Jengo la Mafuta House labadilishwa jina kuwa B W Mkapa

Mwanagenzi

JF-Expert Member
Sep 11, 2006
700
213
Jengo refu kuliko yote jijini Dar es Salaam limepewa jina la rais mstaafu Benjamin William Mkapa kinyume na matarajio ya wengi kuwa jengo hilo lingeendelea kuitwa Mafuta House.

Kwa wadadisi wa mambo ya kisiasa huenda jina hilo jipya likazusha gumzo kutokana na ukweli kwamba tangu rais Mkapa atoke madarakani na hususan kwa siku za karibuni amekuwa akituhumiwa na kuhusishwa na ubadhirifu na ukosefu wa maadili kama kiongozi mkuu wa nchi wakati wa utawala wake.
 
At least hayumo kwenye ile official list ya watuhumiwa 11 wa Tundu Lisu. Kwi kwi kwi.
 
Hicho kichwa cha habari!!!
mimi nilifikiri linakuwa la kwake, nikajua aliyenacho tayari kaongezewa tena
 
Usikute hawa wanataka kumtosa kwenye Stadium aliyoijenga.
Uwanja uitwe Benjamin Mkapa Stadium.

Watasema tushaita jengo kwa jina lako inatosha!!!!!!!!!!
 
..kujipendekeza tuu kwa waswahili huko hakuna lolote hapo,hapo misifa mbele faida nyuma,i'm glad i didnt put my money kwa hao wazushi.
 
Simnajua wabongo tumeshazoea pigwa changa la macho, usikute wanaanza taratibu kwa kulipa jina la mkuu, kisha baadae mkuu ananunua hisa, na mwisho kabile hisa zote zinakuwa zake. Na hapo ndipo hati ya jengo itakapo onyesha liko chini ya mkuu. Teh teh teh ....Just a guess!!
 
Hivi hawa CCM wanafanya hivi kwa kumkubuka kwa lipi hasa alilo lifanya ndani ya CCM ? Lazima patakuwa na sababu tu , hebu wajuvi njoeni na sababu za kupewa heshima hii ama ndiyo tena inakuwa namna kurithishana majina kila kona ? Maana hata miaka 2 bado kila kona kuna shule za Salm JK wakati Maria Nyerere sijui kwamba hata anakumbukwa kwa namna hii .
 
Usikute hawa wanataka kumtosa kwenye Stadium aliyoijenga.
Uwanja uitwe Benjamin Mkapa Stadium.

Watasema tushaita jengo kwa jina lako inatosha!!!!!!!!!!

..uwanja ungeitwa kwa jina lake ndio ingekuwa poa zaidi!bidii zake zile!
 
Mimi nilifikiri kapewa jengo kumbe jengo limetajwa jina lake! Yaani JF mmekuwa kama waandishi wa habari, kichwa cha habari kikubwa, ukisoma ndani, oops. Sasa madamu huyu bwana alishakuwa kiongozi wetu, pamoja na matatizo yake aliyokuwa nayo, mambo kama haya hayakwepeki, majengo, barabara,mashule, n.k. yatajwa tu jina lake, na binafsi sidhani kwamba hii inapaswa kuwa ishu!
 
Hivi hawa CCM wanafanya hivi kwa kumkubuka kwa lipi hasa alilo lifanya ndani ya CCM ? Lazima patakuwa na sababu tu , hebu wajuvi njoeni na sababu za kupewa heshima hii ama ndiyo tena inakuwa namna kurithishana majina kila kona ? Maana hata miaka 2 bado kila kona kuna shule za Salm JK wakati Maria Nyerere sijui kwamba hata anakumbukwa kwa namna hii .


Nakwambia katika mtu ambaye CCM wanapaswa kumheshimu ni huyu. Bila huyu CCM ingekwenda na maji katika kipindi chake. Huyu ndiye aliyeufikisha upinzani hapa ulipo kwa kuhakikisha anawa-frustrate majemedali wote wa upinzani akianzia na Lamwai. Kwa hiyo, yes, huyu bwana did a lot of harm to the country, but he was so good to CCM!


