4 7mbatizaji
JF-Expert Member
- Dec 8, 2019
- 5,978
- 6,782
Ebu na wewe porojo zako hapa .Ccm ikifanya vizuri tutasifia na chadema Leo imefanya vizuri lazima tuisifie,Unakaa kumnanga mwanaume mwenzako Mbowe kafanya nini?Leta hoja hapa watu waipime na kujadili yenye maana kwa nini mnapenda sana kujitoa ufahamu na kuhishiwa mahalifa kwa kufuata mkumbo,jiamini na jikubali kwamba wewe ni nani na bila ccm au chadema au bila chama maisha yako bado yanabaki kama maisha yako sio eti mpaka mtu anasafiri mkoa mpaka mkoa kuvuruga mikutano ya watu na kama amepewa pesa nyingi hata laki tano haifiki.Watanzania wanataka wanataka Demokrasia wasipoiona wasipoipata ndani ya Chadema wataipata nje ya Chadema.
Watanzania wanaangushwa na viongozi wa vyama vya upinzani hasa Mbowe.
Wapo tayari lakini Mbowe hana jipya zaidi ya kulalamika kuwa hapewe nafasi ya kuandamana lakini anashindwa kuoanisha maendeleo na maendeleo vinaendaje sambamba ?
Kwa nini watu waandamane na kufanya mikutano kila siku badala ya kufanya kazi?
Kwa nini kuna umuhimu wa Tume huru kwa CCM na Dola yake?
Nini madhara ya kukosa tume huru?
Nani ataipenda Chadema chama kinachoongozwa na Mbowe asiye na maono? Hivi ni chama gani kinachokataa watu toka vyama vingine na kuwafanyia figisu waliopo ili wakimbie wabaki wachache wasioijua dola wala namna ya kuongoza dola?
Nani ataiamini Chadema inatoongozwa na DJ kihuni huni badala ya kuwatumia watu waliokomaa kisiasa wanaotamani kujiunga na Chadema yeye anawaza kuwafanyia figisu wale wote wenye mawazo tofauti na uongozi wake?
Uongozi wa Kitaifa wa Chadema umepwaya sana.
Siasa za awamu hii ni nyepesi sana mana CCM ya Bshir ni dhaifu kuliko ile ya Kanali wa Jeshi A.Kinana na Luten wa Jeshi Joseph Makamba. Ni CCM Inayojificha nyuma ya Majeshi wakati wanaoiongoza ni raia kamili.
Chadema ingepaswa kuongozwa na Kamanda Heche na Katibu mkuu awe Kamanda Juma Mwalimu na Mwenezi awe Kamanda Sugu.
Msemaji awe ni Kamanda Mch. Mchungaji Msigwa.
Idara ya Fedha ishikiliwe na Kamanda Komu .
Mbowe angetola na mambo yake ya Ukabila na Chama kingetakasika na kuwa kimbilio la kila mtanzania Msomi na mwenye Maono na nia ya kuitoa CCM kwa gharama ya wenye nchi wenyewe bila kujali makabila yetu.
Hatuwezi kukiunga mkono chama cha Mbowe na ukoo wake uliojivika koti la ukabila wa Hai.
Nawapongeza wakina mama wa BAWACHA kwani wameonyesha kuwa Roho ya Chadema sio Mbowe na fedha yake kama tunavyoaminishwa Bali ni wanyonge wanaoipigania Demokrasia kwa gharama zao na nafsi yao juhudi zao.
Sent using Jamii Forums mobile app
Binadamu unanunuliwa kama mfugo mnadani alafu izo pesa unapelekea mkeo na wanao ndo maana tunaandamwa na mikosi na laana very shame binafsi heli nife na umaskini siwezi jaribu ujinga huu mbele ya mungu na wazazi wangu walionileta duniani