Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Mirisho Sarakikya, ameshangazwa na tabia ya baadhi ya watumishi wa serikali kuibuka na utajiri baada ya kufanya kazi kwa muda mfupi tu. Alisema huko nyuma watumishi waliitumikia serikali kwa miaka mingi na kustaafu wakiwa watu wa kawaida.
Alisema kuwa kwa siku za karibuni amekuwa anashangazwa na baadhi ya watu kujenga majengo makubwa yasiyolingana na mapato halali wanayolipwa na kuongeza kuwa anafahamu mishahara ya watumishi wa umma hakuna mwenye uwezo wa kujenga majengo hayo na kwa muda mfupi.
Jenerali Sarakikya alitoa kauli hiyo mjini Arusha jana, alipokuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa Muungano wa Wanajeshi Wastaafu Tanzania (Muwawata).
Mimi mwenyewe nilikuwa Mbunge, kisha nikawa waziri na kumalizia ubalozi na kustaafishwa rasmi na Jeshi mwaka 2004, bado sikuweza kujenga nyumba ya kifahari, bali nimejenga kibanda tu cha kuishi tena kwa miaka 10, iweje watu wajenge majengo hayo kwa muda mfupi? Alihoji Jenerali Sarakikya.
Katika hatua nyingine, Jenerali Sarakikya ameilalamikia serikali kwa kulipa kiwango kidogo cha posho ya pensheni kwa wanajeshi wastaafu ya Sh. 300,000 baada ya miezi sita sawa na Sh. 50,000 kwa mwezi.
Jenerali Sarakikya alisema posho hiyo haiwezi kufanya kitu chochote kulingana na hali halisi ya maisha kwa sasa na wengi wao hujikuta katika wakati mgumu. Alisema kwa mujibu wa taratibu za jeshi, wanajeshi wengi hujikuta wanastaafu kwa vyeo vyao na sio kwa umri, jambo ambalo alisema wengi wao wanastaafu wakiwa bado wana nguvu za kutumikia taifa katika nyanja mbalimbali.
Nipashe
Alisema kuwa kwa siku za karibuni amekuwa anashangazwa na baadhi ya watu kujenga majengo makubwa yasiyolingana na mapato halali wanayolipwa na kuongeza kuwa anafahamu mishahara ya watumishi wa umma hakuna mwenye uwezo wa kujenga majengo hayo na kwa muda mfupi.
Jenerali Sarakikya alitoa kauli hiyo mjini Arusha jana, alipokuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa Muungano wa Wanajeshi Wastaafu Tanzania (Muwawata).
Mimi mwenyewe nilikuwa Mbunge, kisha nikawa waziri na kumalizia ubalozi na kustaafishwa rasmi na Jeshi mwaka 2004, bado sikuweza kujenga nyumba ya kifahari, bali nimejenga kibanda tu cha kuishi tena kwa miaka 10, iweje watu wajenge majengo hayo kwa muda mfupi? Alihoji Jenerali Sarakikya.
Katika hatua nyingine, Jenerali Sarakikya ameilalamikia serikali kwa kulipa kiwango kidogo cha posho ya pensheni kwa wanajeshi wastaafu ya Sh. 300,000 baada ya miezi sita sawa na Sh. 50,000 kwa mwezi.
Jenerali Sarakikya alisema posho hiyo haiwezi kufanya kitu chochote kulingana na hali halisi ya maisha kwa sasa na wengi wao hujikuta katika wakati mgumu. Alisema kwa mujibu wa taratibu za jeshi, wanajeshi wengi hujikuta wanastaafu kwa vyeo vyao na sio kwa umri, jambo ambalo alisema wengi wao wanastaafu wakiwa bado wana nguvu za kutumikia taifa katika nyanja mbalimbali.
Nipashe