Jerry Mulo ahojiwa na polisi Iringa

tz1

JF-Expert Member
Mar 19, 2011
2,121
534
Jerry aliwekwa chini ya ulinzi wa polisi na kuhojiwa kwa masaa matano.Inasemekana alikuwa anatokea Dar kuelekea Mbeya na bus la Sumry leo saa tano na alipofika check point ya Iringa alishuka kwenye bus na kutaka kuwapiga picha trafik polisi, ndipo alipokamatwa na kupelekwa kituoni na kuhojiwa.

Aliachiwa huru mida ya saa kumi jioni.

Source francisgodwinblog
 
Tatizo la nchi hii ukifichua mabaya lazima uzushiwe tu..manake the whole system is rotten to its totality...hapa Mungu tu awasaidie wtz
 
Jerry aliwekwa chini ya ulinzi wa polisi na kuhojiwa kwa masaa matano.Inasemekana alikuwa anatokea dar
kuelekea mby na bus la sumry leo saa tano na alipofika check point ya iringa alishuka kwenye bus na kutaka
kuwapiga picha trafik polisi,ndipo alipokamatwa na kupelekwa kituoni na kuhojiwa.Aliachiwa huru mida ya
saa kumi jioni.Source francisgodwinblog
huyo dogo ataumia sana au atapotea. Asishindane na vyombo vya usalama vina nguvu nyingi. Atafute umaarufu kwa njia nyingine, sio polisi. Ohooo!acha aendelee mie nitayasikia mengine yakimtokea!
 
Mwacheni afanye kazi yake mnaoponda naona mnaongea msichokijua...
Ipo siku mwenzenu mtamuona yupo BBC, SKY NEWS kwa sababu anajituma na ni jasiri
 
Jerry aliwekwa chini ya ulinzi wa polisi na kuhojiwa kwa masaa matano.Inasemekana alikuwa anatokea dar
kuelekea mby na bus la sumry leo saa tano na alipofika check point ya iringa alishuka kwenye bus na kutaka
kuwapiga picha trafik polisi,ndipo alipokamatwa na kupelekwa kituoni na kuhojiwa.Aliachiwa huru mida ya
saa kumi jioni.Source francisgodwinblog

Jerry nae,haya bwana....ngoja tuone.Hivi ile kesi yake imefikia wapi wakuu?
 
huyo dogo ataumia sana au atapotea. Asishindane na vyombo vya usalama vina nguvu nyingi. Atafute umaarufu kwa njia nyingine, sio polisi. Ohooo!acha aendelee mie nitayasikia mengine yakimtokea!

Mkuu acha uoga usio na tija,hakuna nchi iliyokombolewa na watu legelege,waoga hata kuhoji mambo yakawaida tu....utaishia kuongea hivo na utabakia na umaskini wako wa kukutosha kabisaa...
 
huyo dogo ataumia sana au atapotea. Asishindane na vyombo vya usalama vina nguvu nyingi. Atafute umaarufu kwa njia nyingine, sio polisi. Ohooo!acha aendelee mie nitayasikia mengine yakimtokea!
kijana unakuwa mwoga namna hiyo??
Huwezi kufanikiwa kama kila ndoto yako inaishia kuzimwa na mazimwi kama hawa na unawaachia tu!!
Success haiji kwa kuwa muoga kiivo mkuu!!
 
Jeri ni moja kati ya waandishi wa habari wenye ujasiri na uelewa wa hali ya juu sana! Ni mtu asiyekata tamaa! Ni mtu anayerisk maisha yake kutafuta habari! Ananyanyaswa kwa sababu ya mfumo mbovu wa uongozi ambao wamehanisi nchi so watu kama hawa hawawataki make wanaanika issue zao! So jery namtabiria kufika mbali sana tena sana!dunia inaona na mungu anaona!
 
Hongera Kaka komaa nao hao Maafande hadi kieleweke. Maana wanapenda sana uonevu wa raia wenye kipato kidogo.
 
Kila kazi ukitaka ikutoe ni lazima ukomae,na ukikomaa na kazi yako ilimradi inalenga kuwakomboa viumbe wa Mungu basi utawini si hapa tu bali hata Mbinguni utaenziwa na siku moja familia yako yaweza kurudishiwa baraka tele...Muro Mungu akutangulie na siku moja ukazidishiwe katika kila lililo jema.
 
Back
Top Bottom