..
Mfano: Kuna Mbunge wa CCM anaitwa Dr. Godwin Mollel wa Jimbo la Siha, alisema mbele ya Umma kwamba ana Video za watu waliomshambulia kwa risasi Tundu Lissu. Aliyasema hayo 8/2/2019, lakini hadi leo 15/2/2019 Polisi wameshindwa kwenda kuuchukua huo ushahidi. Japo hata kumhoji tu wameshindwa.
Case closed: Mbunge Mollel adai ana ushahidi wa Chadema kuhusika issue ya Lissu - JamiiForums
Hapo ndo wasiwasi wangu ulipo.
Kuna kada wa CCM alimtishia kumuua Ben Saanane na Ben Saanane akapotea kweli. Ila alikuwa kashatoa namba ya simu ya wanaomtishia kituo cha Polisi, lakini hadi leo hakina aliyehojiwa..
Ben Saanane: Ninatishwa kuuawa kwa kuikosoa Serikali - JamiiForums
Kuna waliomuua Mwenyekiti wa CHADEMA Geita Alfonce Mawazo, pamoja kwamba wanajulikana lakini hakuna aliyekamatwa.
Kinachoniuma zaidi, Tundu Lissu, Ben Saanane na Alphonce Mawazo ni Wanachama wenzangu wa JamiiForums.
Kwa hali hii Polisi wataaminikaje?
Je, CCM wanayoyafanya, wafuasi wa vyama vingine wanashindwa kuyafanya?
Polisi inabidi wajitafakari kwa hili..
Polisi wanabambikia watu kesi, wengi wanaobambikiwa kesi ni vyama vya Upinzani. Hili nakumbuka hata rais alishawaonya.
Jaji Kiongozi:Askari Polisi wanabambika raia kesi - JamiiForums
Ninayo mengi ya kuongea.. Ila nawaogopa Polisi sababu wana bunduki. Lakini wangekuwa wanakubali kuweka bunduki chini tukabishana kwa hoja, wangekimbia kwa aibu.
TANZIA: Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo auawa kikatili mjini Katoro - JamiiForums
Kwanza niwapongeze TAKUKURU na taasisi ya Kupambana na dawa za kulevya kwa kuweza kutenda kazi zao bila kujali chama cha mtu wala cheo chake.
Japo TAKUKURU wamekuwa wakipokea Maagizo kutoka juu, lakini wanaonesha japo nia ya kifanya kazi wasipoingiliwa. Mfano Wapokea waliokuwa wanahusika na kununua Madiwani, Nasssri alipeleka ushahidi lakini ukaharibiwa. Tunaelewa.
Taasisi ya kupambana na dawa za kulevya hadi sasa sina la kuwalaumu kwani wanafanya kazi nzuri kabisa.
Ila jeshi la Polisi wameshindwa kujipambanua kwenye ukada wa chama tawala. Hii ni changamoto kwao..
Mfano: Kuna Mbunge wa CCM anaitwa Dr. Godwin Mollel wa Jimbo la Siha, alisema mbele ya Umma kwamba ana Video za watu waliomshambulia kwa risasi Tundu Lissu. Aliyasema hayo 8/2/2019, lakini hadi leo 15/2/2019 Polisi wameshindwa kwenda kuuchukua huo ushahidi. Japo hata kumhoji tu wameshindwa.
Case closed: Mbunge Mollel adai ana ushahidi wa Chadema kuhusika issue ya Lissu - JamiiForums
Hapo ndo wasiwasi wangu ulipo.
Kuna kada wa CCM alimtishia kumuua Ben Saanane na Ben Saanane akapotea kweli. Ila alikuwa kashatoa namba ya simu ya wanaomtishia kituo cha Polisi, lakini hadi leo hakina aliyehojiwa..
Ben Saanane: Ninatishwa kuuawa kwa kuikosoa Serikali - JamiiForums
Kuna waliomuua Mwenyekiti wa CHADEMA Geita Alfonce Mawazo, pamoja kwamba wanajulikana lakini hakuna aliyekamatwa.
Kinachoniuma zaidi, Tundu Lissu, Ben Saanane na Alphonce Mawazo ni Wanachama wenzangu wa JamiiForums.
Kwa hali hii Polisi wataaminikaje?
Je, CCM wanayoyafanya, wafuasi wa vyama vingine wanashindwa kuyafanya?
Polisi inabidi wajitafakari kwa hili..
Polisi wanabambikia watu kesi, wengi wanaobambikiwa kesi ni vyama vya Upinzani. Hili nakumbuka hata rais alishawaonya.
Jaji Kiongozi:Askari Polisi wanabambika raia kesi - JamiiForums
Ninayo mengi ya kuongea.. Ila nawaogopa Polisi sababu wana bunduki. Lakini wangekuwa wanakubali kuweka bunduki chini tukabishana kwa hoja, wangekimbia kwa aibu.
TANZIA: Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo auawa kikatili mjini Katoro - JamiiForums