Halafu JK yeye ndiye kabisa inabidi huyu bwana amlambe hata miguu. Kumbuka kama angeamua JK asingewahi kuwa Rais wa nchi. Tena angeweza kumtoa uwaziri mapema kabisa na kumpeleka kuwa balozi wetu somewhere na huo ndio ungekuwa mwisho wake. Yaani nikisikia JK anamsifia Mkapa namuelewa na kwa kweli I sympathise with him, it is so natural!
 
Kitila nimekupata vizuri sana hapo mjomba,Mkapa angeamua JK asiwe raisi was sooo easy...ni ubalozini kwa miaka yote au angemnyima kazi tuu na kuwa kapuku nani angemjua!
 
Ni aibu kubwa kwa Taifa kuliita jumba hili jina la huyo fisadi ambate alitumia madaraka yake kujitajirisha na kusaini mikataba mibovu ambayo mpaka leo ni siri kwa Watanzania. Hapa ndio Watanzania inabidi tuonyeshe umoja wetu ili kupinga uamuzi huu kwa nguvu zote. Fisadi katudharau Watanzania hata tuhuma nzito dhidi yake hataki kuzijibu.
 
mimi nilipoona heading nikajua aliyeileta anaongelea nyumba ya mkapa anayojengewa na serikali MASAKI kama zawadi ..ikiwa ni sehemu ya stahili za rais mstaafu..kumbe mnaongelea MAFUTA HOUSE ..infact mkapa kajitahidi kuleta maendeleo pamoja na makosa anayotuhumiwa ..SIO VIBAYA HILO JENGO Kuitwa BENJAMIN WILLIUM MKAPA....

HATA na UWANJA WA TAIFA MPYA uitwe BENJAMIN WILLIUM MKAPA NATIONAL MORDERN STADIUM....or like that..walioingia wajenge vyao navyo tuvipe majina yao....ie JAKAYA MRISHO KIKWETE NATIONAL THEATRE OR JAKAYA KIKWETE NATIONAL INDOOR STADIUM ets
 
mimi nilipoona heading nikajua aliyeileta anaongelea nyumba ya mkapa anayojengewa na serikali MASAKI kama zawadi ..ikiwa ni sehemu ya stahili za rais mstaafu..kumbe mnaongelea MAFUTA HOUSE ..infact mkapa kajitahidi kuleta maendeleo pamoja na makosa anayotuhumiwa ..SIO VIBAYA HILO JENGO Kuitwa BENJAMIN WILLIUM MKAPA....

HATA na UWANJA WA TAIFA MPYA uitwe BENJAMIN WILLIUM MKAPA NATIONAL MORDERN STADIUM....or like that..walioingia wajenge vyao navyo tuvipe majina yao....ie JAKAYA MRISHO KIKWETE NATIONAL THEATRE OR JAKAYA KIKWETE NATIONAL INDOOR STADIUM ets

..Nisingelipenda kuamini ulichoandika hapo juu hata kama ni kweli. Sasa huyu mkapa pamoja na tuhuma zote hizo, bado anajengewa nyumba??? Dr.Bundala akiandika waafrika ndivyo tulivyo tunavimba utadhani tumekunywa hamira!!!
 
....Tanzania inajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno...halafu nina hasira na huyu Mkapa yaani ni mjeuri wa wazi wazi......goddamn it.
 
Mheshimiwa kikwete embu jaribu kuwa na busara katika uongozi wako!!! Ina maana hiyo issue ya nyumba anayojengewa mkapa huko masaki kama anavoyodai philemon huna taarifa nayo??? Usifanye watanzania wakaanza kutumia jina lako vibaya. Ukiendelea hivyo, usishangae kusikia watu tumeanza kusema: Seleman siku hizi ni kikwete kweli. Embu tazama alivyotelekeza familia yake!!! Mwalimu jamuhuri siku hizi ni kikwete kweli embu tazama wanafunzi wake wote wamepata divisheni zero!!! Dr.Ali siku hizi ni kikwete kweli!!!, embu tazama amempasua mgonjwa mguu badala ya kichwa!!! Nanihii siku hizi ni kikwete kweli, embu tazama alivyolewa chakari mpaka anatembea uchi!!!

Chonde chonde, kikwete!!! Rekebisha mambo usije kusema sikujua kama itakuwa hivi.

 
Back
Top Bottom