Jengo walilopanga CHADEMA kama Ofisi, Mtaa wa Ufipa Kinondoni ni la Nani na kodi yake ni kiasi gani?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
DSC00086.JPG


Baada ya kusikia habari kuwa CHADEMA wana mpango wa kujenga Chuo cha Maadili ya viongozi kwa heshima ya Bw. Sabodo aliyeahidi kuwachangia shilingi 150 nimejikuta nikitamani kunyofoa nywele zangu kichwani. Kati ya vitu vya kwanza ambavyo ninaamini Chadema wanahitaji kwa haraka zaidi ni makao makuu ya kisasa ya chama kinachojiandaa kutawala.

Ninaposema "makao makuu ya kisasa" nina maana ya jengo na mazingira yanayoendana na hadhi ambayo Chadema imejijengea sasa hivi lakini vile vile mahali ambapo kuna miundombinu ya kisasa vile vile. Lakini zaidi pia kujenga makao makuu ambayo hayatokuwa ofisi tu bali pia sehemu ya kitega uchumi.

Wapo wanaofikiri kula makao makuu sii kitu cha muhimu au si jambo la haraka kabisa. Wanafikiri wataendelea kujiandaa kushinda kwa kutumia vibanda vya nyasi na kutoa matangazo ya mipango yao kutoka uani! Chadema kama kinataka kianze kujipanga kiukweli sasa basi la kwanza ni kuandaa a modern command center. Nitawaachia wengine wafikirie makao makuu ya kisasa yaweje.

Lakini ukiniuliza mimi.. kati ya vitu vya kwanza kabisa vya kujiandaa na vitatupa mwanga kuwa sasa kweli CHadema inataka kushinda utawala wa nchi ni jinsi gani inajiandaa kwa makao yake makuu na kutoka hapo ofisi zake za ngazi za chini. Wakijenga hayo makao makuu basi wanaweza kuwa na sehemu ya mafunzo ambapo mafunzo ya maadili na mengine yataweza kutolewa.

======
Jan 8, 2014
WanaJF,

Ni takribani mwaka mmoja na nusu sasa tangu Mfanyabiashara maarufu nchini ndugu Sabodo kuahidi kuwa atasaidia kwa hali na mali katika ujenzi wa ofisi za makao makuu ya CHADEMA.

Ndugu Sabodo alitoa ahadi hiyo alipokuwa amealikwa na CHADEMA katika hafla fulani ambapo alisema kwamba pamoja na kwamba yeye ni kada wa CCM lakini ana imani kubwa na CHADEMA na kwenda mbali zaidi kuitabilia ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Kutokana na imani yake kwa CHADEMA, Ndugu Sabodo aliahidi kuisaidia CHADEMA kupata ama kujenga ofisi za kisasa makao makuu ya CHADEMA.

Tangu siku ile sijasikia tena Sabodo wala CHADEMA kuzungumzia hatua zilizofikiwa ili kufikia adhima hiyo.

Naomba msemaji wa Chama,au Kurugenzi ya Habari chadema ama Sabodo mwenyewe kama ni member wa jamii Forum kulitolea ufafanuzi na maelezo ya kutosha.


Nawasilisha.
 
Umenena vyema kiongozi. Makao makuu ya kisasa ni muhimu sana. Tena ukifikiria pale walipo sasa ni makao ya muda mfupi (wamejiegesha tu).

Pesa za ruzuku zimeongezeka na pia wanaweza kuanzisha mfuko maalumu wa ujenzi wa makao makuu kwa wabunge kukubali kukatwa kiasi cha pesa kutoka kwny mishahara na marupurupu yao ili kufanikisha zoezi ilo.

Tena ujenzi usiishie kwa makao makuu tu,bali uende hadi kwny ofisi za kata na vijiji. Huko nako mfuko huo wa wabunge ukiongezewa nguvu na makato ya madiwani utumike katika ujenzi wa ofisi izo. Hapo ndipo patakua ni dalili za kujiandaa kuongoza dola na serikali.
 
Huo ni mtazamo wako mkuu! lakini chuo cha maadili ya viongozi pia ni kitu muhimu! maana ni kitega uchumi pia!
 
Una pointi hapo ndugu makao makuu ni bora yawe ya kisasa hata kupata misaada isewe shida watu nafasi ya kuongea peoples power wapitishe bakuli wananchi tutajitolea kwa moyo wote
 
nimekuelewa mwanakijiji,lakini nafikiri hapo itakapokuwepo ofisi tunaweza kuweka na chuo cha maadili pia,does this make sense?
 
