MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Mimi ni kada kindakindaki wa Chama cha mapinduzi lakini ningeomba katika andiko langu nichukuliwe kama mzalendo anayependa maadili ndani ya chama na serikali ya Mama yetu mpendwa. Kama DC Muro ana wapambe wake humu na itawagusa basi wacha iwaume lakini wajifunze.
Jerry Muro binafsi nimekua nikifuatilia kauli zake za kujiapia kupoteza watu wanaompinga yeye, kujiapia kutotangaza majina ya washindi wa uchaguzi, Yeye kama nani?wakati DC hatakiwi kukaribia milango ya vituo vya wapiga kura? Ndani ya CCM ni lini tutawamaliza kina Sabaya hawa ili chama hiki kiwe chama cha watu? DC anapata wapi ujasiri wa kuwaambia kinamama watabaki wajane? Yeye ataishi milele? Kwani mke wake hawezi kua mjane siku moja?
Ninamuomba Rais wangu kipenzi Samia Suluhu Hassan ambaye nimetokea kumwelewa sana kuliko Marais wote waliopita ukimtoa Mwl Nyerere, amtazame sana hatua kwa hatua ndugu Jerry Muro hata kwenye uadilifu wake juu ya usimamizi wa rasilimali za umma na utendaji wake kwa ujumla. Ni mtu ambaye mabega yako juu wakati wote, ndani ya chama hatutaki hii tabia na mwisho wake si mzuri.
Nimuombe tu DC Muro aache tabia hizi, serikali hii ni ya wananchi siyo yake. Wenye kutoa hukumu juu ya utekelezaji wa ilani ya chama ni Wananchi na siyo yeye. Asimwakilishe Rais wetu vibaya akalaumiwa.
Jerry Muro binafsi nimekua nikifuatilia kauli zake za kujiapia kupoteza watu wanaompinga yeye, kujiapia kutotangaza majina ya washindi wa uchaguzi, Yeye kama nani?wakati DC hatakiwi kukaribia milango ya vituo vya wapiga kura? Ndani ya CCM ni lini tutawamaliza kina Sabaya hawa ili chama hiki kiwe chama cha watu? DC anapata wapi ujasiri wa kuwaambia kinamama watabaki wajane? Yeye ataishi milele? Kwani mke wake hawezi kua mjane siku moja?
Ninamuomba Rais wangu kipenzi Samia Suluhu Hassan ambaye nimetokea kumwelewa sana kuliko Marais wote waliopita ukimtoa Mwl Nyerere, amtazame sana hatua kwa hatua ndugu Jerry Muro hata kwenye uadilifu wake juu ya usimamizi wa rasilimali za umma na utendaji wake kwa ujumla. Ni mtu ambaye mabega yako juu wakati wote, ndani ya chama hatutaki hii tabia na mwisho wake si mzuri.
Nimuombe tu DC Muro aache tabia hizi, serikali hii ni ya wananchi siyo yake. Wenye kutoa hukumu juu ya utekelezaji wa ilani ya chama ni Wananchi na siyo yeye. Asimwakilishe Rais wetu vibaya akalaumiwa.