Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Mkuu, hivyo ndivyo ilivyoelezwa na Nyerere siku hiyo ya Tarehe 12 April, 1984. Mie hadi leo naamini kuwa Sokoine alifia Dodoma na mwili wakaubeba kama Mzima na kwenda kucheza film ya ameuawa kwa ajali ya gari hapo Dakawa (Masahihisho, siyo Kongwa). Naamini hivyo kwa sababu siku hiyo asubuhi, niliona ndege ya Rais ikija kumchukua yeye Sokoine kama PM hapo Dodoma na jioni nikasikia kafa kwa ajali ya gari. Hadi leo siamini kuwa aligoma kupanda ndege na akapanda gari. Nafikiri walimwambia Rubani wewe rudi, jamaa anakuja kwa gari.
Hii ilikuwa baada ya kikao cha Bunge Dodoma na akatoa Mkwara mzito sana kuwa waliozembea kwenye kilimo na sasa wananchi watakumbwa na njaa, wataonana Dodoma. Wakamuwahi yeye na hakuna aliyekiona cha moto.
Tulivyoambiwa: PM Sokoine akitokea Dodoma na msafara wake, walipofika eneo la Dakawa, walikutana na gari la Mpigania Uhuru kutoka South Africa akielekea eneo la Kongwa walikokuwa wakiishi. Jamaa alikuwa akiendesha Mitsubishi Pajero. Mbele yalikuwepo magari matatu na nyuma ndiyo gari la Sokoine. Nashindwa kujua kwa nini PAJERO ya Dube haikusimama na kuupisha msafara kama ilivyo kawaida. Polisi na magari matatu ya mwanzo pia wakaruhusu lile gari lipite na mwendo kasi na lilivyofika gari la Sokoine, eti gari la Dube likaacha njia na kuingia kuligonga gari la Sokoine na kwenye hiyo ajali, akaja kufa Sokoine peke yake.
Dube alionyeshwa yupo Hospital chini ya ulinzi eti kavunjika mguu.
Kipindi hicho ndiyo ilikuwa zimeingia Pajero kwa wingi Tanzania pamoja na Note za Tsh 500. Hapo ndipo Tsh 500 ikaitwa PAJERO na Pajero zenyewe zikaanzwa kuitwa DUBE.
Baadaye miaka ya 80 mwishoni, Tanzania zikaanza kuingia nyimbo za Lucky Dube na hivyo kuwa Dube wa pili maarufu Tanzania, Afrika na dunia nzima....
Benzi la Sokoine likiwa hoi......
Lucky Dube Old School: Lucky Dube (RIP) - Ive got you babe - YouTube kutoka SLAVE Album.
Hii ilikuwa baada ya kikao cha Bunge Dodoma na akatoa Mkwara mzito sana kuwa waliozembea kwenye kilimo na sasa wananchi watakumbwa na njaa, wataonana Dodoma. Wakamuwahi yeye na hakuna aliyekiona cha moto.
Tulivyoambiwa: PM Sokoine akitokea Dodoma na msafara wake, walipofika eneo la Dakawa, walikutana na gari la Mpigania Uhuru kutoka South Africa akielekea eneo la Kongwa walikokuwa wakiishi. Jamaa alikuwa akiendesha Mitsubishi Pajero. Mbele yalikuwepo magari matatu na nyuma ndiyo gari la Sokoine. Nashindwa kujua kwa nini PAJERO ya Dube haikusimama na kuupisha msafara kama ilivyo kawaida. Polisi na magari matatu ya mwanzo pia wakaruhusu lile gari lipite na mwendo kasi na lilivyofika gari la Sokoine, eti gari la Dube likaacha njia na kuingia kuligonga gari la Sokoine na kwenye hiyo ajali, akaja kufa Sokoine peke yake.
Dube alionyeshwa yupo Hospital chini ya ulinzi eti kavunjika mguu.
Kipindi hicho ndiyo ilikuwa zimeingia Pajero kwa wingi Tanzania pamoja na Note za Tsh 500. Hapo ndipo Tsh 500 ikaitwa PAJERO na Pajero zenyewe zikaanzwa kuitwa DUBE.
Baadaye miaka ya 80 mwishoni, Tanzania zikaanza kuingia nyimbo za Lucky Dube na hivyo kuwa Dube wa pili maarufu Tanzania, Afrika na dunia nzima....
Benzi la Sokoine likiwa hoi......
Lucky Dube Old School: Lucky Dube (RIP) - Ive got you babe - YouTube kutoka SLAVE Album.
Ndugu samahani kama hutajali,hebu nielezee khs sokoine kufia Kongwa na huyo Dube ndo nani?plz