Jenister Mhagama - Waziri Mtiifu ambaye hakujali wa chini zaidi ya cheo chake

Tila-lila2

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
653
1,058
Amini usiamini angekuwa ni Waziri Mwanaume pale asingedumu vile. Jenister Mhagama amedumu kwa sababu hakuwa na uwezo wa kutofautiana na Waziri Mkuu hata Rais kuhusu maslahi ya wafanyakazi.

Ni Waziri gani angekubali miaka mitano ya uongozi wake wafanyakazi wa nchi hii wasipate nyongeza ya mishahara? Ni Waziri gani huyo mwenyewe kujiamini akubali hilo?

Magu mjanja sana - alimweka Jenny pale makusudi kabisa! Ukweli Jenny ni Mwanasiasa makini kwa maana ya siasa kweli. Huwezi kuamini kama elimu yake ni Diploma tu ya Ualimu. Jenny ni mtekelezaji mzuri wa maelekezo ndiyo maana alidumu pale. Ni msomaji mzuri wa trends za watakayo wakuu! Hana reasoning yake binafsi - attitude yake ni kutetea hata lisilo jema.

Ni mara moja tu alijaribu kutetea uamuzi mzuri wa Serikali wa kuunganisha mifuko ya pensheni. alitoa maneno yake pale Ikulu lkn bado hayakuzaa kitu ingawa yaliokoa asitumbuliwe kwani tayari Mkulu alikuwa kishaamua kuiharibu sekta ya hifadhi ya jamii kwa sababu ya kuzitaka fedha za mifuko.

Dada na Mheshimiwa Waziri wa Nchi Jenny kama utasoma hii thread jua kuwa huna la kujivunia katika miaka yako mitano kwamba uliboresha hali za wafanyakazi. Wewe ni Waziri uliyeumiza wafanyakazi kuliko Mawaziri wote waliowahi kusimamia jukumu hilo katika nchi yetu. U

kirudishwa nafasi hiyo na ukaendelea hivyo hivyo basi mtakuwa mnaunda nchi ya kidikteta kwani wafanyakazi hawatakuwa na uhuru wa kusikilizwa kuhusu maslahi yao kwa miaka kumi.

Mwenyezi Mungu wetu ni mwema na ni kweli anakuona!
 
Ni waziri gani huyo asiyekubali kufuata maelekezo ya bosi wake na kupingana naye?
 
Hivi Wabunge na mawaziri wanakatatwa 15% bodi ya Mkopo? Au walikimbia Umande.

Maana Naona Bunge la Tanzania Ya Baadae Kujaa wadaiwa wa Mikopo halafu tuone kama Hawatajadili hiyo 15% ambayo mtu anadaiwa Maisha Yake Yote
 
Huyu dada nin zero alizunguka na gari la Serikali nchi nzima huku akilamba per diem kufanya semina na kutetea sheria mpya ya kikokotoo Cha WATUMISHI WA UMMA ikiwa wao ikawa haiwahusu.

Ule ulikuwa uhujumu uchumi, zile pesa za posho, mafuta na per diem za dereva kuzunguka nchi nzima kutetea upuuzi anatakiwa azirudishe
 
Tila-lila2,

Hivi kutekeleza majukumu bila kutumia akili yako na ukweli nayo ni Sifa? Huu ulimwengu sijui unaenda wapi! Hiyo hata bata anafanya akielekezwa vizuri!
 
Wakati mwingine tusiwalaume hawa mawaziri, hivi Wizara ya Afya wakati wa corona aliyokuwa anafanya jiwe kuna haja ya kumlaumu Ummy, watu walikuwa wanamhurumia Ummy kwa kazi ya maagizo anayofanya. Wa kulaumiwe ni jiwe kuhusu kila kitu
 
Wakati mwingine tusiwalaume hawa mawaziri,hivi wizara ya afya wakati wa corona aliyokuwa anafanya jiwe kuna haja ya kumlaumu Ummy,watu walikuwa wanamhurumia Ummy kwa kazi ya maagizo anayofanya.Wa kulaumiwe ni jiwe kuhusu kila kitu
Angejiuzuru Kama hakuwa huru kutimiza majukumu yake
 
Serikali ya awamu ya tano kwa ujumla wake haikuwa na tija yoyote ile kwa Wafanyakazi. Ni moja ya Serikali ya hovyo sana kuwahi kuishuhudia ndani ya miaka zaidi ya 10 ya utumishi wangu wa umma.

Madaraja wanapandisha kwa kusuasua na kwa kutofuata utaratibu, hakuna nyongeza ya mshahara, wameongeza makato ya bodi, wanatishatisha wafanyakazi kana kwamba wana msaada wowote ule kwao, na wakati ni useless tu!

Kwenye hii miaka 5 ijayo, wajiandae tu kwa hujuma kutoka kwetu. Ni mwendo wa kujiongeza tu kwa sasa na kufanya kazi chini ya kiwango. Na hii ndiyo dawa kwa Mwajiri yeyote yule asiyejitambua na asiyetambua haki za Waajiriwa wake.

Mara zote sababu zao ni za hovyo hovyo tu! Eti tunanunua ndege kwanza! Sasa hao wafanyakazi watakula hizo ndege!!! Wafanyakazi kote duniani wanahitaji mishahara inayokidhi mahitaji yao na ndipo watakapofanya kazi kwa ari na moyo. Ukiwaletea siasa na wao watagoma moja kwa moja, au chini kwa chini.
 
Awamu hii sijaona Waziri wote walikuwa bendera fata upepo na kusifu sifu tuu.

Waziri mkuu makonda ndo Alikuwa anajitutumua alifanikiwa kumfukuzisha kazi nape. Alifanikiwa kuvamia clouds.
 
Back
Top Bottom