Jerusalema Master KG

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,293
18,889
AFRIMMA imetoa list ya wanamuziki wa kupewa tuzo mwaka huu; mojawapo ni artist of the year. Sasa mwanamuziki Master KG wa south Africa, wimbo wake wa Jerusalema ni maarufu sana duniani kote sasa hivi kama hizo video zionekanavyo hapo chini, kwa hiyo kulikuwa hakuna haja ya kumshindanisha na wanamuziki wengine tena kwa vile kazi yake imeheshimiwa sana.

1600019822444.png



















 
Kqakweli aliyekaa na kusuka hilo biti la huo wimbo alitulia akili sasa changanya na hiyo sauti kama ya wanyakyusa akina bahati kukuku ndio wimbo unakuwa mtamu zaidi
Utunzi wa wimbo hauhitaji kipaji tu bali pia utaalamu wa muziki kuweza kufanya muziki huo kuwagusa watu wengi. Nimekuwa nafuatilia nyimbo nyingi za wasanii wetu (mimi ni mpenzi wa muziki na nina mafunzo ya muziki) wanatoa nyimbo za kufurahisha watu papo kwa papo bila kuplani long term impact. Nyimbo nyingi zinazoitwa singeli ni nyimbo za hovyo sana kuacha impact ingawa zinakubaliwa haraka haraka ila pia husahaliwa mapema pia.
 
sana
Kqakweli aliyekaa na kusuka hilo biti la huo wimbo alitulia akili sasa changanya na hiyo sauti kama ya wanyakyusa akina bahati kukuku ndio wimbo unakuwa mtamu zaidi
Wimbo bwana unabebwa na beat 50% wakati mwingine 80% beat
south nyimbo zao nyingi Beats mtu anaweza asiimbe ukaskia beat tu tayari mziki na una trend
Bongo maproducer bado, Tudd alikuaga mkali....Tecno anagonga sana beat kali kwenye nyimbo zake /Davido
 
Nasikia ni nyimbo ya dini
Siyo wimbo wa dini pase; anasema tu kuwa jerusalem ndiyo nyumbani kwangu, unilinde usiniache. Hilo ndilo shair lenyewe. Ila sana ametumia melodic contour nzuri sana inayoingia kichwani mwa mtu yeyote kirahis na kwa ndani sana, halafu ridhim yake ni ya kustarehesha wakati huyo mama mwimbaji wake naye sauti iko poa sana. Ndiyo maana wimbo umepokelewa dunia nzima. Pamoja na kuwa tayari ina clones nyingi sana Yutube ambazo zimeshasikilizwa zaidi ya milioni mia moja, ile copy ya original ina watazamaji zaidi ya milioni moja na laki tatu, kwa hiyo wimbo wote una watazamaji zaidi ya milioni mia mbili na nusu ndani ya miezi tisa tu.
 
sanaWimbo bwana unabebwa na beat 50% wakati mwingine 80% beat
south nyimbo zao nyingi Beats mtu anaweza asiimbe ukaskia beat tu tayari mziki na una trend
Bongo maproducer bado, Tudd alikuaga mkali....Tecno anagonga sana beat kali kwenye nyimbo zake /Davido
Ingekuwa rahisi hivyo mbona ingekuwa poa.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom