Jeneral Ulimwengu: Huu ni utawala wa milipuko! Wafanyakazi wanafanya kazi kwa uoga

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,024
24,374
Akiwa katika mahojiano na kituo cha radio cha DW leo 31.12.2016 Jenerali Ulimwengu ameeleza ni kwa jinsi gani utawala huu ulivyo wa milipuko, kwamba inatokea matamko yanatolewa asubuhi kisha jioni yanabadilishwa.

Amebainisha wazi pia wafanyakazi wengi wa umma wanafanya kazi kwa uoga bila kujiamini ili wawafurahishe watawala kwa kuogopa kutumbuliwa.

Ameeleza pia jinsi ambavyo JPM alivyokiri hapo awali kuwa ameshindwa kwani alitamani muhula wa uongozi upunguzwe lakini baadaye akabatilisha na kusema ataaendelea.

Hii ni dalili tosha kwamba kwa yanayotokea kwa sasa hayataleta ufanisi mkubwa kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi na kwamba itachukua muda sana kuweza kupata mustakabali wa hali iliyopo kwa sasa!
 
Awamu hii tunaendelea kushuhudia kauli, na tungo za kila aina zinazofadhiliwa na mafisadi!

Mkuu sasa hv aibu imewakumba, na nyie ndio mliochangia kumpotosha mkuu, alipokuwa anafanya mambo bila kufuata utaratibu mliona sawa mkidhani anawakomoa wapinzani. Sasa umeme umepanda, je ni hao mafisadi unaowataja? Hakuna kiwanda hata kimoja kilichojengwa kwa wakati wake.

Maamuzi anachukua mwenyewe hata yanayohitaji maamuzi ya wengi (bunge). Unasikia mishahara haipandi na waliojiriwa kawatoa lakini anahubiri hapa kazi tu. Ukimuuliza kazi ziko wapi anasema watu wachape kazi kwelikweli.

Saa hii hata nyie wapiga tarumbeta mmebaki kusema sijui ufipa, mara wachaga wezi, lakini hakuna anayeonyesha kiwanda!!
 
Tulizoea awamu ya mzamo hii ya mlipuko inashtua na kuamsha walolala
 
36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom