Jenerali Ulimwengu, kumbe hata wewe ni mnafiki!

hakuna mashiko kwenye hoja zenu wote. ninyi kma hamumtaki msitulishe sisi dhana ya kumkataa kwani sisi tunamkubali sana. inawalazimu mfanye kazi ya ziada kuwashawishi wapiga kura wamkatae na sisi tunawashawishi wamkubali. dakika tisini zinaisha oktoba 25 saa nne mpaka saa saba usiku....sikiliza kishindo chake halafu uje jamvini tufanye tathmini kwa pamoja
nakubaliana na wewe kiongozi ukiangalia historia ya chimbuko la vyama vingi vya siasa ulaya utaona limetokana na kutoelewana ndani ya bunge ndipo vyama vikaundwa tafsili fupi hapa ni uibukaji wa vyama vyetu hapa haikua hvyo kwa hyo maslahi ndio kigezo kikubwa cha kuundwa vyama vyetu baada ya kufosiwa na wakoloni wetu kwahyo pindi lowasa atakapo shindwa uchaguzi hatakua tena naupenzi wa kudumisha chama cha chadema mwisho wake kita sinzia km nccr
 
Wewe Dilema ni mjinga kabisa. Kwanini unataka kila mtu aishi unavyotaka wewe.??? Kumbuka kuwa wewe kura yako ni moja tuu. Huna haki ya kuamulia wengine wapende nini au wachukie nini. Na kumbuka kuwa kila mtu anatumia haki yake kikatiba ya kushiriki katika siasa kupitia chama chochote kile au kumuunga mkono mgombea yoyote yule.
Usiwe na mawazo mgando ya kuamini kuwa mawazo na hisia zako ndizo bora kuliko za wengine. Kila mtu yuko huru kufuata upande anaoupenda.
 
Waambie hao! Ni kweli kwamba uandishi wa raia mwema na raia tanzania umebadilika kutoka kukemea maovu hadi kutetea mafisadi. Nadhani watakuwa wamenunuliwa na mafisadi (ccm).

Huu ndio wakati wa kutegea nafasi za Ukurugezi wa Habari mara baada ya Uchaguzi. Kumbuka Salva rweyemamu weye? Amekula mapochopocho na mchuzi wa Ikulu kwa miaka kumi sasa, akitoka hapo kiinua mgongongo kikubwa na pensheni kila mwezi.

Vv
 
Hivi kama sijaelewa. Kwani lazima wote tushabikie UKAWA jamani? Nijuavyo mimi hii ni nchi huru na kila mmoja ana uhuru wa kushapikia kile anachokiona yeye ni sahihi kwake. Sidhani kama ni busara sana kumuita mtu mnafiki kwasababu tu ametofautiana na wewe. Ujue ukiona yeye anampigia debe Magufuli basi ana imani naye, kama mimi na wengine tunaompigia debe Dr. Slaa kwasababu ndio tunaona mpinzani wa kweli. Na kuna wengine wanamshabikia Lowassa, yaani ni haki yao kabisa na waendelee kufanya hivyo.
 
Ulimwengu anaandika makala zake kwa nadharia na falsasa sana. Makala zake ni abstract sana, kiasi kwamba kama ni msomaji mgeni hutazipenda. Hii haijalishi ameandika kwa Kiswahili au Kiingereza. I can vouch for this guy-I have known him for a long time to know he is a true activist/reformist. Ni mmoja ya waandishi wachache wasiopelekeshwa na dini, ukada wala ukanda.

Yeye kama mmoja wa wamiliki wa Raiamwema ni mwandishi mkongwe wa habari na anajua sio busara na ni kinyume cha maadili ya uandishi kuwapangia wenzake cha kuandika. Na inafahamika toka enzi za Rai kuwa kuna baadhi ya waandishi wao 'akili zinahama' wakati wa uchaguzi na wamewahi kuliweka bayana. Mfano Maggid wa nyakati za uchaguzi ni tofauti na wa nyakati zingine zote. Wakati wa uchaguzi, yeye ni pro CCM.

Kwa upande wa Mbwambo, huyu nae ni mwanamageuzi asiyetetereka. Amekuwa na msimamo usioyumba kwenye kutetea mageuzi. 'Tatizo' lake, uanamageuzi wake umejikita kwenye misingi-sio pragmatist. Kiukweli, kwa wafia mageuzi na washabiki wa siasa za chadema, kumpokea Lowassa ilikuwa ngumu sana kwasababu anaenda kinyume na wengi wanachokiamini. Baada ya kuandika makala zaidi ya 20 za kuponda ufisadi na Lowassa, naweza kumuelewa akikataa kumeza matapishi yake.

Namuunga mkono Lowassa kwa sababu he is a real threat to CCM.Japo naunga mkono ukawa, nina wasiwasi (kama Mbwambo) na mstakabali wa baadae wa chadema. Rejea historia ya NCCR mageuzi. Baada ya NCCR kuzimia kisiasa, upinzani wa kweli na mhemuko wa siasa za upinzani ulipoa sana-hiki ndo wanamageuzi waliojikita kwenye misingi wanakihofia. Ukiondoa ajenda ya ufisadi, chadema itazimia kisiasa. Hata hivyo tumaini lipo kwenye idadi ya wabunge wengi wanaoweza kupata. Sina tatizo na Mbowe, ni mwanasiasa makini na mahiri, amefanya kile Mandela na ANC walikifanya-kuungana na adui (National party) kuunda serikali ili kujenga nchi na kusonga mbele. Historia itamhukumu Mbowe, kama ambavyo baadhi ya weusi wanamlaumu Mandela.

Ulimwengu ahishimiwe, ni mwanamageuzi na mwanaharakati nguli. Ni kama Dr. Slaa. Hatuwezi kuthubutu kuusahau mchango wake (kama tunajiheshimu) ktk mageuzi eti kwasababu tu haungi mkono kuja kwa Lowassa, hata kama tunampenda sana Lowassa.

Kila mtu anapimwa kwa wakati.

Kama alikuwa mzuri kipindi kilichopita si lazima awe hivyo kila binadamu anabadilika.

Kama ana maslahi na alcohol inaeleweka.

Lakini ni kipindi kizuri kuwatambua watu wanavyokimbiza maslahi yao na ukinyonga wao halisi. Sitashangaa kama Jenerali ni mmojawapo. ndivyo watu hupotea na kuhukumiwa na historia.
 
Waambie hao! Ni kweli kwamba uandishi wa raia mwema na raia tanzania umebadilika kutoka kukemea maovu hadi kutetea mafisadi. Nadhani watakuwa wamenunuliwa na mafisadi (ccm).

Nakubaliana na prof James Watson kuwa sisi watu weusi tuna uwezo mdogo sana wa kufikiri, ni wewe Jenerali Ulimwengu uliyewahi kutofautiana na serikali ya CCM kisa kuandika maovu yao, wakakupora uraia wako wakisema kuwa wewe si mtanzania na ukaanza kuishi ndani ya nchi yako kwa kulipia kibali, mtu uliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya unaambiwa si raia na uishi kwa kibali, sasa hivi unaipigia kampeni CCM iendelee kutawala wewe na mwenzako Mbwambo, huu ni unafiki wa hali ya juu kupindukia, leo CCM imekuwa nzuri kwako kwa lipi hasa?

Hata kama padlocks ni best yako tambua kuwa CCM ni mfumo hata aje malaika awe rais kupitia CCM hakuna kitakachobadilika,tupo vitani kuhakikisha kuwa CCM inaanguka kwa gharama yoyote ile, unapokuwa vitani huwezi kuchagua silaha za kupigania, inapobidi unaweza kutumia silaha ya adui ili kushinda vita pindi ukifanikiwa kuiteka ndo maana tukamchukua Lowassa, Lowassa ni bomu la nyuklia ktk vita dhidi ya CCM na kwa hiyo lazima tushinde hii vita,wewe na wenzako mmetugeuka ktk battle field,hamfai kabisa.

Sisi hayo magazeti hatusoni huku vijijini tunajua lowasa ndio rais
 
Nakubaliana na prof James Watson kuwa sisi watu weusi tuna uwezo mdogo sana wa kufikiri, ni wewe Jenerali Ulimwengu uliyewahi kutofautiana na serikali ya CCM kisa kuandika maovu yao, wakakupora uraia wako wakisema kuwa wewe si mtanzania na ukaanza kuishi ndani ya nchi yako kwa kulipia kibali, mtu uliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya unaambiwa si raia na uishi kwa kibali, sasa hivi unaipigia kampeni CCM iendelee kutawala wewe na mwenzako Mbwambo, huu ni unafiki wa hali ya juu kupindukia, leo CCM imekuwa nzuri kwako kwa lipi hasa?

Hata kama padlocks ni best yako tambua kuwa CCM ni mfumo hata aje malaika awe rais kupitia CCM hakuna kitakachobadilika,tupo vitani kuhakikisha kuwa CCM inaanguka kwa gharama yoyote ile, unapokuwa vitani huwezi kuchagua silaha za kupigania, inapobidi unaweza kutumia silaha ya adui ili kushinda vita pindi ukifanikiwa kuiteka ndo maana tukamchukua Lowassa, Lowassa ni bomu la nyuklia ktk vita dhidi ya CCM na kwa hiyo lazima tushinde hii vita,wewe na wenzako mmetugeuka ktk battle field,hamfai kabisa.
umesikitika kwa sababu hukuwafahamu zaidi ,hao uliowataja hawana mapenzi na maendeleo ya upinzani(hasa inapokuja suala la kuchukua doala) kwa sababu haina maslahi kwao, wakijifanya wako na upinzani ni lip service only and not for real
 
Hivi kama sijaelewa. Kwani lazima wote tushabikie UKAWA jamani? Nijuavyo mimi hii ni nchi huru na kila mmoja ana uhuru wa kushapikia kile anachokiona yeye ni sahihi kwake. Sidhani kama ni busara sana kumuita mtu mnafiki kwasababu tu ametofautiana na wewe. Ujue ukiona yeye anampigia debe Magufuli basi ana imani naye, kama mimi na wengine tunaompigia debe Dr. Slaa kwasababu ndio tunaona mpinzani wa kweli. Na kuna wengine wanamshabikia Lowassa, yaani ni haki yao kabisa na waendelee kufanya hivyo.

Umesema kweli mkuu tusilazimishwe wote kuwa manyumbu, mbugani kuna wanyama wengi tu werevu kuliko nyumbu ila hawana makeke wala mikeke, hivyo hawawezi kuliwa na simba
 
ukawa vp,yan nyie mtu akiwa against nyie kwenye media kanunuliwa,hii nchi ya kidemokrasia kila m2 ana uhuru wa kusema anachotaka na kua upande anaoutaka...na kwenye demokrasia yyte lazma kuwe na kukinzana haiwezekan wote mkawa upande mkasema ni demokrasia never...nyie wnywe mlisema hakuna adui wa kudumu kwenye siasa iweje leo muanze kumponda dkt ulimwengu wakt nyie adui wenu alikua lowassa sasa hv mnambeba kwa mbeleko...achen siasa za kitoto yan inaonyesha hatuja mature kwenye siasa hata kdg

Wanataka wote tuburuzwe na maamuzi ya Mbowe.

Hao ukitofautiana nao tu utapewa majina yote yanayowaridhisha,.

Wanataka wote tumwimbie Lowassa mapambio ya kumsifu na kumtukuza kama mkombozi. ..

Wanataka wote tuseme ndio Mwenyekiti kwa Mbowe hakuna kupinga wala kuhoji maamuzi ya Mwenyekiti ..

Wanataka wote tumchukie Lipumba, tumtukane na kumkashifu kisa hakubaliani nao...

Wanataka wote kwa pamoja tumkashifu Dr. Slaa, tumtukane na kumzushia propaganda chafu kisa Kagoma kuburuzwa...

Ukweli hawana hoja wenyewe ni vioja na matusi kwa kila anaepingana nao hata kwa hoja zilizowazi.

Wanafikiri wote tunaweza kumkabidhi akili Mbowe na maamuzi Lowassa.
 
Kule katika ulimwengu usio wa mwili ni mfueni kali.

For we wrestle not against flesh and blood, but against principalities, against powers, against the rulers of the darkness of this world, against spiritual wickedness in high places.
 
Mandela alishirikiana na makaburu na wapinzani wake baada ya kuingia ikulu na siyo kabla. Kwa hiyo Mbowe amekosea kumkaribisha Lowasa na kumfanya mgombea wa chadema. Watu wenye akili za kutosha hawawezi kumpa Lowasa kura. Huyu mtu hana maadili na anatumia fedha kutafuta urais na hii ni Hatari. Nina hakika baada ya kampeni wengi wanaonfuata watabadilika na hawatampa kura. Ukawa turidhike na wabunge zaidi ya nusu ili kuithibiti serikali na Sera zetu na ilani yetu zitekelezwe na serikali itakayoundwa hata kama Tingatinga akiwa rais.

hoja ya kuwa fulani anatumia hela kusaka urais me naona haina mashiko kwani hakuna kipimo kuwa ukitumia isizidi kiasi gani magufuli ma ccm wao wanatumia nini
 
mfianchi yaani unaonyesha waziwazi kufia nchi...ama kweli ...hakuna mrusha mitusi na hakuna msaka madaraka kwani demokrasia inatoa wigo mpana wa raia kushiriki siasa. usifikiri ukimnyima kwako basi asiende kwingine hapana. EL ametafakari na sisi tumetafakari sote kwa pamoja tumeona anatosha kuiondoa CCM madarakani. sasa ninyi wachche mliobaki kufia nchi mnao wajibu wa kufikiri upya. Tanzania bila CCM inawezekana
Sawa ndugu ndio demokrasia,tuonane kwa debe hiyo Oct 25th
 
Msichojua wengi ni kuwa raia mwema ni kampuni ambayo mmoja ya wenye hisa wakubwa ni Zito Zuberi Kabwe. Nadhani anamzidi hata generali. Sasa kazi ya Zito zuberi Kabwe imekuwa wazi sasa kuwa ni kuhakikisha CCM inaendelea kuwa chama tawala na yeye anaendelea kupata mkate wake kwa mwamvuli wa mpinzani.
 
Nakubaliana na prof James Watson kuwa sisi watu weusi tuna uwezo mdogo sana wa kufikiri, ni wewe Jenerali Ulimwengu uliyewahi kutofautiana na serikali ya CCM kisa kuandika maovu yao, wakakupora uraia wako wakisema kuwa wewe si mtanzania na ukaanza kuishi ndani ya nchi yako kwa kulipia kibali, mtu uliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya unaambiwa si raia na uishi kwa kibali, sasa hivi unaipigia kampeni CCM iendelee kutawala wewe na mwenzako Mbwambo, huu ni unafiki wa hali ya juu kupindukia, leo CCM imekuwa nzuri kwako kwa lipi hasa?

Hata kama padlocks ni best yako tambua kuwa CCM ni mfumo hata aje malaika awe rais kupitia CCM hakuna kitakachobadilika,tupo vitani kuhakikisha kuwa CCM inaanguka kwa gharama yoyote ile, unapokuwa vitani huwezi kuchagua silaha za kupigania, inapobidi unaweza kutumia silaha ya adui ili kushinda vita pindi ukifanikiwa kuiteka ndo maana tukamchukua Lowassa, Lowassa ni bomu la nyuklia ktk vita dhidi ya CCM na kwa hiyo lazima tushinde hii vita,wewe na wenzako mmetugeuka ktk battle field,hamfai kabisa.
anaogopa kufutiwa tena, humuoni baba yetu wa UDP toka atishiwe kunyang'anywa nyumba kapotea...........
 
Tunazungumzia ukweli wa kula matapishi yao na kuanza kumtakasa mtu walietumia tumia nguvu nyingi kumchafua ina maana hakukuwa na mtu wa kutupeperushia bendera ukawa
Nilisha wambia zaidi ya mara moja kwamba kukurupuka kwa UKAWA bila ya kutafakali mambo kutawa-cost an arm and leg, sioni kama somo hilo limewaingia,mwanzoni mlikuwa mmejipanga vizuri mkaja kujikoroga wenyewe at the eleventh hour! Kila mtu anayetofautiana nanyi mnamchukulia ni adui!/msaliti hamjui kwamba majanga ya Urusi chini ya Uongozi wa YELTSIN yanaweza kulikumba Taifa letu tusipokuwa makini, sina shaka Mh.Ulimwengu na raia wengine wanao litakia mema Taifa letu wamekwisha lishtukia hilo.
 
Ni kweli.
Jenerali lazima amsapoti ndugu yake Magufuli hata kama zamani alikuwa mpinzani.
That is natural.
Wanatoka eneo moja kona ya kaskazini magharibi ya nchi. Wenyeji wengi pale in wahamiaji kutoka Rwanda na Burundi.
Lakini wote nia raia halali wa nchi hii
Katika dunia ya leo huwezi ku-victimize mtu kutokana na background yake.
Ndiyo maana hata Obama ameweza kutawala Marekani.
Tatizo ni kwamba hapa kwetu ni kwamba hutawaamini sana ndugu zetu hawa ambao wakati mwingine tunawaita Banyamulenge.
 
Raia mwema na Raia tanzania ni magazeti ya kuachana nayo. Tuyapige vita kwa sababu yanapinga mabadiliko!
 
Back
Top Bottom