Mwanadada machachali wa chama cha democrasia na maendeleo bi Jesca kishoa maarufu kama (Iron Lad) jana tarehe 12.12.2013 amekamilisha na kukabizi taarifa ya uchunguzi wa unyang'anyi wa viwanja unaofanywa na mkurugenzi wa manispaa ya singida katika taarifa hiyo iliyoambatanishwa na miktasari ya vikao vilivyokaliwa na waanga wa tukio hilo imemtaja mwenyekiti wa ccm mkoa wa Singida kuhusika na uharamia huo ambapo wajumbe wamedai m/kiti huyo bwana Mgana msindai akishirikiana na mkurugenzi wa manispaa bwana Joseph mchina waliwahadaa wananchi na kuwataka wahame wakidai ni eneo la wazi na baadae wakamuuzia bwana Akwii mfanyabiashara wa mkoani hapa mwenyekiti wa ccm amekua na tabia ya kuingilia majukumu yasio yake kila wakati ususani kwenye mambo haya ya viwanja,itakumbukwa kua yeye ndiye alisababisha Singida kuwe na stand bubu nyingi baada yakuwaruhusu wenye mabasi kitendo ambocho mbali na kuweka mji katika mazingira machafu lakini pia inapoteza mapato ya manispaa kwa magari kutokufika stand kuu na badara yake mapato kwenda ccm kwa stand bubu kua nyuma ya ofisi zao