KazaMwendo
New Member
- Nov 1, 2009
- 4
- 0
Inasikitisha sana kuona vijana wanapata ajira serikalini halafu bila kutendewa haki mnawafukuza kwa makosa yenu wenyewe.Jeshi la magereza walitangaza nafasi za kazi ambapo walitakiwa wasomi na wengineo.Tulijitokeza kufanya interview na baada ya wiki mbili majibu ya tuliofanikiwa yakatoka.Tukaweka kambi chuo cha maofisa UKONGA na kufanyiwa vipimo vyote mbavyo vinatakiwa.Ninaposema vyote namaanisha vyote.Baada ya hapo tukapewa majibu yetu na kujiandaa kwa ajili ya kwenda kiwira kwa mafunzo.Tukaenda mafunzoni tukiwa tunajua tumeajiriwa na serikali kwani walituhakikishia kuwa tayari rumepata ajira.Sasa ndugu zangu ajabu ni kwamba baada ya kuanza mafunzo kule kiwira kwa miezi miwili,wanakuja haohao waliotuambia tumeajiriwa,wanakuja na kuwafukuza wenzetu kwa kigezo cha matatizo ya afya.Ndugu zangu,hawa watu walitupima wote na kutupa majibu kulekule UKONGA kabla ya kwenda mafunzoni.sasa kama sio njama za kuwatoa wenzetu na kuwaweka watu wao ni nini? Kwanini hawakusema mapema?Kweli ni haki iliyotendeka hapa.? Kuwapeleka watu mafunzoni wamehangaika miezi 2 halafu mnawafukuza kwa makosa yenu nyie?? Wana JF hapo pako sawa? Mbaya zaidi wengine wametolewa kwa kisingizio cha kuwa wanaumwa macho,wakati walipimwa na kuridhika nao...Serikali inatupeleka wapi???
Mkereketwa
Mkereketwa