mathcom
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,396
- 518
Wana jamii na wasomi waliobobea katika mambo ya siasa naomba tuujadili japo kwa ufupi huu mfumo wa "ujamaa na kujitegemea" ambao tunaambiwa na wanasiasa wetu na hata kuambiwa (kama si kufundishwa) mashuleni kwamba ndio unaofuatwa nchini Tanzania. Jee lengo la mfumo huu limefanikiwa kweli, na kwa ufanisi huo (kama upo) jee bado ni mfumo bora wa kuendelea kuwa nao nchini Tanzania??
Mimi mtazamo wangu nahisi wengi waliopata bahati ya kushika nafasi za juu serikalini au hata secta binafsi, wameacha kifungu cha kwanza na kuchagua cha pili yaani "kujitegemea" nikiwa na maana ya kwamba kila mtu kwa nafasi yake anajikusanyia mali kadri iwavyo ili aweze kujitegemea ama akiwa kazini na hata baada ya kustaafu, hili la "Ujamaa" nahisi kama halipo kabisaaa labda miongoni mwa masikini na fukara wao kwa wao!!
Naombeni mawazo mbadala au kwa muono wenu wajumbe,
ahsanteni!
Mimi mtazamo wangu nahisi wengi waliopata bahati ya kushika nafasi za juu serikalini au hata secta binafsi, wameacha kifungu cha kwanza na kuchagua cha pili yaani "kujitegemea" nikiwa na maana ya kwamba kila mtu kwa nafasi yake anajikusanyia mali kadri iwavyo ili aweze kujitegemea ama akiwa kazini na hata baada ya kustaafu, hili la "Ujamaa" nahisi kama halipo kabisaaa labda miongoni mwa masikini na fukara wao kwa wao!!
Naombeni mawazo mbadala au kwa muono wenu wajumbe,
ahsanteni!