Baada ya kusikia habari kuwa CHADEMA wana mpango wa kujenga Chuo cha Maadili ya viongozi kwa heshima ya Bw. Sabodo aliyeahidi kuwachangia shilingi 150 nimejikuta nikitamani kunyofoa nywele zangu kichwani. Kati ya vitu vya kwanza ambavyo ninaamini Chadema wanahitaji kwa haraka zaidi ni makao makuu ya kisasa ya chama kinachojiandaa kutawala.

Ninaposema "makao makuu ya kisasa" nina maana ya jengo na mazingira yanayoendana na hadhi ambayo Chadema imejijengea sasa hivi lakini vile vile mahali ambapo kuna miundombinu ya kisasa vile vile. Lakini zaidi pia kujenga makao makuu ambayo hayatokuwa ofisi tu bali pia sehemu ya kitega uchumi.


Wapo wanaofikiri kuwa makao makuu sii kitu cha muhimu au si jambo la haraka kabisa. Wanafikiri wataendelea kujiandaa kushinda kwa kutumia vibanda vya nyasi na kutoa matangazo ya mipango yao kutoka uani! Chadema kama kinataka kianze kujipanga kiukweli sasa basi la kwanza ni kuandaa a modern command center. Nitawaachia wengine wafikirie makao makuu ya kisasa yaweje.

Lakini ukiniuliza mimi.. kati ya vitu vya kwanza kabisa vya kujiandaa na vitatupa mwanga kuwa sasa kweli CHadema inataka kushinda utawala wa nchi ni jinsi gani inajiandaa kwa makao yake makuu na kutoka hapo ofisi zake za ngazi za chini. Wakijenga hayo makao makuu basi wanaweza kuwa na sehemu ya mafunzo ambapo mafunzo ya maadili na mengine yataweza kutolewa.

Mara moja nilifika makao makuu ya chadema. Kindondoni.

Ni nyumba ya mtu.

Na wanastahili pongezi kwa kuendesha harakati zilizowapa mafanikio makubwa kwa kuanzisha mashambulizi kutoka kwenye nyumba ya mtu.

Wakipata jengo lao, nadhani mafanikio yao yatakuwa mara elfu.

Wazo zuri MM.
 
nimekuelewa mwanakijiji,lakini nafikiri hapo itakapokuwepo ofisi tunaweza kuweka na chuo cha maadili pia,does this make sense?

una hoja mkuu.

lakini vema chuo kikajengwa nje ya mji kidogo. si unajua vurugu za mjini? utazalisha wanasiasa vilaza.

na makao makuu ya chama lazima yawe 'mjini kati'
 
QUOTE=Geza Ulole;Huo ni mtazamo wako mkuu! lakini chuo cha maadili ya viongozi pia ni kitu muhimu! maana ni kitega uchumi pia!

Ndio. Huu ni mtazamo wangu kama ulivyo wa kwako mkuu.
 
yep itakuwa ni moja ya hatua kubwa na njia mojawapo ya kuelekea kuchukua nchi na wanapokuwa wanafundisha wawe wanakwenda na vijijini zaidi na kujikita uko na kuelimisha jamii na kuwaeleza pia kwamba nyerere kwa sasa ni hayati uwezi kuamini wengi hawajui kama alisha rip
 
Huo ni mtazamo wako mkuu! lakini chuo cha maadili ya viongozi pia ni kitu muhimu! maana ni kitega uchumi pia!

unaamini kabisa kuwa unaweza kuwafundisha watu maadili, wakahitimu halafu wakawa na maadili mazuri? HIvi unakumbuka jina la zamani la IDM Mzumbe lilikuwa linatangulizwa vipi?
 
Mkiwa na chuo cha Maadili ya Viongozi halafu wakahitimu na baadaye wakaonekana wamekosa maadili ina maana chuo kimeshindwa au hawakuhitimu? Forget about chuo cha maadili ya viongozi. Mkitaka wapelekeni vyuo vikuu au vyuo vilivyopo. Its cheaper.
 
Mkiwa na chuo cha Maadili ya Viongozi halafu wakahitimu na baadaye wakaonekana wamekosa maadili ina maana chuo kimeshindwa au hawakuhitimu? Forget about chuo cha maadili ya viongozi. Mkitaka wapelekeni vyuo vikuu au vyuo vilivyopo. Its cheaper.

hata mie sipati picha wanavyosema wanajenga chuo cha maadili. kama ni kuwafunza uongozi tayari kuna vyuo vingi. maadili binadamu tunazaliwa nayo (kujua mema na mabaya) mtu anafanya mabaya kwa tamaa yake binafsi iwe ya fedha, umaarufu nk. hivyo kufunza maadili ni kuwabana na kuwaadhibu watu waovu.

JENGENI OFISI NA KITEGAUCHUMI
 
Maadili gani iko chuo kinafundisha. Kama mtu afundwi kwao chuo kitafunza nini? Ila kama watafundisha sheria na mambo ya kawaida katika siasa kwa waliokuwa na maadili yao tayari toka makwao sawa. Lakini kufunza jitu zima maadili tena chuoni ni kupoteza muda. Aisee kama nachemsha haya maoni ujue naongea nikiwa na heineken kusherehekea ushindi wa Kilimanjaro Stars 5-4.
 
nimekuelewa mwanakijiji,lakini nafikiri hapo itakapokuwepo ofisi tunaweza kuweka na chuo cha maadili pia,does this make sense?

nami nafikiri kwa aina ya viongozi tulionao nahisi hii ndo itakuwa plan yao unaua ndege wengi kwa jiwe moja i.e ofisi chuo+vitega uchumi vingine bravo cdm!
 
na yawe maeneo ya kueleweka, sio kujificha mtaa wa Ufipa ambao mvua ikinyesha ni kichefuchefu tupu

ninaapa kwa jina la Jamhuri ya Tanzania, nilienda kuchukua kadi CHADEMA nikarudia mlangoni baada ya kuona yale mazingira tapishi
 
Umenena vyema kiongozi. Makao makuu ya kisasa ni muhimu sana. Tena ukifikiria pale walipo sasa ni makao ya muda mfupi (wamejiegesha tu). Pesa za ruzuku zimeongezeka na pia wanaweza kuanzisha mfuko maalumu wa ujenzi wa makao makuu kwa wabunge kukubali kukatwa kiasi cha pesa kutoka kwny mishahara na marupurupu yao ili kufanikisha zoezi ilo. Tena ujenzi husiishie kwa makao makuu tu,bali uende hadi kwny ofisi za kata na vijiji. Huko nako mfuko huo wa wabunge ukiongezewa nguvu na makato ya madiwani utumike katika ujenzi wa ofisi izo. Hapo ndipo patakua ni dalili za kujiandaa kuongoza dola na serikali.

kwani hiki chama mwakani kitakuwepo?, si nasikia alfi na kabwe wako mahututi hospitali?, si nasikia wanamsaka mchawi na wabunge wake watatu wamehojiwa na chama?. Ninamashaka chama kinaenda kusambaratika.
 
Ninaposema "makao makuu ya kisasa" nina maana ya jengo na mazingira yanayoendana na hadhi ambayo Chadema imejijengea sasa hivi lakini vile vile mahali ambapo kuna miundombinu ya kisasa vile vile. Lakini zaidi pia kujenga makao makuu ambayo hayatokuwa ofisi tu bali pia sehemu ya kitega uchumi.
.
what do u mean by kitega uchumi? usije ukawa unamaanisha non-performing office blocks
waulize pension funds watakuambia, it takes 25yrs to recover the money. angalau dr dau amekuwa mjanja yeye ame invest more into the govt bonds.
cdm needs a modest place to call home na sio jengo kuubwa. kama jengo la sasa hivi ni la kwao basi walikarabati na kama wamepanga wajaribu kulinunua. vikao vikubwa vya chama always vitakuwa vinafanyika kwenye conference hall.
ukienda znz unatakuta ccm ina majengo makubwa kila baada ya 5mins drive. haya majengo ni magofu tu
pia chadema wanahitaji kujenga small offices za makao makuu ya mikoa, wilayani party activist wanatosha kusambaza kadi. hawaitaji majengo ya vioo kusambaza kadi
 
Tatizo pesa za ruzuku zitatumiwa ovyo unajua tena Slaa amekosa ila atalipwa na hizi pesa kama sharti alilowapa chadema kuwa atalipwa kama mbunge kwa miaka yote mitano.Sasa ofisi itatoka wapi?
 
Back
Top Bottom