Jeshi Hili la Wanawake Chadema Laweza Kufanya Mabadiliko Makubwa 2020

Mkongwe Mzoefu

JF-Expert Member
Aug 10, 2018
842
2,467
Kongamano lililofanywa na BAWACHA (Baraza la Wanawake Chadema) Leo hii katika ukumbi wa Mlimani City halijapata kuonekana nchini sio kwa wingi wake bali VIBE na msisimko wake wa kweli toka kwa wahudhuriaji.

Wamekuja kwa hiari, kwa gharama zao, mioyo yenye furaha na heshima pamoja na kutikuwa na woga wowote na tabia ya watawala kuonea yeyote asiye CCM akiwa na furaha.

Jee Wanawake hawa wakirudi watokako na kueneza ujumbe wa Chadema wa #NohateNofear kwa Wanawake wote nchini na kuwafahamisha kiini cha matatizo yao ni CCM na huku uongozi ukipambana kuleta Tumehuru ya uchaguzi hadi iwepo CCM itapona?

Kumbe kifo cha CCM kimeshikiliwa na Wanawake?
chadema_newz_tz___B9eMiEmHxvM___.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya ndio mambo yanayokifanya chama dola hadi leo wasiwe na amani,kwa wana ccm wote viacheni vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi zake kikatiba,weka tume huru(sio hii ya watendaji kuteuliwa na mkaazi mkuu wa pale magogoni),level playing field then uchaguzi ufanyike ,atakayeshinda awe ameshinda kihalali na atakayeshindwa awe wa kwanza kumpongeza aliyeshinda,sio sasa eti ccm wapo Ilula wanashuka Kitonga Pass na wengineo wapo comfort Hotel halafu ccm wanadai tuone nani atawahi kufika !!
 
Aluta Continuaa....!!munaweza mukatishwa mukakatiswhwa tamaa,lakini niwambie wanawake ni Dada zetu,mama zetu,rafiki zetu,walezi wetu. Munajua nini mnakifanya mnajua nini tunakikosa..azma ya kuturidhisha mnayo;azma ya kutukomboa mnayo!!pambaneni mpaka mjue mahtaji yetu yamepatkana!!mwanamke ndy nuru. Nuru ya kumulika penye Giza!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kongamano lililofanywa na BAWACHA (Baraza la Wanawake Chadema) Leo hii katika ukumbi wa Mlimani City halijapata kuonekana nchini sio kwa wingi wake bali VIBE na msisimko wake wa kweli toka kwa wahudhuriaji.
Wamekuja kwa hiari, kwa gharama zao, mioyo yenye furaha na heshima pamoja na kutikuwa na woga wowote na tabia ya watawala kuonea yeyote asiye CCM akiwa na furaha.
Jee Wanawake hawa wakirudi watokako na kueneza ujumbe wa Chadema wa #NohateNofear kwa Wanawake wote nchini na kuwafahamisha kiini cha matatizo yao ni CCM na huku uongozi ukipambana kuleta Tumehuru ya uchaguzi hadi iwepo CCM itapona?
Kumbe kifo cha CCM kimeshikiliwa na Wanawake?
View attachment 1380918

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuanzia Leo chadema shimoo,never seen before.siku ya Leo wakinamama Wa chadema wamefanya jpili yangu kua safi hawa jamaa kweli wanasiasa za namba au hesabu au kidigital.Naunga mkono hoja yako mkuu
 
Kongamano lililofanywa na BAWACHA (Baraza la Wanawake Chadema) Leo hii katika ukumbi wa Mlimani City halijapata kuonekana nchini sio kwa wingi wake bali VIBE na msisimko wake wa kweli toka kwa wahudhuriaji.
Wamekuja kwa hiari, kwa gharama zao, mioyo yenye furaha na heshima pamoja na kutikuwa na woga wowote na tabia ya watawala kuonea yeyote asiye CCM akiwa na furaha.
Jee Wanawake hawa wakirudi watokako na kueneza ujumbe wa Chadema wa #NohateNofear kwa Wanawake wote nchini na kuwafahamisha kiini cha matatizo yao ni CCM na huku uongozi ukipambana kuleta Tumehuru ya uchaguzi hadi iwepo CCM itapona?
Kumbe kifo cha CCM kimeshikiliwa na Wanawake?
View attachment 1380918

Sent using Jamii Forums mobile app
Makonda mwenyewe aliona kwenye You Tube akawa haamini ikabidi atimbe viwanjani kushuhudia macho yake. Haamini umati mkubwa wa wanawake wasioogopa mabomu wametoka wapi?
 
Mkuu kuanzia Leo chadema shimoo,never seen before.siku ya Leo wakinamama Wa chadema wamefanya jpili yangu kua safi hawa jamaa kweli wanasiasa za namba au hesabu au kidigital.Naunga mkono hoja yako mkuu
Namba hazidanganyi
 
Watanzania wanataka wanataka Demokrasia wasipoiona wasipoipata ndani ya Chadema wataipata nje ya Chadema.

Watanzania wanaangushwa na viongozi wa vyama vya upinzani hasa Mbowe.

Wapo tayari lakini Mbowe hana jipya zaidi ya kulalamika kuwa hapewe nafasi ya kuandamana lakini anashindwa kuoanisha maendeleo na maendeleo vinaendaje sambamba ?
Kwa nini watu waandamane na kufanya mikutano kila siku badala ya kufanya kazi?
Kwa nini kuna umuhimu wa Tume huru kwa CCM na Dola yake?
Nini madhara ya kukosa tume huru?
Nani ataipenda Chadema chama kinachoongozwa na Mbowe asiye na maono? Hivi ni chama gani kinachokataa watu toka vyama vingine na kuwafanyia figisu waliopo ili wakimbie wabaki wachache wasioijua dola wala namna ya kuongoza dola?

Nani ataiamini Chadema inatoongozwa na DJ kihuni huni badala ya kuwatumia watu waliokomaa kisiasa wanaotamani kujiunga na Chadema yeye anawaza kuwafanyia figisu wale wote wenye mawazo tofauti na uongozi wake?

Uongozi wa Kitaifa wa Chadema umepwaya sana.
Siasa za awamu hii ni nyepesi sana mana CCM ya Bshir ni dhaifu kuliko ile ya Kanali wa Jeshi A.Kinana na Luten wa Jeshi Joseph Makamba. Ni CCM Inayojificha nyuma ya Majeshi wakati wanaoiongoza ni raia kamili.

Chadema ingepaswa kuongozwa na Kamanda Heche na Katibu mkuu awe Kamanda Juma Mwalimu na Mwenezi awe Kamanda Sugu.
Msemaji awe ni Kamanda Mch. Mchungaji Msigwa.
Idara ya Fedha ishikiliwe na Kamanda Komu .

Mbowe angetola na mambo yake ya Ukabila na Chama kingetakasika na kuwa kimbilio la kila mtanzania Msomi na mwenye Maono na nia ya kuitoa CCM kwa gharama ya wenye nchi wenyewe bila kujali makabila yetu.
Hatuwezi kukiunga mkono chama cha Mbowe na ukoo wake uliojivika koti la ukabila wa Hai.

Nawapongeza wakina mama wa BAWACHA kwani wameonyesha kuwa Roho ya Chadema sio Mbowe na fedha yake kama tunavyoaminishwa Bali ni wanyonge wanaoipigania Demokrasia kwa gharama zao na nafsi yao juhudi zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku zinavyozidi kusonga wanaume nawatoa kwenye imani, Mara nyingi huwa najiuliza mbona wanawake hawayumbishwi na uungaji mkono juhudi? na ukiangalia kwenye mikutano/makongamano huwa wanajitokeza kwa wingi sana huku wamevalia sare za chama bila woga wowote? na huwa wanatembea kwa kulinga na madaha bila woga wowote?inashangaza, inafurahisha na kuleta matumaini,ina maana wanawake wametuzidi ujasili na maamuzi wanaume?ebu ngoja kwanza
 
Back
Top Bottom