Tetesi: Jerry Muro na William Malecela ndani ya mpango wa hatari wa kuidhibiti timu ya Fiesta

mapessa

JF-Expert Member
Oct 9, 2014
612
1,045
Kuna mpango mkakati ulioundwa na Team ya Makonda kwa ajili ya kuidhibiti timu ya Fiesta katika mkoa wa Dar es salaam. Makonda na wenzake wana mkakati juu ya mpango wa kuharibu show ya Fiesta Kwa hali na mali siku ya Tarehe 25-11-2017.

Wanamkakati wa Mtandao huo wakiongozwa na Jerry Muro pamoja William Malecela (Lemutuz) wametajwa kuunda kikosi cha mipango wa kuvuruga show ya Fiesta. Habari hizi zimekuja baada ya juzi kugomea mahojiano ya kushirikiana na waandaji wa Fiesta.

Leo asubuhi majira ya saa tano William Malecela (Lemutuz) alionekana katika vituo tofauti vya Bodaboda cha Mbuyuni, Salasala Manzese Darajani pamoja na Kigogo alionekana akizungumza na baadhi ya vijana wa Bodaboda ambao amewahaidi kuwapa Mafuta Kwa ajili ya kusindikiza msafara wa mkuu wa mkoa akienda katika show aliyoianda siku ya Jumamosi na kituo cha redio cha EFM.

Lengo la kuandaa msafara ni kutaka kuonyesha kuwa ni mtu anayependwa sana na kituo cha EFM kinakubalika kuliko kituo cha Clouds Fm.

Wawili hawa (Lemutuz na Jerry Muro) wanatajwa kuwa ni wanamkakati ambao walipendekeza na kushauri mpango wa kuharibu Fiesta pamoja na mzito huyo.

Zoezi lingine lililopangwa katika siku hiyo ya Jumamosi na Timu hiyo ya Waovu ni kuwaleta vilema waliokosa miguu kuwa wanafunzi wenye ulemavu na wapatiwe bure.

Majina yao ni
Zainab Hamissi
Sultan Gonga
Bahati Ally
Advera Shoo
Juma Ally
Aisha Mkoba
Mwanamvua Mkambara
Shukuru kuyoha
Mwidadi Mapunga

Jambo hilo limeratibiwa pia na baadhi ya waandaji wa kipindi cha Joto la Asubuhi kupitia kwa ndugu Abel Onesmo zoezi hili uwepo wake ni wa Siri sana kutoka kwa kiongozi huyo mkuu wa mkoa.

Majina ya wanamkakati wengine ambao walikutana katika kikao cha Jana usiku Masaki Kwa mkuu wa Mko ni hawa wafuatao;

1. Omar Ali Shehe (TRA)
2. ACP Emmanuel kilerwa
3. Abdilahi Jihad (NON)
4. Said Ally Mbarouk (NON)
5. Jeniffer Mpangala (TRA)

Kikao kilichofanyika jana usiku Nyumbani Kwa Mhe. Walijadili kuhusu ukaguzi wa Vifaa vitakavyotumika katika Fiesta na matumizi ya risiti za EFD. Jambo kingine walijadili kuhusu kipindi cha Joto la Asubuhi ambapo kitaruka kesho tarehe 17-11-2017.

Makonda atakuwa anahojiwa kuelezea habari za mabahari na show ya wanafunzi ya bure waliyoianda siku ya Jumamosi kingine ni kuhusu zoezi la ugawaji miguu mabandia.

Kuna hatihati ya mtangazaji wa EFM kusimamishwa kutokana na kupingana na ujio wa Mkuu wa Mkoa katika kipindi hicho.

Siri imevuja...!
HUWEZI KUSHINDA VITA UKIWA NA NJAA.


Upepo mbaya wa kisiasa unamyemelea bwana mkubwa mmoja na hii huenda ni kutokana na ushauri mbaya anaoupata toka kwa marafiki zake kwa nje ilhali ndani wakiyachukia mafanikio yake na kumtakia mabaya yamfike!

Nimejaribu kufuatilia na kufanyia tathmini ya yanayoweza kujitokeza siku ya tukio la fiesta na baada ya siku hiyo nikaona ni bora nimtaadharishe 'boss mtoto' huyo kwa kuwa nampenda na sipendi nyota yake ya kisiasa ikafia njiani.

Boss mtoto bado ni kijana mdogo na tunamuhitaji katika utumishi wa uma. Hivyo ninachukua nafasi hii kumtaadharisha aachane kabisa kujihusisha kwa namna yeyote ile na haya mambo ya fiesta. Tena ikiwezekana siku hiyo asafiri nje ya mkoa ili upepo mbaya upite.

Ni hivi, kutokana na maagizo ya boss mtoto, polisi wataweza kuingilia kati kuhakikisha tukio la fiesta linakwisha itakapotimu saa sita kamili. Kumbuka muda huo kwenye mkusanyiko wa fiesta kutakuwepo na mkusanyiko kama wa watu elfu ishirini na zaidi WALIOLEWA pombe!

Kitendo cha polisi kuingilia mkusanyiko huo huenda kikasababisha stampede (mkanyagano) na hali hiyo inaweza kusababisha vifo vinavyokadiriwa kuwa kati ya 60-120!

Tukio hilo litakuwa ni baya na la aina yake kuwahi kutokea hapa nchini na hili litazua hasira kali ya wananchi ambao watashinikiza bosi mtoto ang'olewe mara moja.
Kumbuka kuwa, polisi wamekuwa wakizima vurugu uwanja wa taifa wenye watu kadiri ya elfu sitini bila shida kutokea, ila hawa wa fiesta ni watu waliokwishalewa pombe mida hiyo ya usiku. Kwa hiyo, sanity ni kitu adimu uwanjani hapo.

Nimeshawahi kukaa baa. DJ anazima mziki na watu hawataki kuondoka. Wao wameshajipanga kukaa hapo mpaka kukuche. Kwa hiyo, hata mawingu wakizima muziki muda huo, am sure mashabiki hawatokubali kuondoka kwa hiyari kwa kuwa kiu yao bado itakuwa haijakwisha. Kwa hiyo kitendo cha kuwaondoa kwa nguvu, kitakuwa ni janga kubwa kuwahi kutokea kwenye historia ya mikusanyiko ya nchi hiii!

Na hata ukisema kuwa mziki uwahi kuzimwa, Mawingu watakuwa wameshatengeneza pesa yao upfront. Kuwahi kumaliza au kuchelewa kumalizika kwa tukio, haliwatii hasara yeyote mawingu studio kwa sababu wao tayari wameshalamba kiiingilio chao.

Ninamshauri boss mtoto afunike hili kombe ili mwanaharamu apite. Huu ni upepo mbaya sana kwake na akicheza nao, unaweza kumuondoa vibaya sana. Kwa hiyo kwa sababu nampenda, nimeona tu nimtaadharishe up front kabla mambo hayajamwaribikia tena.
 
Kuchonganisha jamii siyo jambo jema.

Kwa nini, fiesta wasichukue hatua ya kuvuka dar au kuiondoa kabisa Dar kwenye ratiba yao na kuendelea na mikoa mingine ambako fiesta ina kubarika na viongozi au uongozi wa mikoa hiyo!?

Btw, kila jambo lina umuhimu wake ila fiesta siyo muhimu hata ikikosekana kila mwaka hadi kipindi cha miaka mi tano 5 bado hakutakuwa na faida au hasara kubwa ya moja kwa moja maana zaidi fiesta ni starehe zaidi.
 
Back
Top Bottom