nyamakonge
JF-Expert Member
- May 28, 2013
- 363
- 130
Wanabodi nachukua fursa hii kuwatakia afya njema. Nami naomba nichukue fursa hii kutoa maoni yangu juu ya yale aliyoyazungumza Mh. Jesca Kishoa mbunge wa viti maalumu kupitia CHADEMA na mke halali wa mwanasiasa David Kafulila.
Mapema katikati ya wiki hii David Kafulila ambaye alikua mwanachama wa chama cha demokrasia na maendeleo alitangaza uamuzi wake wa kujitoa kwenye chama hicho akidai kimepoteza dira katika kupambana na ufisadi.
Kafulila awali alikuwa mbunge na kada wa NCCR Mageuzi kabla ya kujiunga CHADEMA. Kafulila na Jesca wamefunga ndoa na kubahatika kupata mtoto mmoja.
Kuhama kwa Kafulila ni moja ya haki yake ya kikatiba bila kuangaliza sababu alizozitaja. Kilichonifanya niandike ni hiki sasa mara baada ya Kafulila kuhama mke wake Bibi Jesca Kishoa aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kukosoa uamzi huo wa mme wake hadharani huku akienda mbali na kuponda sababu zilizomfanya ahame. Jesca hakuishia hapo amediriki kubadili account zake mitandao ya kijamii kwa kutoa picha zote za mme wake na kubadili jina ambapo awali alikua akijiita Jesca Kafulila.
Kama mzalendo na mpenda taifa hili nimejiuliza hatua hii ya mke wa Kafulila ni ya nini? Yaani sisi kama taifa tumefika sehemu mpaka mambo ya kisiasa yanatugawa hadi kwenye familia?
Hata kama Jesca hakuridhishwa na uamuzi wa mme wake alitakiwa amuunge mkono kwa uamzi wake ambao ni halali kikatiba na kumpa moyo wa kusonga mbele na kumtaka wapambane kwa hoja sasa. Lakini kitendo cha yeye kuitisha mkutano na wanahabari na kumkosoa mme wake kimemfanya aonekane bado sio mkomavu kisiasa.
Na kama hali ndio hii itafika wakati ili kuoa utakua unaulizwa chama cha kisiasa unachokikubali ni kipi ndio unaruhusiwa kuoa/kuolewa. Tusifike uko kama taifa tuanze kukataa hizi chuki zinazotaka kutugawa .
Wasalaaam
Mapema katikati ya wiki hii David Kafulila ambaye alikua mwanachama wa chama cha demokrasia na maendeleo alitangaza uamuzi wake wa kujitoa kwenye chama hicho akidai kimepoteza dira katika kupambana na ufisadi.
Kafulila awali alikuwa mbunge na kada wa NCCR Mageuzi kabla ya kujiunga CHADEMA. Kafulila na Jesca wamefunga ndoa na kubahatika kupata mtoto mmoja.
Kuhama kwa Kafulila ni moja ya haki yake ya kikatiba bila kuangaliza sababu alizozitaja. Kilichonifanya niandike ni hiki sasa mara baada ya Kafulila kuhama mke wake Bibi Jesca Kishoa aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kukosoa uamzi huo wa mme wake hadharani huku akienda mbali na kuponda sababu zilizomfanya ahame. Jesca hakuishia hapo amediriki kubadili account zake mitandao ya kijamii kwa kutoa picha zote za mme wake na kubadili jina ambapo awali alikua akijiita Jesca Kafulila.
Kama mzalendo na mpenda taifa hili nimejiuliza hatua hii ya mke wa Kafulila ni ya nini? Yaani sisi kama taifa tumefika sehemu mpaka mambo ya kisiasa yanatugawa hadi kwenye familia?
Hata kama Jesca hakuridhishwa na uamuzi wa mme wake alitakiwa amuunge mkono kwa uamzi wake ambao ni halali kikatiba na kumpa moyo wa kusonga mbele na kumtaka wapambane kwa hoja sasa. Lakini kitendo cha yeye kuitisha mkutano na wanahabari na kumkosoa mme wake kimemfanya aonekane bado sio mkomavu kisiasa.
Na kama hali ndio hii itafika wakati ili kuoa utakua unaulizwa chama cha kisiasa unachokikubali ni kipi ndio unaruhusiwa kuoa/kuolewa. Tusifike uko kama taifa tuanze kukataa hizi chuki zinazotaka kutugawa .
Wasalaaam