Jee waandishi wa habari wa Tanzania wana-abuse power waliokuwa nayo??

Mar 30, 2007
86
1
JF,

Watanzania wengi wanapoamka asubuhi kwenda ofisini, kabla hawajaingia ofsini wanatupa macho yao kwenye vichwa vya habari vya magezeti!!!

Tukiangalia kwa kina tutaona kwamba waandishi wa habari wa Tanzania wananguvu kubwa sana. Yaani mpaka hatari! Waandishi wa habari wamekuwa wakimanipulate habari nyingi na tukizipindua wanavyotaka wao!..

Watanzania wanasoma sana magazeti. Na infact wanaamini sana magazeti!

Waandishi wetu wakobiased ile mbaya!...... Hawa hawa waandishi wanaotuandikia habari za viongozi mafisadi wao wenyewe wengi wao ni mafisadi na wanafanya kazi na hao (hidden) expert fisadis!...

Waandishi ama mass media ni chombo muhimu kwenye jamii!!! Jee tunakubali kutawaliwa na waandishi waongo,mafisadi na wanafki waliokosa uzelendo kazi kuchochea fitna na uhasama baina yetu?
 
Toa mifano kidogo (mingi siyo vibaya) ili kujenga kesi yako au kile unachobase swali lako. Na kwa vile wamo humu nina uhakika hawatasita kukujibu.
 
Toa mifano kidogo (mingi siyo vibaya) ili kujenga kesi yako au kile unachobase swali lako. Na kwa vile wamo humu nina uhakika hawatasita kukujibu.


1. Kuna magazeti yanajulikana kwa ku RE-WRITE habari za zamani na kulichochea swala ambalo limetatuliwa au limepita just kuamsha hisia za watu na kuharibu jina!....
 
Waandishi wa habari wa Tanzania wengi wanafanya kazi vizuri kabisa, ukiondoa wahuni wachache wanaotumiwa na mafisadi kuandika kile ambacho mafisadi wanataka kiandikwe au kisiandikwe katika magazeti yaTanzania.

Magazeti ndiyo yamekuwa mstari wa mbele kufichua uozo mbali mbali wa hali ya juu uliokuwa ukifanywa na viongozi mafisadi wangazi za juu akiwemo fisadi Mkapa. Wamekuwa mstari wa mbele katika kuibua uozo wa mbali mbali ndani ya BoT kama vile EPA, fisadi mkono kulipwa bilioni 8 ambazo hakustahili, fisadi Mzindakaya kupatiwa mkopo na BoT pamoja na kwamba BoT hawatoi mikopo kama hiyo bali benk za biashara, gharama kubwa kupita kiasi za ujenzi wa Twin Towers, kuajiriwa kwa watoto wa 'viongozi ambao hawana quaifications zozote za kuajiriwa BoT na mengi mengineyo yakiwemo ya mkataba wa Buzwagi, Richmond n.k.

Hata mabalozi mbali mbali wa nchi za wafadhili zikiwemo US, UK, Holland, Germany, Denmark n.k. wamewasifia waandishi wa habari wa Tanzania kwa kufichua maovu mengi ndani ya CCM na SIRI KALI. Hata wanahabari wa CNN na BBC mashirika makubwa ya habari duniani huwa wanafanya makosa mara nyingi na kuomba samahani.

Hivyo tusiwakatishe tamaa waandishi wa habari wa Tanzania ambao wengi wao wanafanya kazi yao vizuri sana ukiondoa wahuni wachache.
 
Waandishi wa habari wa Tanzania wengi wanafanya kazi vizuri kabisa, ukiondoa wahuni wachache wanaotumiwa na mafisadi kuandika kile ambacho mafisadi wanataka kiandikwe au kisiandikwe katika magazeti yaTanzania.

