Jenerali 'Msauzi' Azungumza Kiswahili Msiba wa Mandela!

Mkuu, hivyo ndivyo ilivyoelezwa na Nyerere siku hiyo ya Tarehe 12 April, 1984. Mie hadi leo naamini kuwa Sokoine alifia Dodoma na mwili wakaubeba kama Mzima na kwenda kucheza film ya ameuawa kwa ajali ya gari hapo Dakawa (Masahihisho, siyo Kongwa). Naamini hivyo kwa sababu siku hiyo asubuhi, niliona ndege ya Rais ikija kumchukua yeye Sokoine kama PM hapo Dodoma na jioni nikasikia kafa kwa ajali ya gari. Hadi leo siamini kuwa aligoma kupanda ndege na akapanda gari. Nafikiri walimwambia Rubani wewe rudi, jamaa anakuja kwa gari.

Hii ilikuwa baada ya kikao cha Bunge Dodoma na akatoa Mkwara mzito sana kuwa waliozembea kwenye kilimo na sasa wananchi watakumbwa na njaa, wataonana Dodoma. Wakamuwahi yeye na hakuna aliyekiona cha moto.

Tulivyoambiwa: PM Sokoine akitokea Dodoma na msafara wake, walipofika eneo la Dakawa, walikutana na gari la Mpigania Uhuru kutoka South Africa akielekea eneo la Kongwa walikokuwa wakiishi. Jamaa alikuwa akiendesha Mitsubishi Pajero. Mbele yalikuwepo magari matatu na nyuma ndiyo gari la Sokoine. Nashindwa kujua kwa nini PAJERO ya Dube haikusimama na kuupisha msafara kama ilivyo kawaida. Polisi na magari matatu ya mwanzo pia wakaruhusu lile gari lipite na mwendo kasi na lilivyofika gari la Sokoine, eti gari la Dube likaacha njia na kuingia kuligonga gari la Sokoine na kwenye hiyo ajali, akaja kufa Sokoine peke yake.

Dube alionyeshwa yupo Hospital chini ya ulinzi eti kavunjika mguu.

Kipindi hicho ndiyo ilikuwa zimeingia Pajero kwa wingi Tanzania pamoja na Note za Tsh 500. Hapo ndipo Tsh 500 ikaitwa PAJERO na Pajero zenyewe zikaanzwa kuitwa DUBE.

Baadaye miaka ya 80 mwishoni, Tanzania zikaanza kuingia nyimbo za Lucky Dube na hivyo kuwa Dube wa pili maarufu Tanzania, Afrika na dunia nzima....

Benzi la Sokoine likiwa hoi......

sokoine-car_thumb.jpg


Lucky Dube Old School: Lucky Dube (RIP) - Ive got you babe - YouTube kutoka SLAVE Album.
Ndugu samahani kama hutajali,hebu nielezee khs sokoine kufia Kongwa na huyo Dube ndo nani?plz
 
Mkuu, nimefanya utafiti kidogo na nakubali maneno yako kuwa ajali ilitokea Dakawa ambapo leo hii wameweka Sanamu. Ni siku nyingi kidogo maana ni kama miaka 30 hadi leo hii. Ila kama sikosei, huyu Dube ndiyo alikuwa akielekea Kongwa akitokea Morogoro na Sokoine akitokea Dodoma.

Ni miaka kadhaa iliyopita ndipo nilikuja kufahamu kuwa Kongwa kulikuwa na Kambi ya Wanajeshi wakati Mazimbu kulikuwa na Wakimbizi na sanasana Wanasiasa na Wanawake/Watoto huku Vijana wakila shule ya kuuwa.
Ulimolaaa?Panga kaya?....makopa na nyanya ntole zipo?....hebu tuwekee kumbukumbu sawa..alifia Kongwa au pale Dakawa,ambapo panaitwa Dakawa -Sokoine??Jirani na Wami-Dakawa?....#TeamWekaPicha #
 
Habari

IBADA YA MANDELA


Waandishi Wetu

Toleo la 329 11 Dec 2013


329_obama.jpg



  • Kigogo ANC asema mbingu zimeandaa zulia jekundu, Kiswahili chasikika


JINA la Tanzania na Lugha ya Kiswahili jana Jumanne, vilitajwa na kuzungumzwa wakati wa ibada ya kumuombea Nelson Mandela, iliyofanyika katika Uwanja wa FNB jijini Johannesburg, Afrika Kusini, huku Rais wa Marekani, Barack Obama, akiwaumbua baadhi ya viongozi wanafiki.


Kutokana na hotuba hiyo ya Obama, baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa vimetafsiri kuwa maneno ya Obama kwamba wapo viongozi wanafiki wanaojidai kuunga mkono mshikamano kama ilivyo kwa Mandela lakini hawafanyi hivyo kwa wananchi wao, yamewalenga Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na Raul Castro wa Cuba.


Ibada hiyo ya aina yake ilikuwa ni fursa ya viongozi kutoka kote duniani na wananchi wa Afrika Kusini kumuombea na kutafakari kuhusu maisha ya kiongozi huyo aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita akiwa na umri wa miaka 95.


Wakati akitambulisha wageni mashuhuri kwenye ibada hiyo jana, mmoja wa washereheshaji katika shughuli hiyo, Baleka Mbete, alimtambulisha Rais Jakaya Kikwete aliyekuwepo uwanjani hapo kwa kusema; "Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, karibu mgeni wetu."


Lugha rasmi iliyokuwa ikitumika jana ilikuwa ni Kiingereza na Kikwete ni kiongozi pekee kutoka nje ya Afrika Kusini ambaye alikaribishwa uwanjani hapo kwa kutumia lugha hiyo.


Mbete ni mmoja wa wanasiasa mashuhuhuri nchini Afrika Kusini na aliwahi kuwa Makamu Rais wa nchi hiyo lakini katika miaka ya sabini alikuwa mmoja wa wapigania uhuru waliokimbia kutoka nchini humo na kuja kuishi Tanzania.


Rais Kikwete aliyekuwa miongoni mwa viongozi wa mwanzo kuingia katika uwanja huo, alitabasamu tu wakati Mbete akimkaribisha.


Ibada ya jana ilihudhuriwa na karibu viongozi wote wakubwa duniani na tayari inasemwa ni miongoni mwa ibada kubwa za kuwahi kufanyika duniani baada ya ile ya mazishi ya Papa John Paul II.


Katika hotuba ya kusisimua, Rais Barack Obama wa Marekani alisema maisha ya Mandela ndiyo yamemfanya yeye apate wadhifa alionao sasa na kusema ingawa dunia sasa ni sehemu nzuri kuliko miaka 40 iliyopita, bado kuna safari ndefu ya kufikia dunia yenye fursa sawa, demokrasia na kuheshimiana.


"Wako viongozi wengine hapa ambao wanajifanya kumheshimu na kusifia maisha ya Mandela lakini kwenye nchi zao hawana uvumilivu kwa watu ambao wana mawazo nao tofauti au wana imani tofauti za kidini au kiitikadi," alisema Obama.


Obama alitumia hotuba yake iliyokuwa ikishangiliwa mara kwa mara na wananchi kumfananisha Mandela na viongozi waliotangulia mbele ya haki kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King na Abraham Lincoln; akisema wote hao wamechangia katika kuifanya dunia kuwa sehemu salama zaidi.


Katika tukio hilo la jana-Jumanne, baadhi ya viongozi waliohudhuria walishangiliwa na umati uliojitokeza huku wengine wakizomewa na wananchi kwa sababu mbalimbali.


Miongoni mwa walioshangiliwa sana ni Obama, Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Mahmoud Abbas wa Palestina, Rais mstaafu wa nchi hiyo, Thabo Mbeki na mtalaka wa Mandela, Winnie-Madikizela.


Makamu wa Rais wa China, Li Yuanchao, alizomewa na wahudhuriaji katika kile kinachoelezwa wananchi wa Afrika Kusini kutofurahishwa na namna China inavyochangia kidogo katika vita dhidi ya Ukimwi.


Mshereheshaji Mkuu katika tukio la jana, Cyril Ramaphosa, mara kwa mara alikuwa akikatisha hotuba za viongozi na kuwataka wananchi kuwa wasikivu ili wageni waone namna wana Afrika Kusini walivyomuheshimu kiongozi wao huyo.


Awali, Ramaphosa, ambaye pia Naibu Rais wa ANC, alisema mvua ambayo iliyonyesha siku nzima ya jana Jumanne ni dalili kwamba mbingu tayari imeandaa kapeti jekundu kwa ajili ya kumpokea Mandela.


Mara baada ya ibada ya jana, mwili wa Mandela unatarajiwa kusafirishwa kupelekwa jijini Pretoria ambako watu wataanza kutoa heshima zao za mwisho kuanzia leo asubuhi. Mandela anatarajiwa kuzikwa Jumapili hii kijijini kwake Qunu.


Soma zaidi kuhusu:


- See more at: Raia Mwema - Obama aumbua wanafiki
 
"Wako viongozi wengine hapa ambao wanajifanya kumheshimu na kusifia maisha ya Mandela lakini kwenye nchi zao hawana uvumilivu kwa watu ambao wana mawazo nao tofauti au wana imani tofauti za kidini au kiitikadi," alisema Obama.

Nimekupata mkuu
 
Naye Obama aache unafiki,kuna nchi inapenda ubabe kama USA!wao democrasia ni kufuata yale wanayoyataka ukibisha basi ww dikteta na watakuundia njama mpk unapinduliwa au kuuawa kabisa.

OBAMA kuna utofauti... KATIBA YAO IMEANDIKWA na KUBEBA UMWAMBA wa DUNIA... na ukiangalia RAIS wa nchi hana NGUVU kupita KATIBA au VYOMBO vya SHERIA kama BUNGE; MAJAJI; POLISI wanaweza kumshitaki au kumuondoa MADARAKANI... Sio kama Marais wetu wa KIAFRIKA wana NGUVU zaidi hata ya MUNGU

Sasa OBAMA akiongelea vitu kama hivyo Anamaanisha KWELI lakini sio kwamba ataweza kushawishi NGUZO ZOTE ZA SHERIA NCHINI kwake wakubaliane nae... HIYO NDIO DEMOKRASIA na NI KATIBA yao imeashiria hayo...

Kwahiyo MENGI Angependa kuyabadilisha lakini sio kwa Mkono wake Mmoja watamuita BUNGENI to be IMPEACHED...
 
the issue here is whether you still have a space in your brain cubicle to think a little bit more, SA has not helped any African state to confront their poor economic situations including TZ which was dearly close and still stands on their side come rain or sun when it comes to political opinions.

My brain might be microbrain compared to your super big brain but its enough to think that its not their duty to do so. They are not obligated to do that. They have enough of their problems to add us in the list.

I still insist with my small brain intact, we have to solve our own problems and SA are free to do anything with their economy! We have all these resources that we need to use!
 
If you are talking about freedom in its own context, you are right Stefano, I thought we were going through human moral obligations as well. It is through moral reality Mandela went here and there looking for support, this in human sense has to be reciprocated unless if they prove it otherwise.
 
Wengine asili yao ni wabongo walienda huko miaka hiyo. So wanakuja huku kusalimia ndg zao
 
Mkuu, hivyo ndivyo ilivyoelezwa na Nyerere siku hiyo ya Tarehe 12 April, 1984. Mie hadi leo naamini kuwa Sokoine alifia Dodoma na mwili wakaubeba kama Mzima na kwenda kucheza film ya ameuawa kwa ajali ya gari hapo Dakawa (Masahihisho, siyo Kongwa). Naamini hivyo kwa sababu siku hiyo asubuhi, niliona ndege ya Rais ikija kumchukua yeye Sokoine kama PM hapo Dodoma na jioni nikasikia kafa kwa ajali ya gari. Hadi leo siamini kuwa aligoma kupanda ndege na akapanda gari. Nafikiri walimwambia Rubani wewe rudi, jamaa anakuja kwa gari.

Hii ilikuwa baada ya kikao cha Bunge Dodoma na akatoa Mkwara mzito sana kuwa waliozembea kwenye kilimo na sasa wananchi watakumbwa na njaa, wataonana Dodoma. Wakamuwahi yeye na hakuna aliyekiona cha moto.

Tulivyoambiwa: PM Sokoine akitokea Dodoma na msafara wake, walipofika eneo la Dakawa, walikutana na gari la Mpigania Uhuru kutoka South Africa akielekea eneo la Kongwa walikokuwa wakiishi. Jamaa alikuwa akiendesha Mitsubishi Pajero. Mbele yalikuwepo magari matatu na nyuma ndiyo gari la Sokoine. Nashindwa kujua kwa nini PAJERO ya Dube haikusimama na kuupisha msafara kama ilivyo kawaida. Polisi na magari matatu ya mwanzo pia wakaruhusu lile gari lipite na mwendo kasi na lilivyofika gari la Sokoine, eti gari la Dube likaacha njia na kuingia kuligonga gari la Sokoine na kwenye hiyo ajali, akaja kufa Sokoine peke yake.

Dube alionyeshwa yupo Hospital chini ya ulinzi eti kavunjika mguu.

Kipindi hicho ndiyo ilikuwa zimeingia Pajero kwa wingi Tanzania pamoja na Note za Tsh 500. Hapo ndipo Tsh 500 ikaitwa PAJERO na Pajero zenyewe zikaanzwa kuitwa DUBE.

Baadaye miaka ya 80 mwishoni, Tanzania zikaanza kuingia nyimbo za Lucky Dube na hivyo kuwa Dube wa pili maarufu Tanzania, Afrika na dunia nzima....

Benzi la Sokoine likiwa hoi......

sokoine-car_thumb.jpg


Lucky Dube Old School: Lucky Dube (RIP) - Ive got you babe - YouTube kutoka SLAVE Album.

Sahihisho:
Mkuu Sikonge, Gari alilotumia Dumisan Dube ni TOYOTA Landcruiser na siyo Mitsubishi Pajero.
 
This is where the point is....... Kiswahili juu

wenyewe wanasema ni romantic language pia........km mtu hajui kabisa kiswahili..alafu awasikilize,,, anaona mnaongea lugha tamu sana....sasa uwe hujui kichina au kisandawe alafu uwasikilize....hapo....mbona utahama eneo gafla
 
Back
Top Bottom