Jenerali Ulimwengu aponda utovu wa umakini katika diplomasia ya JK

chademaistheway

Senior Member
Aug 18, 2010
100
86
NIMESEMA kwamba tunafanya makosa kama taifa na wala hakuna jambo la kushangaza katika kutenda makosa. Kila mtu hufanya makosa maishani mwake na kila taifa pia. Ni jambo la kawaida.

Jambo ambalo si la kawaida ni pale mtu mwenye akili timamu anapofanya kosa na asijue kwamba kafanya kosa, ama akafanya kosa na akajua kwamba kafanya kosa na kisha akajisahau na kuja kulifanya kosa lile lile.

Jamii zenye kujali uendelevu hujifunza kutokana na makosa ziliyoyatenda huko nyuma ili zisiyarudie. Jamii zisizojali uendelevu huishi kwa kuangalia kilicho mezani hii leo na zisijali kilichotendeka jana wala juzi. Hizi jamii za aina hii zinaweza zikawa zinarudia makosa yale yale siku hadi siku na mwaka hadi mwaka mpaka ikawa ndiyo hulka ya jamii hizo.

Ili kukumbuka ni mahali gani zilikosea katika historia yake, jamii za mapokeo (kabla ya maandiko) ziliweka simulizi, hadithi na ngano ili kuwajuvya vijana wake mambo yaliyotendeka zama za kale kama mafundisho kwa watoto na vijana. Siku hizi mambo kama hayo huwekwa ndani ya vitabu.

Laiti kama tungekuwa tukiandika mambo tunayoyafanya, mazuri na mabaya, tungekuwa tumejijengea hazina ya ujuzi katika mambo mengi. Kwa bahati mbaya hatuna hazina hiyo kwa sababu tunaishi siku hadi siku na hatuna kumbukumbu ya mambo tuyatendayo. Matokeo yake ni kuwa na watu kama ‘Balozi Mstaafu' ambaye kazi yake kuu ni kusema kwamba kila kitu kimekwenda sawa na hakuna cha kubadilisha, ambayo ni falsafa ya Profesa Pangloss wa Voltaire.

Katika mfululizo huu nimeandika kwamba tumewahi kufanya makosa ambayo yangetulazimu tujifunze kutokana nayo. Nimezungumzia jinsi tulivyoshindwa kabisa kuisoma vyema hali ya Angola mwaka 1964-65, na jinsi tulivyojikuta tukiwa kama vile tuko upande mmoja na Makaburu wa Afrika Kusini katika kukataa kuitambua serikali ya MPLA na Agustino Neto.

Nimeeleza ni jinsi gani Mwalimu Julius Nyerere alijaribu kuisahihisha hali hiyo hadi akawa mtetezi mkuu wa serikali hiyo. Lakini leo hii sidhani kwamba wanadiplomasia wetu, pamoja na ‘Balozi Mstaafu' wamesoma ni nini kilichotendeka mpaka tukawa na msimamo wa hovyo na ni jinsi gani Jonas Savimbi aliweza kuiingilia Serikali ya Nyerere kiasi hicho. Hatutaki kuangalia tulikotoka, na kwa jinsi hiyo hatupati mafunzo muhimu kutokana na historia yetu. Tunakuwa ni watu wa kuanza upya siku zote.

Hata hivyo ni kweli kwamba serikali ya Tanzania haikuwakilishwa na mjumbe hata mmoja katika sherehe ya Uhuru wa Angola mjini Luanda na hili halitafutika milele. Inaelekea ‘Balozi Mstaafu' halijui hili, na wala wenzake hawalijui, na wala hawataki kulijua.

Tulifanya makosa katika kuisoma Afrika Kusini na harakati zake za ukombozi. Tulishindwa kuiona African National Congress (ANC) kwamba ndiyo ngome kuu ya harakati hizo na tukajiruhusu kupumbazwa na hisia hafifu za watu waliokuwa hawana uwezo wa kuangalia mbali na pua zao. Leo hii Afrika Kusini ni nchi pekee, pamoja na Angola, ambako, miongoni mwa nchi za kusini zilizokombolewa miaka ya hivi karibuni, hakuna alama ya mtaa au jumba au kitongoji, linakoonekana jina la Tanzania au Nyerere. Hatujiulizi.

Natumai kwamba si ‘Balozi Mstaafu' aliyesaidia kuandika hotuba ya Mheshimiwa Rais wetu katika mazishi ya Nelson Mandela mwezi uliopita. Kwamba kiongozi wetu alikosea hata mwaka wa ujio wa Mandela nchini Tanganyika (siyo Tanzania) lilikuwa ni kosa muhimu. Lakini pia aliyeandika hotuba hiyo ya Rais alisahau kutaja sababu za Mandela kuja Tanganyika na msimamo wa Tanganyika wakati huo ndani ya Jumuiya ya Madola (Ama Afrika Kusini iondoke ama sisi, Tanganyika tutaondoka).

Inanikumbusha jinsi mwakilishi mmoja wa nchi yetu (hakuwa mtu wa serikali lakini aliiwakilisha nchi hii) alivyosemwa kwenye mazishi ya wapiganaji wa ANC miaka kadhaa ilyopita aliposema kwamba sasa ndiyo nafasi ya kuunganisha ubongo wa weupe na misuli ya weusi kuijenga nchi mpya! Hili nalo hatulikumbuki.

Tunazungumzia diplomasia ya kiuchumi, lakini binafsi sielewi hii ina maana gani wakati naona mabalozi wakiteuliwa kama shukrani kwa fadhila hii au ile. Najiuliza ni diplomasia gani watafanya watu wanaopewa zawadi kwa jambo hili au lile. Najiuliza pia iwapo kuna nchi inayoitwa ya Kiafrika ambayo tunayo maslahi nayo kama Algeria, ni kwa nini hatuna ubalozi nchini Algeria, nakosa jibu.

Hivi sasa, tunao makumi ya wanafunzi wa Tanzania wanasomeshwa bure, bure! nchini Algeria katika fani muhimu kama uganga, dawa, uhandisi wa gesi na mafuta. Lakini ubalozi wetu unaoshughulikia Algeria uko Paris! Hatuoni haya kuwawekea wananchi wa Algeria ubalozi wetu nchini Ufaransa. Mkoloni aliyewatawala na kuwatesa hadi kuua watu milioni moja unusu!

Source: Raia Mwema
 
Maswali:

Hivi kweli Ubalozi wa Tanzania Algeria uko Paris?

Huyu ''Balozi Mstaafu'' anayetajwa na Jenerali ni nani?

Hivi kweli hakuna hata mtaa mmoja South Africa na Angola wenye jina la Nyerere?

Hivi kuna sababu zingine zilizopelekea Mandela kuja Tanzania zaidi ya zile alizotaja JK kwenye mazishi ya Madiba pale Qunu?
 
Hivi nyinyi mnadhani kila nchi ina tabia ya kujipendekeza kugawa majina ya barabara hovyohovyo mpaka eti hadi Mwai Kibaki naye kapewa barabara? only in Tanzania kwa heshims ipi aliyonayo Kibaki?
 
Afrika Kusini hakuna mtaa wowote wenye jina la Tanzania ama tu Nyerere lakini kuna wilaya inayoitwa Dr Kenneth Kaunda. Kaunda kapewa wilaya nzima kwa jina lake. Ahsante sana Jenerali
 
Kama ningekuwa ke ningembamba mjomba nadhan angeupa mtaa jina langu ha haa!
 
Tumjue kwanza balozi mstaafu ni nani ili tuweze kumjadili

Balozi mstaafu hataki kujulikana maana katika article yake kwenye RAIA Mwema akijibu hoja za Ulimwengu alijitambulisha kama "Balozi Mstaafu".

Ni kweli ingelikuwa vema kumjua maana tunaweza kuwa tunajadiri mawazo ya mtu ambaye wala si balozi. Kama anasimamia anachokisema na kukuamini kwa nini ajifiche kwenye chaka la "balozi mstaafu?"
 
Sikubaliani na jenerali ktk hili la south Africa:
1. Tz ilikuwa mstari wa mbele ktk kupinga Sera za ukabulu ndio maana iliruhusu kuwa uwanja wa mapambano dhidi ya ubaguzi (mazimbu morogoro)
2: Ktk Africa mashariki ni Kenya pekee ndio waliokuwa wanafanya biashara na Africa kusini ya kibaguzi , Tanzania iligoma kama ishara ya kupinga.
3: Kwa kulipa fadhira kwa Tanzania , Africa kusini imeruhusu watanzania waingie nchini kwao bila viza , nadhani hii NI heshima kubwa na Ina manufaa kwa mtanzania mmoja mmoja kuliko kuita mtaa au wilaya Jina la kiongozi.
"Kumbuka ktk siasa hakuna rafiki au adui wa kudumu !"
 
Balozi Mstaafu ndo yupi!tafadhari Jitokeze tukujadili
Nadhani anamzungumzia Chief Of Staff; Balozi Ombeni Sefuwe.

Nikirudi kwenye mada, Kwa maoni yangu, hapa, ni kama kuna Triangle inazungumziwa...triangle yenyewe ni ile inayounganisha Tanzania, Rwanda na Uganda! Ni kama anazungumza kwamba Tanzania bado haijajifunza kupitia maamuzi ya kukurupuka. Kwamba, kutokana na kukurupuka kwetu, tukajikuta hatuiungi mkono MPLA bila kuangalia usoni...good enough tukajirekebisha! Tukafanya makosa hata katika harakati za Afrika Kusini pale tulipodhani kila chama cha weusi nchini humo kilkuwa ni kwa ajili ya kumkomboa Mwafrika; kumbe tulipotea...kwani hata vijana wa leo tulishuhudia jinsi Inkatha Freedom Part ya Chief Buthelez kilivyokuwa kina-side na Makaburu na kuihujumu ANC! Ikumbukwe kwamba, Dar haikuwa makao makuu ya ANC tu bali hata vyama vingine vilivyojiita vya ukombozi wakati walikuwa wanahujumu wenzao!!

Bila shaka Jenerali Ulimwengu ameacha kwa makusudi kuitaja Uganda coz' I think hapa ndipo ilipojikita hoja yake! Baada ya Dr. Milton Obotte kupinduliwa na Iddi Amin, Obotte alikimbilia Tanzania ambako alipewa hifadhi na Mwalimu. Baada ya Obotte kukimbilia Tanzania, wimbi la wafuasi wake likavuka mpaka na kuingia Tanzania. Obotte, akiwa kwenye ardhi ya Tanzania na wafuasi wake; wakaanzisha harakati za kumpindua Amin ili kumrejesha madarakani. Inasemekana kwamba kule Handeni (wanaotoka huko wanaweza kuthibitisha hili) kulijengwa kambi ya kutoa mafunzo ya kijeshi kwa wafuasi wa Obotte/UPC ili waweze kurudi Uganda na kumpindua Amin. Na kweli, ndani ya mwaka mmoja au mmoja unusu baadae, wafuasi wa Obotte walirudi Uganda na kufanya jaribio la kumpindua Idd Amin. Hata hivyo jaribio hilo lilishindwa.

Kimsingi, pamoja na propaganda za hapa na pale, harakati hizi za kutaka kumrudisha Obotte madarakani ndiyo sababu iliyoleta uhasama kati ya Mwalimu Nyerere na Iddi Amin hadi kufikia Tanzania kuingia vitani na Uganda! Kwa tabia za Amin, ilikuwa ni kama kumpa kichaa rungu huku ukimchezea makalio!!

Hivyo basi, kwa maoni yangu ni kama Jenerali anaamini kwamba Tanzania bado hatujajifunza katika hili linapokuja suala la Tanzania na uhasama wa sasa na Rwanda! Majuma ya hivi karibuni imekuwa ikiripotiwa kuja kwa waasi wa FDLR nchini Tanzania! Kama habari hizi ni kweli, basi ni kweli kwamba Tanzania bado hatujajifunza yale ya Mwalimu na Amin! Mbaya zaidi, "ujaji" huu wa FDLR nchini umekuja wakati ambao tayari Tanzania ikiwa katika hali tete na Rwanda! Ingawaje binafsi ni mtetezi mkubwa wa Tanzania yangu hususani linapokuja suala la external provocation, lazima nikiri wazi kwamba serikali haijatoa maelezo yanayobebeka katika hili hata kama nitaendelea kuitetea! Huku kutotoa majibu ya kuridhisha ndiko bila shaka Jenerali anakokueleza kwamba Matokeo yake ni kuwa na watu kama ‘Balozi Mstaafu’ ambaye kazi yake kuu ni kusema kwamba kila kitu kimekwenda sawa na hakuna cha kubadilisha, ambayo ni falsafa ya Profesa Pangloss wa Voltaire.
 
Generali Ulimwengu siku zote ni mtu wa stress tu, hana jipya. Nadhani haya ameyakumbuka baada ya kukosa kuteuliwa kwenye bunge maalum la Katiba. Huyu na NYARONYO KICHERE ni kundi moja.
 
Maswali:

Hivi kweli Ubalozi wa Tanzania Algeria uko Paris?

Huyu ''Balozi Mstaafu'' anayetajwa na Jenerali ni nani?

Hivi kweli hakuna hata mtaa mmoja South Africa na Angola wenye jina la Nyerere?

Hivi kuna sababu zingine zilizopelekea Mandela kuja Tanzania zaidi ya zile alizotaja JK kwenye mazishi ya Madiba pale Qunu?

Hayo maswali yote aliyauliza ULIMNWENGU , binafsi sijui kama yana tija, Jina la nyerere kutokuwepo au kuwepo kwenye mitaa ya afrika ya kusini au angola , watanzania tunafaidika na nini. NYERERE alishatenda wema akaenda zake, fadhila za nini? ULIMWENGU ana msongo tu wa mawazo, si arudi tu kwao kama anaona Tanzania anakereka?
 
My guess, Atakuwa katibu mkuu kiongozi pale ikulu ombeni sefue aliyekuwa balozi wa Tanzania UN kabla ya kuja ikulu maana .

Ila mbona Ulimwengu kaandika too low,..au I'm missing a point.!

Hata kama ni yeye, so what?
 
Back
Top Bottom