Magazeti ndiyo yamekuwa mstari wa mbele kufichua uozo mbali mbali wa hali ya juu uliokuwa ukifanywa na viongozi mafisadi wangazi za juu akiwemo fisadi Mkapa. Wamekuwa mstari wa mbele katika kuibua uozo wa mbali mbali ndani ya BoT kama vile EPA, fisadi mkono kulipwa bilioni 8 ambazo hakustahili, fisadi Mzindakaya kupatiwa mkopo na BoT pamoja na kwamba BoT hawatoi mikopo kama hiyo bali benk za biashara, gharama kubwa kupita kiasi za ujenzi wa Twin Towers, kuajiriwa kwa watoto wa 'viongozi ambao hawana quaifications zozote za kuajiriwa BoT na mengi mengineyo yakiwemo ya mkataba wa Buzwagi, Richmond n.k.

Hata mabalozi mbali mbali wa nchi za wafadhili zikiwemo US, UK, Holland, Germany, Denmark n.k. wamewasifia waandishi wa habari wa Tanzania kwa kufichua maovu mengi ndani ya CCM na SIRI KALI. Hata wanahabari wa CNN na BBC mashirika makubwa ya habari duniani huwa wanafanya makosa mara nyingi na kuomba samahani.

Hivyo tusiwakatishe tamaa waandishi wa habari wa Tanzania ambao wengi wao wanafanya kazi yao vizuri sana ukiondoa wahuni wachache.

Mimi bado napata shaka katika hayo ya kufichuwa maovu!... Wanafanya wao wynyewe au wanalipwa na wakubwa, na kambiwa nani wamharibie jina!... na kuongeza uongo kidogo!.....

Maana ukiamuliwa kuondesha sehemu! waandishi wa habari ndio weapon nzuri....

Habari wanazoandika ni SADIKI ukipenda!!!
 
kituko cha TANZANIA DAIMA wikiendi hii:
WAZIRI wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Musa Hassan na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Ramadhan Dau wasomi wazalendo na wacha Mungu mnaoheshimika, bado wananchi wanawalilia.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/8/2/makala1.php

Ok inawezekana ikawa mara moja ni bahati mbaya...lakini huyu mwandishi wa gazeti la Mbowe akakisha likaendelea kuonyesha ujinga na uvivu wa kufikiri na kufanya research kwa kudai hivi:



Nafahamu kabisa Mwenyekiti wa Bodi ya NSSF, Dk. Hassan naye ni mswahilina mzuri na anayeheshimika ukiachia nafasi kubwa ya usomi aliyonayo, amebeba dhamana kubwa ya kuiongoza bodi inayojali na kuzingatia kwa dhati haki za binadamu.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/8/2/makala1.php


UKWELI WA NANI MWENYEKITI WA BODI YA NSSF HUU HAPA:


http://www.nssf.or.tz/board_of_trustees.php


Jamani tuache ushabiki halafu tuangalie hili gazeti FREEMAN MBOWE LINAVYOOAJIRI makanjanja



hivi huyu kweli ndio Dr MUSSA HASSAN au kajibadilisha?
b_nyoni.gif

Mrs. Blandina Nyoni
Board Chairperson
National Social Security Fund
Dar es salaam


hivi wanashindwa kuingia JAMII FORUMS kutafuta referencing kama KUBENEA na MWANAHALISI?

What a shame!
 
Mimi bado napata shaka katika hayo ya kufichuwa maovu!... Wanafanya wao wynyewe au wanalipwa na wakubwa, na kambiwa nani wamharibie jina!... na kuongeza uongo kidogo!.....

Maana ukiamuliwa kuondesha sehemu! waandishi wa habari ndio weapon nzuri....

Habari wanazoandika ni SADIKI ukipenda!!!

Wewe kama bado unapata shaka hilo ni tatizo lako, lakini wengi wa Watanzania tunaamini kwamba waandishi wengi wa habari utendaji wao wa kazi ni mzuri. Naam wako wahuni wachache wanaotumiwa, lakini huwezi kuwachafulia majina watu kama RA, Lowassa, na Mkapa wakashindwa kuja na ushahidi wa kuonyesha kile kilichoandikwa na magazeti ni uzushi mtupu!!!! Na siku zinayoyoma bila kusikia chochote toka kwao

Tulisikia RA kuwashtaki Mwanahalisi kwa kumchafulia reputation yake, lakini hadi hii leo hajafanya hivyo. Tukasikia tena Lowassa akitamka kuwashtaki hao hao mwanahalisi hadi hii leo hajafanya hivyo!!! Tukasikia tena kwamba fisadi Mkapa atayashtaki magazeti yote yanayomchafua kuhusiana na ufisadi alioufanya wakati akiwa Ikulu, hadi hii leo bado n bubu na hata anazikacha shughuli za chama na serikali ambazo alistahili kuhudhuria.

Mabalozi toka nchi za wafadhili walikuwa wanasoma Newsweek, Times, The Guardian la UK na magazeti mbali mbali ya nje lakini hivi sasa wanasoma baadhi ya magazeti yetu yakiwemo THIS DAY, THE CITIZEN na mengineyo na kusifia yale wanayasoma ndani ya magazeti hayo
 
Lakini siku za nyuma kuna mwana JF alitoa analysis juu ya waandishi Tanzania na alimzungumzia mhariri wa TANZANIA DAIMA au tuseme gazeti la FREEMAN MBOWE kwa kusema hivi:




7. Absalom Kibanda – The editor of Tanzania Daima is really an attack pit-bull that Freeman Mbowe unleashes once in a while. (Deodatus Balile is a pitbull for Rostam Aziz). The problem with Kibanda is the "Mbeya problem". He hasn't gotten over the fact that Mwandosya lost to JK fairly and squarely in 2005.

source: https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=13378&highlight=Stan+Katabalo

need i say more?
 
Lakini siku za nyuma kuna mwana JF alitoa analysis juu ya waandishi Tanzania na alimzungumzia mhariri wa TANZANIA DAIMA au tuseme gazeti la FREEMAN MBOWE kwa kusema hivi:






source: https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=13378&highlight=Stan+Katabalo

need i say more?

GT
watakwambia wewe ni mnafiki na huwatakii mema ktk mafanikio ya kisiasa na kihabari,kwani wewe hujui kua Tanzania daima ndilo gazeti pekee ambalo halitumiwi na RA na siku zote linaandika ukweli mtupu.
 
Kama nilivyosema kuna wahuni wachache katika fani ya uandishi kama ilivyo katika fani yoyote ile Tanzania na hata duniani zikiwemo uhandisi, uhasibu, udaktari n.k. Pamoja na kuwa na hao wahuni wachache waandishi wa habari wengi wanafuata miiko ya taaluma na wanafanya kazi nzuri sana ambayo imetufahamisha uozo mwingi na wa kutisha uliofanywa na mafisadi ndani ya chama na serikali hata kumwagiwa sifa kem kem na mabalozi wa nchi mbali mbali za wafadhili na hata baadhi ya wabunge wa bunge letu uchwara wamewamwagia sifa kem kem. Sikubaliani na msemo usemao kwamba "samaki mmoja akioza basi wote wameoza" Kuna wahuni wachache katika taaluma hiyo lakini kuwatuhumu waandishi wa habari wote kamwe si kuwatendea haki hata kidogo wale wengi ambao ni wazuri.
 
Ngoja nishangae kwanza. Mwanzisha thread amezungumzia WAANDISHI wa habari. GT analishambulia Tanzania Daima. Naomba mwongozo, tujadili nini?
 
waandishi wao wenyewe hawana maadili, wanafanya mambo ya kifisadi na kihuni. wakifika kwenye makazi yao wanayaendeleza tu
 
Sawa. Hakuna waandishi wa habari TZ.

Lakini tujiulize, ni fani ipi hapa TZ ambayo inaweza kusimama kidete kudai ina mchango mkubwa kwa wananchi wa TZ.

Engineers ndio hao wanaoishia kujenga barabara/magorofa zisizo na viwango; Accountants ndio hao embezzlers na wanaosaidia wakwepaji kodi wakubwa; Doctors wanaopasua mguu kwa mgonjwa wa kichwa; Lecturers/Teachers wanaoendekeza maksi za chupi; Town Planners wanaogawa Plots moja kwa zaidi ya wamiliki wawili; Bankers wanaomtoza mfanyakazi riba ya 18% wakati ana guarantee ya mwajiri hivyo mkopo huo kuwa almost risk-free; Judges/Mahakimu wenye kutoa hukumu za utata. Kifupi ni kuwa fani zote hapa nchini zina watu wachache tu walio makini na fani zao. Big % ni wabangaizaji tu. Tusiishangae fani ya Journalism tu!
 
kituko cha TANZANIA DAIMA wikiendi hii:


Ok inawezekana ikawa mara moja ni bahati mbaya...lakini huyu mwandishi wa gazeti la Mbowe akakisha likaendelea kuonyesha ujinga na uvivu wa kufikiri na kufanya research kwa kudai hivi:






UKWELI WA NANI MWENYEKITI WA BODI YA NSSF HUU HAPA:


http://www.nssf.or.tz/board_of_trustees.php


Jamani tuache ushabiki halafu tuangalie hili gazeti FREEMAN MBOWE LINAVYOOAJIRI makanjanja



hivi huyu kweli ndio Dr MUSSA HASSAN au kajibadilisha?
b_nyoni.gif

Mrs. Blandina Nyoni
Board Chairperson
National Social Security Fund
Dar es salaam


hivi wanashindwa kuingia JAMII FORUMS kutafuta referencing kama KUBENEA na MWANAHALISI?

What a shame!

Tanzania Daima, Alhamisi, 7 septemba 2006

Nyoni Mwenyekiti Bodi NSSF

Na Jamal Zuberi, MAELEZO-Dodoma

RAIS Jakaya Kikwete amemteua Blandina Nyoni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk. Ladislaus Komba, Nyoni anachukua nafasi ya Mbunge wa Tabora Mjini, Siraju Kaboyonga Juma.

Taarifa hiyo imeeleza pia Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana amewateua wajumbe 11 wapya kwenye bodi hiyo.

Wajumbe hao ni Nicholaus Mbwanji (ATE), Ally Mwinyimvua (Benki Kuu) na Nicholas Kingazi (CRDB) ambao wanawakilisha waajiri, wakati Nestory Ngula (TUCTA), Boniface Nkakatisi (TUICO) na Adelgunda Mgaya (RAAWU) wanawakilisha Vyama Huru vya Wafanyakazi.

Wengine walioteuliwa kuiwakilisha serikali ni Dk. Mussa Assad (Kitivo cha Biashara na Uongozi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam), Ekingo Ekingo (Wizara ya Maliasili na Utali), Ezekiel Maige na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.

Bodi hiyo mpya itafanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Septemba mosi mwaka huu.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2006/9/7/habari35.php

Lakini hii si sehemu ya mjadala wa aliyeanzisha, turudi kwenye mada
 
GT
watakwambia wewe ni mnafiki na huwatakii mema ktk mafanikio ya kisiasa na kihabari,kwani wewe hujui kua Tanzania daima ndilo gazeti pekee ambalo halitumiwi na RA na siku zote linaandika ukweli mtupu.

Mkamap na mwenzio GT, munajikaanga kwa mafuta yenu. Hiyo mada ya huo waraka wa kina Mkapa na wenzake, ulijadiliwa kwa kina murudi na kuisoma vyema. Tukirudi kwenye mada husika kuhusu waandishi wa Tanzania, nadhani mukiwa munatenda haki, munaweza kurudi na kuangalia habari zote zilizoandikwa na Majira na Rai kwa wiki mbili zilizopita, mutaona ni aibu tupu. Angalia Majira habari walizoandika kuhusu Wangwe, utaona siku ya Press Conf ya Kina Lipumba waliandika stori na baada ya siku mbili wakarudia habari ile ile tena kwa uzito mkubwa, hapo sijui hao ndio wanaokusudiwa kuandika habari kwa kutumwa, au munazungumzia kina nani? Angalia Majira wanaandika wakimnukuu Paul Kyara, bila kuwaambia wasomaji Kyara ni nani na alitokea wapi kabla ya kuanzisha chama chake na kauli zote za Kyra zina mrengo gani!! Huo ndio mfano hai wa uchafu katika fani ya habari. Vinginevyo urudi nyuma na mifano hai ya jinsi, Sumaye, MWandosya, Malecela, Kitine, Kigoda, Dk. Salim na wengine wengi walivyoathiriwa vibaya na matumizi mabaya ya vyombo vya habari na walioshiriki kutunukiwa japo sasa wameonekana udhaifu wao na mifano ipo wazi. Vinginevyo musilete mjadala wa kujadili HEWA toeni mifano watu wajadili na kuona PUMBA na MCHELE ni upi
 
