Mtailaumu serikali lakini ukumbuke wafanyakazi wote wa serikali hawafiki laki saba, ukumbuke tupo watanzania zaidi ya milioni 55 na zaidi kila siku watu wanasoma hivo lazima tubadili mitazamo yetu kwanza na kubadili mfumo wa elimu yetu ili tusonge mbele zaidi maana duniani kote ni sekta binafsi ndio imeajiri watu wengi kuliko sekta ya umma hivo tupambane ili kuipigania sekta binafsi isianguke izidi kukua na kuleta mapinduzi kwenye maisha ya vijana wetu pia.