Jerry Silaa: Serikali iwe na utaratibu mzuri wa kufanya uthamini na kulipa wananchi

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Jerry Silaa, ameitaka Serikali kuweka Utaratibu mzuri wa kufanya uthamini na kulipa Wananchi kwa wakati akisisitiza lazima Fedha ziwe zimeshatengwa wakati uthamini unafanyika

Wakati wa Majadiliano ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, amesema "Mara nyingi uthamini unafanyika lakini Taasisi inayoagiza hivyo hata Fedha kwenye Bajeti haijatengewa. Matokeo yake Uthamini unafanyika, Fidia zinachelewa na Wananchi wanapata shida"
 
Binafsi nilifanyiwa uthamini kwenye eneo langu Kinyerezi mwaka 2017na TANESCO kuwa kuna mradi wa umeme mkubwa unapita. Nilikiwa nimeanza ujenzi wa nyumba nikiwa nimemwaga jamvi. Nikaambiwa nisiendeleze. Mpaka leo hii sijalipwa fidia na tanesco wanasisistiza mradi upo na tusiendeleze.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom