Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujiunga na mafunzo kwa wakujitolea, 2017

Nimeiinulia mikono pitch ya udsm, round 8 pale sio poa kwa kweli, asikudanganye mtu. Mtu unaeza ukafa kama masihara, haishangazi kuona wengi wamezimia leo. Nlikua kwenye kundi la watu wanaokimbia hatari, binafsi ilifkia hatua mwili ukakataa ilihali akili na moyo vinataka, nkaona nkipiga hatua nyingine hata 1 tu naeza nkazima kweli. Nkaona isiwe kesi, ya nini nizime wakati miarobaini ya kivuli naiona
pole sana mkuu...hukutema nyongo kweli hhaahh....
 
Asante sana mkuu, ilifkia hatua nlishindwa kuendelea, nadhani ningeendelea kujifanya nakaza ningetema kweli nyongo. Acha kabisa mziki wa kukimbia mita 400 ×8 wakati wa jua la saa 7 mchana ilihali watu mmekaa chini tangu saa 11 alfajiri bila kula wala kunywa chochote
Pole sana mkuu... maisha popote si lazma jkt kwanza uhakika wa ajira hakuna kule....

Unaweza lima miaka yote then ukaambulia kurudi nyumbani mikono mitupu...
 
Pole sana mkuu... maisha popote si lazma jkt kwanza uhakika wa ajira hakuna kule....

Unaweza lima miaka yote then ukaambulia kurudi nyumbani mikono mitupu...
Shukran mkuu, ndo maana baada ya kutambua hilo mnamo round ya 6 mwili ukiwa umekataa ilihali najua 8 ndo ingependeza sasa, nkaona bora nijilaze kwenye kivuli safi cha miarobain ili kuepusha maafa ambayo yangeweza kujitokeza
 
Shukran mkuu, ndo maana baada ya kutambua hilo mnamo round ya 6 mwili ukiwa umekataa ilihali najua 8 ndo ingependeza sasa, nkaona bora nijilaze kwenye kivuli safi cha miarobain ili kuepusha maafa ambayo yangeweza kujitokeza
tuko pamoja mkuu....

Huko binafsi niliona hakunifai nikaamua kupapotezea ngoja niendelee kupambana na maisha ya kitaa....
 
Asante sana mkuu, ilifkia hatua nlishindwa kuendelea, nadhani ningeendelea kujifanya nakaza ningetema kweli nyongo. Acha kabisa mziki wa kukimbia mita 400 ×8 wakati wa jua la saa 7 mchana ilihali watu mmekaa chini tangu saa 11 alfajiri bila kula wala kunywa chochote


Wait...
Umesema mlikaa chini tangu saa 11 alfajiri, ilikuaje mkakaa hivo...
Kwani mliambiwa mfike muda huo hapo UDSM kuanza kukimbia?? Sasa iweje mkakimbia saa saba mchana??
Muda wote toka alfajiri mpaka mchana huo mlikua mnafanya nini...
Ni kweli mlifika saa 11 alfajiri kweli na huu usafiri shida wa Dar...
 
Kila la kheri kwa wote waliofanikiwa kuendelea na hii safari, Mungu azidi kuwatia nguvu na kuwafanikisha katika safari yenu


Mkuu...
Kama bado una maganzi na kihangaiko, si ukimbie kwenye wilaya zingine ambazo usaili bado haujamalizika ukajaribu tena bahati yako... Mfano hata mkoani huko... Kwani wilaya zote wanafanya usaili simultaneously??
Mbona nasikia zingine tayari, zingine bado... Dandia wilaya zingine mkuu...
 
Nimeiinulia mikono pitch ya udsm, round 8 pale sio poa kwa kweli, asikudanganye mtu. Mtu unaeza ukafa kama masihara, haishangazi kuona wengi wamezimia leo. Nlikua kwenye kundi la watu wanaokimbia hatari, binafsi ilifkia hatua mwili ukakataa ilihali akili na moyo vinataka, nkaona nkipiga hatua nyingine hata 1 tu naeza nkazima kweli. Nkaona isiwe kesi, ya nini nizime wakati miarobaini ya kivuli naiona


Dah mkuu poleni aisee maana jinsi unavyoelezea mweeh
 
Shukran mkuu, ndo maana baada ya kutambua hilo mnamo round ya 6 mwili ukiwa umekataa ilihali najua 8 ndo ingependeza sasa, nkaona bora nijilaze kwenye kivuli safi cha miarobain ili kuepusha maafa ambayo yangeweza kujitokeza

Ila mkuu jinsi unavyoelezea unaniacha hoi sana kwa kweli yani bora ukaenda ombea nafasi vijijini huko hapa mjini jau saana
 
Wait...
Umesema mlikaa chini tangu saa 11 alfajiri, ilikuaje mkakaa hivo...
Kwani mliambiwa mfike muda huo hapo UDSM kuanza kukimbia?? Sasa iweje mkakimbia saa saba mchana??
Muda wote toka alfajiri mpaka mchana huo mlikua mnafanya nini...
Ni kweli mlifika saa 11 alfajiri kweli na huu usafiri shida wa Dar...
Tulifika saa 11 kasoro alfajiri mkuu, na jana walitupiga mkwara kinoma kua nidhamu ya kuwahi ndo inaanza kupimwa hapo, na kweli waliochelewa wakawekwa pembeni, ingawa walisamehewa baadae. Baadae wakasema wanasubiri kijua kianza kutoka saa 2 asubuh mchakato uanze, na wakaanza na la saba na kuendelea, ambao walikua kibao, wakawekwa vikundi vya watu 20 20, wengine tumekalishwa chini kusubiri. Sisi ndo tukawa wa mwisho. Inafika zamu yetu tayari ni saa 7 na ushee mchana, jua limechanganya balaa na mtu ushachoka kwa kukaa chini tangu 11 alfajiri bila kutia chochote mdomoni, hata maji. Kundi letu tulianza 20 kama kawaida, ila round ya 6 tukabaki kama wanne au watano hivi, na mi ndo hali yangu ikawa tete nkajilaza kwenye miarobaini. Mwishon kama ilivyo kawaida wakachkuliwa watatu wa kwanza na shughuli ndo ikaishia hapo
 
Mkuu...
Kama bado una maganzi na kihangaiko, si ukimbie kwenye wilaya zingine ambazo usaili bado haujamalizika ukajaribu tena bahati yako... Mfano hata mkoani huko... Kwani wilaya zote wanafanya usaili simultaneously??
Mbona nasikia zingine tayari, zingine bado... Dandia wilaya zingine mkuu...
Nlifkiria hivyo pia mkuu, ila nkaskia wilaya karibu zote deadline tayari, ingawa sikua na uhakika na hiyo taarifa. Ningejua wilaya gani bado ningeenda chap, naskia mikoani hamna msoto kama ule wa udsm
 
Back
Top Bottom