Mkamap na mwenzio GT, munajikaanga kwa mafuta yenu. Hiyo mada ya huo waraka wa kina Mkapa na wenzake, ulijadiliwa kwa kina murudi na kuisoma vyema. Tukirudi kwenye mada husika kuhusu waandishi wa Tanzania, nadhani mukiwa munatenda haki, munaweza kurudi na kuangalia habari zote zilizoandikwa na Majira na Rai kwa wiki mbili zilizopita, mutaona ni aibu tupu. Angalia Majira habari walizoandika kuhusu Wangwe, utaona siku ya Press Conf ya Kina Lipumba waliandika stori na baada ya siku mbili wakarudia habari ile ile tena kwa uzito mkubwa, hapo sijui hao ndio wanaokusudiwa kuandika habari kwa kutumwa, au munazungumzia kina nani? Angalia Majira wanaandika wakimnukuu Paul Kyara, bila kuwaambia wasomaji Kyara ni nani na alitokea wapi kabla ya kuanzisha chama chake na kauli zote za Kyra zina mrengo gani!! Huo ndio mfano hai wa uchafu katika fani ya habari. Vinginevyo urudi nyuma na mifano hai ya jinsi, Sumaye, MWandosya, Malecela, Kitine, Kigoda, Dk. Salim na wengine wengi walivyoathiriwa vibaya na matumizi mabaya ya vyombo vya habari na walioshiriki kutunukiwa japo sasa wameonekana udhaifu wao na mifano ipo wazi. Vinginevyo musilete mjadala wa kujadili HEWA toeni mifano watu wajadili na kuona PUMBA na MCHELE ni upi

Yeah u ryt,.......

Hey i didnt start this thread beacause i hate waandishi ila ni kwamba tunapokwenda ni pabaya. Mwaandishi ikiwa atakubali kutumiwa kuharibu na kuchafua jina kwasababu binafsi maanake tunakaribisha civil war!!! Jamani tuangalie!

Wana JF wengi ni wasomi (wanayajua kupambanua) kuna watu wanameza kila wanacho kiona kwenye gazeti! Tuandike habari inavyotakiwa, tusitie watu hamasa!...
 
JF,

Watanzania wengi wanapoamka asubuhi kwenda ofisini, kabla hawajaingia ofsini wanatupa macho yao kwenye vichwa vya habari vya magezeti!!!

Tukiangalia kwa kina tutaona kwamba waandishi wa habari wa Tanzania wananguvu kubwa sana. Yaani mpaka hatari! Waandishi wa habari wamekuwa wakimanipulate habari nyingi na tukizipindua wanavyotaka wao!..

Watanzania wanasoma sana magazeti. Na infact wanaamini sana magazeti!

Waandishi wetu wakobiased ile mbaya!...... Hawa hawa waandishi wanaotuandikia habari za viongozi mafisadi wao wenyewe wengi wao ni mafisadi na wanafanya kazi na hao (hidden) expert fisadis!...

Waandishi ama mass media ni chombo muhimu kwenye jamii!!! Jee tunakubali kutawaliwa na waandishi waongo,mafisadi na wanafki waliokosa uzelendo kazi kuchochea fitna na uhasama baina yetu?

Mimi ni mpenzi sana wa vyombo vya habari. Siku yangu bila kusoma gazeti au kuangalia TV, inakuwa haijapita sawasawa.
Lakini nachelea kukuunga mkono moja kwa moja kwa sababu umegeneralise.
Ni wkeli wapo waandishi wa aina unayoisema lakini si waandishi wote. wapo ambao wamejichanganua na wanatambulika kwa kazi zao. tatizo ni kuwa hata kwa hao, wanahukumiwa na misimamo ya wanaowasoma. Mtu huijudge habari kutokana na msimamo wake yeye na si ukweli au uongo uliopo katika habari hiyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom