Jerry Muro aipigia magoti TFF, akiri wazi anavyoisoma namba

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,024
24,374
Yule aliyekuwa msemaji wa club ile yenye makazi yake katika eneo maarufu mitaa ya jangwani inayosifika kuwa na boti za mwendo kasi wa hali ya juu hasa wakati wa mafuriko, amejitokeza hadharani kutoka alikokuwa amejificha na kuomba kurudi kwenye kibarua chake ili aweze kupata mahitaji yake muhimu kama binadamu wengine

Ikumbukwe mropokaji huyu alipewa adhabu ya mwaka mmoja, na hadi kufikia hivi sasa imetimia miezi sita ya adhabu yake.
8f0ffb8d0493eaaa120d6d06daae7157.jpg

Juu ni barua aliyoiandika ili kuweza kupata huruma ya utukufu wa TFF.

Bila shaka hatua ya kufanya hivyo imetokana na kauli ya Manara alipotaka aombe msamaha ili arudi kwenye mstari kwa kuwa atakuwa ameshaelewa jinsi mpira unavyoendeshwa.

My take; Muro mpira siyo siasa wala uropokaji, mpira ni taaluma. Kuwa msemaji wa club haihitaji kuzungumza maneno ya taarabu, muone mwenzio Manara mheshimu sana. Othewise upigwe ban ya miaka 70.
 
Msamaha anapaswa kuombwa Mwenyezi Mungu tuu, kuomba omba msamaha kwa binadam mwenzako na hasa unakuwa umeonewa au kunyanyaswa ni kitendo cha uoga na unyonge, over!
 
Huyo mropokaji alinifanya niongeze chuki kwa kandambili kutokana na maneno yake ya khanga kwa klabu bora Africa Mashariki...Mnyama mkali...
Simba ....

Walisamehe tu...nadhani litakuwa limejifunza kuacha kuropoka ropoka...nyambafu
 
Hizi ni habari mbaya sana kwa wale wa Matopeni FC.
Jamaa anawapigia magoti TFF ili aendelee na kusababisha mapovu povu midomoni mwa watu fudenge wa Mchangani FC.
Nasema tena, hizi ni habari mbaya sana kwao.

watakuja hapa kujifanya kukebehi kitendo cha kuwapigia magoti TFF. Chimbeni mahandaki ya kujifichia, maana hapato kuwa na mahala pa kuweka sura zenu tena.

si mnamjua Jerry lakini! Msiniulize mimi, Muulizenu mleta mada awaambie kwanini amebadilisha Heading ya habari ili ilete taswira tofauti na ile iliyokusudiwa na mtoa taarifa hii ya awali.



Ni habari njema sana kwetu sisi, Jerry endelea kuwapigia magoti tu. Likizo uliyo wapa haya wa Matopeni nFC imetosha sasa. Nakumbuka enzi zile ulipokuwa pilipili midomoni na vichwani mwao.

Rudi Kijana Rudi.
 
Msamaha anapaswa kuombwa Mwenyezi Mungu tuu, kuomba omba msamaha kwa binadam mwenzako ni kitendo cha uoga na unyonge, over!
Hapana mkuu si kweli, kuna sala inamaneno haya "tusamehe makosa yetu kama tunavyosamehe na sisi"
Hivyo kabla ya kumuomba Mungu msamaha inabidi sisi tusameheane kwanza, ndipo tuombe msamaha kwa Mungu!!
 
Hizi ni habari mbaya sana kwa wale wa Matopeni FC.
Jamaa anawapigia magoti TFF ili aendelee na kusababisha mapovu povu midomoni mwa watu fudenge wa Mchangani FC.
Nasema tena, hizi ni habari mbaya sana kwao.

watakuja hapa kujifanya kukebehi kitendo cha kuwapigia magoti TFF. Chimbeni mahandaki ya kujifichia, maana hapato kuwa na mahala pa kuweka sura zenu tena.

si mnamjua Jerry lakini! Msiniulize mimi, Muulizenu mleta mada awaambie kwanini amebadilisha Heading ya habari ili ilete taswira tofauti na ile iliyokusudiwa na mtoa taarifa hii ya awali.



Ni habari njema sana kwetu sisi, Jerry endelea kuwapigia magoti tu. Likizo uliyo wapa haya wa Matopeni nFC imetosha sasa. Nakumbuka enzi zile ulipokuwa pilipili midomoni na vichwani mwao.

Rudi Kijana Rudi.
Akirudi akileta tena ujinga na maneno ya shombo atakula tena ban tu!
Kama ni mipasho asilete ile ya akina Amina na Asha..
Mipasho ya soka ndio mpango mzima!!
 
Huyo mropokaji alinifanya niongeze chuki kwa kandambili kutokana na maneno yake ya khanga kwa klabu bora Africa Mashariki...Mnyama mkali...
Simba ....

Walisamehe tu...nadhani litakuwa limejifunza kuacha kuropoka ropoka...nyambafu
Kweli mkuu, huyu jamaa alikuwa kila akiongea lazima upate kichefuchefu!!
 
Akirudi akileta tena ujinga na maneno ya shombo atakula tena ban tu!
Kama ni mipasho asilete ile ya akina Amina na Asha..
Mipasho ya soka ndio mpango mzima!!
Mipasho kwa TFF ndio atayapinguza,na ndicho kilichomfanya afungiwe . Hajafungiwa kwa sabbau ya maneno dhidi ya simba sc.

keep it in mind.
 
Mipasho kwa TFF ndio atayapinguza,na ndicho kilichomfanya afungiwe . Hajafungiwa kwa sabbau ya maneno dhidi ya simba sc.

keep it in mind.
Amefungiwa kwa kukataa kulipa faini ya milioni 5 mwaka 2015 kwa kutoa kashfa dhidi ya TFF. Shtaka la pili kwa kuhamasisha mashabiki wa Yanga wawafanyie vurugu wa Simba katika mchezo dhidi ya TP Mazembe na Yanga kufungwa goli 1.Shtaka la tatu la kupinga mkataba wa matangazo na Azam TV alishinda.
 
Mipasho kwa TFF ndio atayapinguza,na ndicho kilichomfanya afungiwe . Hajafungiwa kwa sabbau ya maneno dhidi ya simba sc.

keep it in mind.

Hata na hivyo, endapo akirejea akitoa maneno yasiyo na staha kwa club yoyote lazima hatua stahiki zichukuliwe dhidi yake, siyo lazima iwe simba tu!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom