Jesca Kishoa aibua ufisadi mwingine wa shilingi Trilion 1.3 sakata la SONGAS

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
NAIBU waziri Kivuli wa Nishati na Madini na Mbunge wa Viti Maalumu, Jesca Kishoa (Chadema) amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndigai kumuita mwanasheria mkuu wa serikali kutokana na mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza maelekezo ya CAG ya kuwepo kwa ufisadi wa kutisha katika kampuni ya SONGAS.

Kishoa alisema kuwa tangu kuanza kwa mradi wa SONGAS mwaka 2004 hadi 2018 serikali imeisha poteza zaidi ya Sh. 1.3 trilioni na ifahamike kuwa mkataba huo unakoma mwaka 2024 na kama serikali serikali itapuuza itapoteza kiasi cha trilion mbili kwa kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

Mbali na hilo alisema kuwa anasikitishwa na serikali ya awamu ya tano ambayo imekuwa ikijipambanua kuwa inapambana na ufisadi katika miradi mbalimbali ya serikali lakini imeshindwa kuchukua hatua katika mradi wa kampuni ya SONGAS kutokana na kuingia mkataba wa kifisadi.

Kishoa alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kutokana na kauli ya Spika Ndugai kumwita Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa madai kuwa amelidhalilisha bunge kwa kuliita dhaifu wakati akihojiwa na kituo kimoja wapo cha utangazaji cha Umoja wa mataifa.

Kishoa alisema kuwa Kampuni ya SONGAS ni kampuni iliyoingia mkataba wa kifisadi na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mara kadhaa amekuwa akipiga kelele kama mbunge na kama waziri kivuli wa Nishati na madini lakini serikali imekuwa ikikaa kimya huku ikijinadi kuwa ni serikali ya kupambana na ufisadi.

“Nimewaita kuzungumza nanyi ili muweze kufikisha ujumbe kwa wananchi wa Tanzania kuhusu ufisadi mkubwa unaoendelea katika kampuni ya SONGAS, ni kampuni ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ili ingia mkataba na serikali ya Tanzania kwa kipindi cha miaka 20 kuanzia mwaka 2004 hadi 2024.

“Gharama za mradi wa SONGAS ilikuwa ni Euro 392 milioni, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mradi huo imetoa Euro 285.7 milioni sawa na asilimia 73 ya mradi mzima, huku kampuni ya SONGAS ikitoa Euro 106.3 milioni sawa na asilimia 27 ya mradi.


“Ufisadi katika mradi wa SONGAS upo katika maeneo matatu ambayo ni mfumo mzima wa uwekezaji na umliki wa mradi, makataba wa Capacity Charges,” alisema Kishoa.

Aidha alieleza kuwa serikali ya Tanzania inamiliki mradi kwa silimia 46 pekee yake na SONGAS inamiliki mradi kwa asilimia 54, na kama serikali iliwekeza asilimia 73 ya mradi mzima wa SONGAS iliwekeza asilimia 27 ya mradi mzima, inakuwaje SONGAS imiliki mradi kwa kiwango kikubwa wakati iliwekeza mtaji mdogo jambo ambalo linaonesha wazi kuwa ni wizi wa fedha za walipa kodi wa Tanzania.

Alisema kuwa kila mwezi Serikali ya Tanzania kupitia TANESCO imekuwa ikilipa SONGAS Capacity Charge ya dola 5 milioni ambapo Capacity Charge ni fedha za fidia anayopewa mwekezaji kufidia gharama aliyotumia kuwekeza, ambapo lengo kubwa la serikali kumiliki mitambo ya SONGAS baada ya mkataba kwisha.

Alieleza kuwa kila dola 5 milioni ya capacity charge inayotolewa kila mwezi na serikali kuipa SONGAS kuna dola 3.6 milioni zilitakiwa kwenda serikalini, lakini serikali inaipatia SONGAS fedha zote za fidia wakati serikali ndiyo iliyowekeza kwa kiasi kikubwa kuliko SONGAS.

“Kilichotufikisha katika hasara hii ya kifisadi ni udhahifu wa Bunge kwa sababu ufisadi huu ulishawahi kuzungumzwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini chini ya Mwenyekiti William Shelukindo mwaka 2005 kwenye taarifa yake Bungeni ukurasa wa 8, Ripoti ya CAG Ludovick Uttoh ya mwaka 2009 ukurasa wa 135, Ripoti ya CAG, Profesa Mussa Assad ukurasa wa 131 ya mwaka 2018 na mimi mwenyewe Naibu Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nilizungumzia suala hili zaidi ya mara tatu Bungeni lakini hakuna hatua zinazochuliwa na Bunge.

“Napenda kutoa rai yangu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Spika wa Bunge, waandishi wa habari na watanzania wote kwa ujumla, Rai yangu kwa Rais Dk. John Magufuli hasira zake alizotuonyesha katika ufisadi wa IPTL sasa ni muda mwafaka kuzionesha kwa SONGAS.

“Rai yangu kwa spika Job Ndugai mwanasheria mkuu wa Serikali (AG) aitwe mbele ya Kamati ya Maadili kwa kulidanganya na kulipuuza Bunge mbele ya kiti chake ndani ya Bunge na siyo nje ya nchi kwa kusema kuwa atalishughulikia suala la SONGAS ndani ya miezi miwili tangu Mei 5 mwaka 2018 lakini hadi leo hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Bunge lililopita nilihoji na hakunijibu,” alieleza Kishoa.

Katika hatua nyingine amewaeleza watanzania kuwa pamoja na yeye kuwa mume wake ambaye alikuwa mwana mageuzi na kuondoka na kujiunga na CCM na kupewa kazi na serikali lakini bado lakini yeye (Kishoa) anaendelea kupambana na kutetea maslahi ya wananchi kwa faida ya watanzania kwa ujumla.

Alisema kuwa ikumbukwe kuwa mume wake ambaye ni David Kafulila anaendelea kumuunga mkono (Kishoa) kwa juhudi zake za kupambana na ufisadi ndani ya serikali bila kujali kuwa yeye ni pinzani na Kafulila yupo serikalini.

SOURCES:
Mbunge Chadema amvaa Spika Ndugai, ampa kazi ngumu

BREAKING: Mke wa Kafulila aibua ufisadi wa mkubwa “Spika aachane na CAG” (+video) – Millardayo.com

Mke wa kafulila Aibua Ufisadi wa Trilion 1.3 Sakata la SONGAS
 
Natabiri ndani ya huu mwezi kutaibuka tukio la kufunika taarifa hizi labda kama la dr. Shika, konki n.k
 
0a15677bf4a425178cad8f692bf2a73b


WAZIRI Kivuli wa Nishati, Jesca Kishoa amemshauri Spika wa Bunge, Job Ndugai kumuita mbele ya Kamati ya Bunge na Maadili, Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa madai ya kulidanganya Bunge na kushindwa kufanyia kazi taarifa za Ufisadi unaendelea katika mikataba ya kampuni ya kuzalisha Umeme wa Gesi ya SONGAS badala ya kumuita Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG Profesa Assad kwa kusema maneno ya ukweli.

Kishoa ambaye ni mke wa aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini ( NCCR–Mageuzi ), ametoa Rai hiyo leo jijini Dodoma ambapo amesema ufisadi huo unaendelea na umebainishwa katika Ripoti ya CAG ya mwaka 2009 na ya mwaka 2018 ambapo Mwanasheria Mkuu waSerikali aliahidi mbele ya Bunge kua atalifanyia kazi ambapo mpaka sasa hajalifanyia kazi huku Bunge likishindwa kumuwajibisha.

Katika Ripoti hizo za CAG zilionyesha Tanzania mepoteza zaidi ya shilingi Trilion 1.3 na mikataba hiyo ikiendelea itapoteza zaidi hivyo Waziri huyo Kivuli pia ameomba Rais Magufuli kutumia Mahakama za Kimataifa katika swala hilo kama kwake limekua gumu ili kuokoa fedha za Watanzania.

Global publishers
 
Mwanasheria wa iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini (before split) na wasaidizi wake pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wawajibishwe.
 
NAIBU waziri Kivuli wa Nishati na Madini na Mbunge wa Viti Maalumu, Jesca Kishoa (Chadema) amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndigai kumuita mwanasheria mkuu wa serikali kutokana na mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza maelekezo ya CAG ya kuwepo kwa ufisadi wa kutisha katika kampuni ya SONGAS.

Kishoa alisema kuwa tangu kuanza kwa mradi wa SONGAS mwaka 2004 hadi 2018 serikali imeisha poteza zaidi ya Sh. 1.3 trilioni na ifahamike kuwa mkataba huo unakoma mwaka 2024 na kama serikali serikali itapuuza itapoteza kiasi cha trilion mbili kwa kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

Mbali na hilo alisema kuwa anasikitishwa na serikali ya awamu ya tano ambayo imekuwa ikijipambanua kuwa inapambana na ufisadi katika miradi mbalimbali ya serikali lakini imeshindwa kuchukua hatua katika mradi wa kampuni ya SONGAS kutokana na kuingia mkataba wa kifisadi.

Kishoa alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kutokana na kauli ya Spika Ndugai kumwita Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa madai kuwa amelidhalilisha bunge kwa kuliita dhaifu wakati akihojiwa na kituo kimoja wapo cha utangazaji cha Umoja wa mataifa.

Kishoa alisema kuwa Kampuni ya SONGAS ni kampuni iliyoingia mkataba wa kifisadi na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mara kadhaa amekuwa akipiga kelele kama mbunge na kama waziri kivuli wa Nishati na madini lakini serikali imekuwa ikikaa kimya huku ikijinadi kuwa ni serikali ya kupambana na ufisadi.

“Nimewaita kuzungumza nanyi ili muweze kufikisha ujumbe kwa wananchi wa Tanzania kuhusu ufisadi mkubwa unaoendelea katika kampuni ya SONGAS, ni kampuni ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ili ingia mkataba na serikali ya Tanzania kwa kipindi cha miaka 20 kuanzia mwaka 2004 hadi 2024.

“Gharama za mradi wa SONGAS ilikuwa ni Euro 392 milioni, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mradi huo imetoa Euro 285.7 milioni sawa na asilimia 73 ya mradi mzima, huku kampuni ya SONGAS ikitoa Euro 106.3 milioni sawa na asilimia 27 ya mradi.

“Ufisadi katika mradi wa SONGAS upo katika maeneo matatu ambayo ni mfumo mzima wa uwekezaji na umliki wa mradi, makataba wa Capacity Charges,” alisema Kishoa.

Aidha alieleza kuwa serikali ya Tanzania inamiliki mradi kwa silimia 46 pekee yake na SONGAS inamiliki mradi kwa asilimia 54, na kama serikali iliwekeza asilimia 73 ya mradi mzima wa SONGAS iliwekeza asilimia 27 ya mradi mzima, inakuwaje SONGAS imiliki mradi kwa kiwango kikubwa wakati iliwekeza mtaji mdogo jambo ambalo linaonesha wazi kuwa ni wizi wa fedha za walipa kodi wa Tanzania.

Alisema kuwa kila mwezi Serikali ya Tanzania kupitia TANESCO imekuwa ikilipa SONGAS Capacity Charge ya dola 5 milioni ambapo Capacity Charge ni fedha za fidia anayopewa mwekezaji kufidia gharama aliyotumia kuwekeza, ambapo lengo kubwa la serikali kumiliki mitambo ya SONGAS baada ya mkataba kwisha.

Alieleza kuwa kila dola 5 milioni ya capacity charge inayotolewa kila mwezi na serikali kuipa SONGAS kuna dola 3.6 milioni zilitakiwa kwenda serikalini, lakini serikali inaipatia SONGAS fedha zote za fidia wakati serikali ndiyo iliyowekeza kwa kiasi kikubwa kuliko SONGAS.

“Kilichotufikisha katika hasara hii ya kifisadi ni udhahifu wa Bunge kwa sababu ufisadi huu ulishawahi kuzungumzwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini chini ya Mwenyekiti William Shelukindo mwaka 2005 kwenye taarifa yake Bungeni ukurasa wa 8, Ripoti ya CAG Ludovick Uttoh ya mwaka 2009 ukurasa wa 135, Ripoti ya CAG, Profesa Mussa Assad ukurasa wa 131 ya mwaka 2018 na mimi mwenyewe Naibu Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nilizungumzia suala hili zaidi ya mara tatu Bungeni lakini hakuna hatua zinazochuliwa na Bunge.

“Napenda kutoa rai yangu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Spika wa Bunge, waandishi wa habari na watanzania wote kwa ujumla, Rai yangu kwa Rais Dk. John Magufuli hasira zake alizotuonyesha katika ufisadi wa IPTL sasa ni muda mwafaka kuzionesha kwa SONGAS.

“Rai yangu kwa spika Job Ndugai mwanasheria mkuu wa Serikali (AG) aitwe mbele ya Kamati ya Maadili kwa kulidanganya na kulipuuza Bunge mbele ya kiti chake ndani ya Bunge na siyo nje ya nchi kwa kusema kuwa atalishughulikia suala la SONGAS ndani ya miezi miwili tangu Mei 5 mwaka 2018 lakini hadi leo hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Bunge lililopita nilihoji na hakunijibu,” alieleza Kishoa.

Katika hatua nyingine amewaeleza watanzania kuwa pamoja na yeye kuwa mume wake ambaye alikuwa mwana mageuzi na kuondoka na kujiunga na CCM na kupewa kazi na serikali lakini bado lakini yeye (Kishoa) anaendelea kupambana na kutetea maslahi ya wananchi kwa faida ya watanzania kwa ujumla.

Alisema kuwa ikumbukwe kuwa mume wake ambaye ni David Kafulila anaendelea kumuunga mkono (Kishoa) kwa juhudi zake za kupambana na ufisadi ndani ya serikali bila kujali kuwa yeye ni pinzani na Kafulila yupo serikalini.

SOURCES:
Mbunge Chadema amvaa Spika Ndugai, ampa kazi ngumu


BREAKING: Mke wa Kafulila aibua ufisadi wa mkubwa “Spika aachane na CAG” (+video) – Millardayo.com

Mke wa kafulila Aibua Ufisadi wa Trilion 1.3 Sakata la SONGAS
sasa kama mkataba ni wa 2004 alikuwa wapi kusema aje kusema sasa?
na kwa nini akimbilie bunge la awamu ya tano kuwa dhaifu? bunge la awamu ya nne limekaa na huu mkataba mbovu kwa nini haliitwi dhaifu?
 
Sawa ufisadi huu ushuhulikiwe.Lakini hiyo isiwe sababu ya kutusahaulisha ile 1.5 trilion,na kishika uchumba chetu kutoka ACACIA

Ila hayo maelezo ya ziada ya kuhusu ndoa yake yanaleta ukakasi,sababu hayahusiani na hoja aliyoileta mezani

Alafu kuwa Mwanaharakati wa upinzani alafu mumeo yuko chama tawala ambacho ni cha kidhalimu nayo inaleta ukakasi vilevile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania tuziokoe fedha hizo zilete maendeleo yetu
NAIBU waziri Kivuli wa Nishati na Madini na Mbunge wa Viti Maalumu, Jesca Kishoa (Chadema) amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndigai kumuita mwanasheria mkuu wa serikali kutokana na mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza maelekezo ya CAG ya kuwepo kwa ufisadi wa kutisha katika kampuni ya SONGAS.

Kishoa alisema kuwa tangu kuanza kwa mradi wa SONGAS mwaka 2004 hadi 2018 serikali imeisha poteza zaidi ya Sh. 1.3 trilioni na ifahamike kuwa mkataba huo unakoma mwaka 2024 na kama serikali serikali itapuuza itapoteza kiasi cha trilion mbili kwa kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

Mbali na hilo alisema kuwa anasikitishwa na serikali ya awamu ya tano ambayo imekuwa ikijipambanua kuwa inapambana na ufisadi katika miradi mbalimbali ya serikali lakini imeshindwa kuchukua hatua katika mradi wa kampuni ya SONGAS kutokana na kuingia mkataba wa kifisadi.

Kishoa alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kutokana na kauli ya Spika Ndugai kumwita Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa madai kuwa amelidhalilisha bunge kwa kuliita dhaifu wakati akihojiwa na kituo kimoja wapo cha utangazaji cha Umoja wa mataifa.

Kishoa alisema kuwa Kampuni ya SONGAS ni kampuni iliyoingia mkataba wa kifisadi na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mara kadhaa amekuwa akipiga kelele kama mbunge na kama waziri kivuli wa Nishati na madini lakini serikali imekuwa ikikaa kimya huku ikijinadi kuwa ni serikali ya kupambana na ufisadi.

“Nimewaita kuzungumza nanyi ili muweze kufikisha ujumbe kwa wananchi wa Tanzania kuhusu ufisadi mkubwa unaoendelea katika kampuni ya SONGAS, ni kampuni ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ili ingia mkataba na serikali ya Tanzania kwa kipindi cha miaka 20 kuanzia mwaka 2004 hadi 2024.

“Gharama za mradi wa SONGAS ilikuwa ni Euro 392 milioni, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mradi huo imetoa Euro 285.7 milioni sawa na asilimia 73 ya mradi mzima, huku kampuni ya SONGAS ikitoa Euro 106.3 milioni sawa na asilimia 27 ya mradi.


“Ufisadi katika mradi wa SONGAS upo katika maeneo matatu ambayo ni mfumo mzima wa uwekezaji na umliki wa mradi, makataba wa Capacity Charges,” alisema Kishoa.

Aidha alieleza kuwa serikali ya Tanzania inamiliki mradi kwa silimia 46 pekee yake na SONGAS inamiliki mradi kwa asilimia 54, na kama serikali iliwekeza asilimia 73 ya mradi mzima wa SONGAS iliwekeza asilimia 27 ya mradi mzima, inakuwaje SONGAS imiliki mradi kwa kiwango kikubwa wakati iliwekeza mtaji mdogo jambo ambalo linaonesha wazi kuwa ni wizi wa fedha za walipa kodi wa Tanzania.

Alisema kuwa kila mwezi Serikali ya Tanzania kupitia TANESCO imekuwa ikilipa SONGAS Capacity Charge ya dola 5 milioni ambapo Capacity Charge ni fedha za fidia anayopewa mwekezaji kufidia gharama aliyotumia kuwekeza, ambapo lengo kubwa la serikali kumiliki mitambo ya SONGAS baada ya mkataba kwisha.

Alieleza kuwa kila dola 5 milioni ya capacity charge inayotolewa kila mwezi na serikali kuipa SONGAS kuna dola 3.6 milioni zilitakiwa kwenda serikalini, lakini serikali inaipatia SONGAS fedha zote za fidia wakati serikali ndiyo iliyowekeza kwa kiasi kikubwa kuliko SONGAS.

“Kilichotufikisha katika hasara hii ya kifisadi ni udhahifu wa Bunge kwa sababu ufisadi huu ulishawahi kuzungumzwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini chini ya Mwenyekiti William Shelukindo mwaka 2005 kwenye taarifa yake Bungeni ukurasa wa 8, Ripoti ya CAG Ludovick Uttoh ya mwaka 2009 ukurasa wa 135, Ripoti ya CAG, Profesa Mussa Assad ukurasa wa 131 ya mwaka 2018 na mimi mwenyewe Naibu Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nilizungumzia suala hili zaidi ya mara tatu Bungeni lakini hakuna hatua zinazochuliwa na Bunge.

“Napenda kutoa rai yangu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Spika wa Bunge, waandishi wa habari na watanzania wote kwa ujumla, Rai yangu kwa Rais Dk. John Magufuli hasira zake alizotuonyesha katika ufisadi wa IPTL sasa ni muda mwafaka kuzionesha kwa SONGAS.

“Rai yangu kwa spika Job Ndugai mwanasheria mkuu wa Serikali (AG) aitwe mbele ya Kamati ya Maadili kwa kulidanganya na kulipuuza Bunge mbele ya kiti chake ndani ya Bunge na siyo nje ya nchi kwa kusema kuwa atalishughulikia suala la SONGAS ndani ya miezi miwili tangu Mei 5 mwaka 2018 lakini hadi leo hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Bunge lililopita nilihoji na hakunijibu,” alieleza Kishoa.

Katika hatua nyingine amewaeleza watanzania kuwa pamoja na yeye kuwa mume wake ambaye alikuwa mwana mageuzi na kuondoka na kujiunga na CCM na kupewa kazi na serikali lakini bado lakini yeye (Kishoa) anaendelea kupambana na kutetea maslahi ya wananchi kwa faida ya watanzania kwa ujumla.

Alisema kuwa ikumbukwe kuwa mume wake ambaye ni David Kafulila anaendelea kumuunga mkono (Kishoa) kwa juhudi zake za kupambana na ufisadi ndani ya serikali bila kujali kuwa yeye ni pinzani na Kafulila yupo serikalini.

SOURCES:
Mbunge Chadema amvaa Spika Ndugai, ampa kazi ngumu

BREAKING: Mke wa Kafulila aibua ufisadi wa mkubwa “Spika aachane na CAG” (+video) – Millardayo.com

Mke wa kafulila Aibua Ufisadi wa Trilion 1.3 Sakata la SONGAS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom