Mwifwa
JF-Expert Member
- Apr 3, 2017
- 46,881
- 122,124
Kuoa mapema au sio mapema, nazani sio tatizo. Tatizo ni kupambana na kuwa na upeo wa hayo mapambano ya kujikwamua. Wenzetu wakiwa wanapambana wanakuwa serious wanafikia malengo yao, ni tofauti na sisi.Sisi huku tunazaa huku mtu anawaza akizeeka mtoto aje amtunze tena anashika na calculator kabisa nakujisemea moyoni "ukioa na miaka 27 ukifikisha miaka 60 mtoto ana miaka 33" tunasahau kila kitu ni mipango na unaweza kuoa mapema na hata usivuke 40 tayari UVIKO 19 inakuondoa
Sisi ukifanikiwa kidogo, unajiona Dunia ni yako pekee unaanza kuonja na kustarehe kwa kila jambo mwishowe unaanguka. Hilo ndio janga kubwa kwetu sisi.
Endapo tungekuwa na mitazamo kama ya wenzetu au hata kukaribiana tungekuwa katika raiti traki!