JENGO la tatu la abiria (Terminal III) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), linatarajiwa kutengeneza ajira lukuki

esther mashiker

JF-Expert Member
May 29, 2018
616
552
JENGO la tatu la abiria (Terminal III) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam linatarajiwa kutengeneza ajira lukuki, zikiwamo 245 za moja kwa moja litakapoanza kutumika Mei mwaka huu.

Aidha, maandalizi yanaendelea kufanyika kwa ajili ya matumizi ya jengo hilo la tatu ambalo litakuwa maalumu kwa abiria wa kimataifa huku jengo la pili likiwa la abiria wa ndani ya nchi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Julius Ndyamukama aliliambia gazeti hili jana kwamba maombi ya kibali cha kuajiri wafanyakazi yameshapelekwa kwenye mamlaka zinazohusika.

“Hizo ni ajira za moja kwa moja, achilia zile za maduka, hoteli na kadhalika,” alisema Ndyamukama na kufafanua kuwa wameomba kuajiri wafanyakazi watakaohudumu katika maeneo mbali mbali. Ndyamukama alisema kibali kilichotoka ni cha ajira 135.

Taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo hilo la tatu iliyotolewa kwa Bodi ya Wakala wa Barabara (Tanroads) iliyofanya ziara JNIA hivi karibuni ilisema TAA inakamilisha mchakato wa kupata watoaji wa huduma mbalimbali katika jengo na mhandisi mshauri wa uendeshaji na uhamisho wa uwanja wa ndege (ORAT).

Vile vile taarifa ilisema TAA wameanza kujifunza kutoka kwa mkandarasi juu ya matumizi na jinsi ya kufanyia matengenezo vifaa na mifumo mbalimbali ya jengo hilo jipya. Ndyamukama alithibitishia gazeti hili kwamba mkandarasi wa mradi, BAM International anaendelea na kazi hiyo ya kutoa mafunzo. “Kila mfumo ukifungwa wafanyakazi wanapewa mafunzo juu ya matumizi,” alisema Ndyamukama aliyekuwa Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam kabla ya uteuzi wa hivi karibuni kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAA.
 
Ni vizuri sana kwa uchumi wetu. Ila hiyo picha ni ya uwanja huo kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
Humo ni ndani ya jengo
1058828
 
 
View attachment 1058815

JENGO la tatu la abiria (Terminal III) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam linatarajiwa kutengeneza ajira lukuki, zikiwamo 245 za moja kwa moja litakapoanza kutumika Mei mwaka huu.

Aidha, maandalizi yanaendelea kufanyika kwa ajili ya matumizi ya jengo hilo la tatu ambalo litakuwa maalumu kwa abiria wa kimataifa huku jengo la pili likiwa la abiria wa ndani ya nchi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Julius Ndyamukama aliliambia gazeti hili jana kwamba maombi ya kibali cha kuajiri wafanyakazi yameshapelekwa kwenye mamlaka zinazohusika.

“Hizo ni ajira za moja kwa moja, achilia zile za maduka, hoteli na kadhalika,” alisema Ndyamukama na kufafanua kuwa wameomba kuajiri wafanyakazi watakaohudumu katika maeneo mbali mbali. Ndyamukama alisema kibali kilichotoka ni cha ajira 135.

Taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo hilo la tatu iliyotolewa kwa Bodi ya Wakala wa Barabara (Tanroads) iliyofanya ziara JNIA hivi karibuni ilisema TAA inakamilisha mchakato wa kupata watoaji wa huduma mbalimbali katika jengo na mhandisi mshauri wa uendeshaji na uhamisho wa uwanja wa ndege (ORAT).

Vile vile taarifa ilisema TAA wameanza kujifunza kutoka kwa mkandarasi juu ya matumizi na jinsi ya kufanyia matengenezo vifaa na mifumo mbalimbali ya jengo hilo jipya. Ndyamukama alithibitishia gazeti hili kwamba mkandarasi wa mradi, BAM International anaendelea na kazi hiyo ya kutoa mafunzo. “Kila mfumo ukifungwa wafanyakazi wanapewa mafunzo juu ya matumizi,” alisema Ndyamukama aliyekuwa Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam kabla ya uteuzi wa hivi karibuni kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAA.
Ajira za mafingu mafungu kama.ya dagaa kwa miaka mnne sasa ya Malaika Mkuu Wa wasiojulikana.
 
Kwani lazima uufikie wa Jomo Kenyata,mbona wewe mke wako hamfikia hata robo kwa uzuri mke wangu lakini bado ni mkeo,Kenya kivyake na TZ kivyake,mambo ya kulinganisha kamlinganishe mkeo
Sasa povu la nini Wakati tuliambiwa Kenya kwa sasa hawafui Dafu kwetu,Mpaka wakalipia kwenda Kuishangaa Ndege yetu..
 
Wanawaua na kuwata umaskini
 
Back
Top Bottom