Jenerali Reuben Kaduma awa Katibu wa CHADEMA Kanda ya Magharibi

Malova

JF-Expert Member
Apr 21, 2011
784
228
Jenerali Reuben Kaduma ni mmoja kati ya Makatibu kumi (10) wa Kanda ambao wametuliwa hivi karibuni kusimamia shughuli za chama katika Kanda zao. Yeye amepangiwa Kanda ya Magharibi inayoundwa na Mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma.

Itakumbukwa kuwa CHADEMA kimegawanya Mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani katika Kanda kumi ili kurahisisha zoezi la kuwafikia wananchi kwa haraka. Kanda hizo na mikoa yake katika mabano ni Kasazini (Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga) , Pwani (Pwani na Dar Es Salaam), Ziwa Victoria (Mwanza, Kagera na Geita), Serengeti (Shinyanga, Simiyu na Mara), Kati (Singida, Dodoma na Morogoro), Nyasa (Mbeya, Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa), Kusini (Lindi, Mtwara na Ruvuma), Pemba (Kaskazini Pemba na Kusini Pemba) na Unguja (Kaskazini Unguja, Kusini Unguja na Mjini Magharibi).

Tunakutakia kila la kheri katika kazi yako hiyo mpya
 
Haswaaaa..... Wanajeshi si Wakuu wa Wilaya peke yao. Hata CHADEMA wapo
 
Jenerali Reuben Kaduma ni mmoja kati ya Makatibu kumi (10) wa Kanda ambao wametuliwa hivi karibuni kusimamia shughuli za chama katika Kanda zao. Yeye amepangiwa Kanda ya Magharibi inayoundwa na Mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma.

Itakumbukwa kuwa CHADEMA kimegawanya Mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani katika Kanda kumi ili kurahisisha zoezi la kuwafikia wananchi kwa haraka. Kanda hizo na mikoa yake katika mabano ni Kasazini (Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga) , Pwani (Pwani na Dar Es Salaam), Ziwa Victoria (Mwanza, Kagera na Geita), Serengeti (Shinyanga, Simiyu na Mara), Kati (Singida, Dodoma na Morogoro), Nyasa (Mbeya, Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa), Kusini (Lindi, Mtwara na Ruvuma), Pemba (Kaskazini Pemba na Kusini Pemba) na Unguja (Kaskazini Unguja, Kusini Unguja na Mjini Magharibi).

Tunakutakia kila la kheri katika kazi yako hiyo mpya
Tunamtakia kila la kheri Jenerali aisongeshe cdm ili mwaka 2020 tuisambaratishe ccm imani
 
nadhani hiyo jenerali ni jina tu,la si jina tu basi atakua mstaafu.mleta uzi ungeuongezea nyama uzi wako
 
hakuna generali wa jina hilo tz iwe kastaafu au kazini bado. mbona wengi wenye majina hayo. yupo generali ulimwengu pia
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom