Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu Machoni Tuu Kwa Uoga, Lakini Moyoni....

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,554
Wanabodi,

Hili ni swali tuu, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Lakini Moyoni Tunawadharau?.

Nikimaanisha inawezekana heshima tunayoionyesha kwa viongozi wetu sio genuine bali ni superficial tuu kutokana na nidhamu ya woga kwa kuwaogopa kufuatia nguvu ya kimamlaka waliyo nayo, lakini sio respect toka ndani na mioyoni mwetu?. Yaani tunawaheshimu machoni tuu lakini mioyoni tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia mazungumzo yangu na baadhi ya watu wengi huku mitaani madongo kuporomoka, wanawazungumzia vibaya baadhi ya viongozi wetu wa wakuu katika hali inayoashiria kuwa wanawadharau sana, sasa nilipokutana na mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kuwiwa kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!". Yaani heshima ni kitu kunachopatikana kwa kustahili na sio kulamisha.

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanawaheshimu kwa heshima za uongo za machoni tuu lakini moyoni mwao wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Kuna kitu kinaitwa 'mutual respect' ikimaanisha kwa kiswahili kuheshimiana

Rais Obama alikuwa anatumia maneno haya ''Treat people the way you want to be treated'
Kuna misemo ya kuongezea inayosema ' talk to people the way you want to be talked'

Na msemo mwingine ' Respect is earned not given'

Uzalendo ni tunu inayogusa kila mmoja katika jamii bila kujali nafasi yake.

Ndicho chombo kinachobeba umoja na utaifa. Uzalendo usitumike kama 'chaka' la kuwabagua wananchi, kwamba wapo wanaopaswa kusimamia uzalendo na wapo wanaopaswa kutumikia uzalendo

Mwananchi asiyemheshimu kiongozi aliyewekwa madarakani na wananchi hana sifa ya uzalendo
Equally, kiongozi asiyewaheshimu waliomweka madarakani hana uzalendo
Mkuu Nguruvi 3, kwanza naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, lazima kwanza wewe mwenyewe ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, ukiongea lazima uonyeshe respect kwa kuwaheshimu wale unaoongea nao, wale unaowaongoza, na kuonyesha heshima kwa watu wote, wakubwa na wadogo, watu wa chama chako na wapinzani, watu wanaokupenda na hata wasio kupenda, wewe ni kiongozi wa wote, timiza wajibu wako na majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio kila kitu hadi watu kukudhania unajidhania wewe ndio kama Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni tuu kwa sababu ya mamlaka yako lakini mioyoni mwao wanakudharau na kukuona ni mtu wa hovyo, mtu wa majisifu, mtu wa kujisikia, mtu wa kujiona wewe ndio wewe, sifa ambazo sio njema kwa mtumushi wa watu.

Kiongozi mzuri ni yule anayejiheshimu yeye na anayeheshimu watu anaowaongoza. Kama ni kiongozi wa kuchaguliwa, Rais, Mbunge, Diwani na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, hawa ni viongozi wa watu, lakini ni watumishi wa watu waliochaguliwa na watu ili wawaongoze, hivyo kwao watu muhimu kabisa ni wale waliowachagua. Kiongozi ukiishachaguliwa usijione wewe ndio wewe, kwa sababu uligombea wewe na ukashinda hivyo unajisikia ulishinda kwa nguvu zako! ,no way, huwezi kushinda kwa nguvu zako hata uwe ni bilionea kumpita Bill Gates, umeshinda kwa kura za waliokuchagua hivyo waheshimu hawa ili heshima hiyo ikurudie na wewe. Jihesabu huo uongozi wako sio malí yako bali ni malí ya waliokuchagua.

Kama ni kiongozi wa kuteuliwa, heshima mamlaka yako ya uteuzi ila heshimu pía wale unaowaongoza kwa kujihesabu kuwa cheo chako ni dhamana tuu kwa ajili ya hao unao waongoza. Hivyo waheshimu subjects wako ili nao wakugeshimu.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjitafakari, mnayoyafanya, mnayo yatenda, mnayo yasema, mjiulize, jee yana command respect?, heshima mnayoipata, inatokana na nyinyi kuistahili heshima hiyo? , do you earning such respect or night heshima tuu ya mamlaka?. Please badilikeni!, True respect is earned and not forced! .

Paskali
 
Nimetafakari historia ya sifa za viongozi tangu enzi na enzi kuanzia Adam, Mussa nk; nikatafakari hawa watu wasingekuwa na heshima na unyenyekevu na watu wao sjui kama tungekuwa tunawakumbuka vizazi na vizazi. Tafakuri tu
 
Pascal Mayalla

"Ninaposimama mimi, Mungu anakuwa amesimama"...kumaanisha mniheshimu kama mnavyoweza kumheshimu Mungu!!

Kwendeni huko na "mutual respect" zenu, wacha tunyooshe nchi kwanza.
 
Na ukishajua tabia ya mtu hakupi shida somtimes unaweza wala usiwe unamuogopa mtu ila sababu umeshamjua ni mtu wa tabia gani unaishi naye kijanja janja tu na kumpuuza ili mradi unajua unachopata hapo ulipo....
 
Wanabodi,

Hili ni swali tus, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Kutokana na Kuwaogopa kufuatia Nguvu ya Kimamlaka Waliyo Nayo, Lakini Ndani na Mioyoni Mwetu, Tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia kusoma mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!".

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanakeheshimu machoni tuu lakini moyoni wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Mkuu Nguruvi 3, naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, kwanza wewe mwenyewe kama kiongozi, lazima kwanza ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, onyesha respect kwa watu wote, timiza majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni kwa sababu wanakuopa lakini moyoni wanakudharau!.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjiulize, jee heshima mnayoipata, inatokana na earning it?. True respect is earned and not forced! .

Paskali
Viongozi watajibu.
Wacha mimi nijibu kama mtanzania tu.
RESPECT ni concept ambayo mtu au watu
hustahili HAKI/RIGHT ya kujiamulia mambo bila kusaidiwa KUFIKIRI.

Respect is a concept that ALL people (Not ONE) DESERVE the RIGHT to FULLY exercise their AUTONOMY.
Kama mtu HAPEWI FULLY autonomy na anakuwa micromanaged kwa kusaidiwa kufikiri, heshima itatoka wapi?
kinachofuata ni UOGA.
Na UOGA si heshima bali ni HOFU ya repercussions yaani hofu ya kuadhibiwa!
 
Wanabodi,

Hili ni swali tus, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Kutokana na Kuwaogopa kufuatia Nguvu ya Kimamlaka Waliyo Nayo, Lakini Ndani na Mioyoni Mwetu, Tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia kusoma mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!".

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanakeheshimu machoni tuu lakini moyoni wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Mkuu Nguruvi 3, naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, kwanza wewe mwenyewe kama kiongozi, lazima kwanza ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, onyesha respect kwa watu wote, timiza majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni kwa sababu wanakuopa lakini moyoni wanakudharau!.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjiulize, jee heshima mnayoipata, inatokana na earning it?. True respect is earned and not forced! .

Paskali
Huu uzi una shari ndani yake. "Mayala" kwetu ina maana ya njaa, naona una njaa ya kuhojiwa.
 
Wanabodi,

Hili ni swali tus, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Kutokana na Kuwaogopa kufuatia Nguvu ya Kimamlaka Waliyo Nayo, Lakini Ndani na Mioyoni Mwetu, Tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia kusoma mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!".

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanakeheshimu machoni tuu lakini moyoni wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Mkuu Nguruvi 3, naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, kwanza wewe mwenyewe kama kiongozi, lazima kwanza ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, onyesha respect kwa watu wote, timiza majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni kwa sababu wanakuopa lakini moyoni wanakudharau!.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjiulize, jee heshima mnayoipata, inatokana na earning it?. True respect is earned and not forced! .

Paskali
Huyu mkulu wetu anataka akikosea ukiri wewe kuwa ndiye uliyekosea na akutumbue ndiyo furaha yake, heshima huja kwa kuifanyia kazi sio zawadi
 
Wanabodi,

Hili ni swali tus, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Kutokana na Kuwaogopa kufuatia Nguvu ya Kimamlaka Waliyo Nayo, Lakini Ndani na Mioyoni Mwetu, Tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia kusoma mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!".

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanakeheshimu machoni tuu lakini moyoni wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Mkuu Nguruvi 3, naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, kwanza wewe mwenyewe kama kiongozi, lazima kwanza ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, onyesha respect kwa watu wote, timiza majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni kwa sababu wanakuopa lakini moyoni wanakudharau!.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjiulize, jee heshima mnayoipata, inatokana na earning it?. True respect is earned and not forced! .

Paskali
Usihangaike Paskali hao viongozi hawaheshimiwi wala hawaogopwi bali tunawakalia kimya tukisubiri muda uleee! Tuwaogope kwani sisi tunataka uDc?
Na biashara yangu hii ya njugu nimwogope nani zaidi ya Mungu na njaa yangu?
 
Paskali umenikumbusha maisha ya kule Jeshini kwa mujibu wa sheria. Tumemaliza kidato cha sita na kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu ilikuwa lazima ulitumikie Jeshi la Kujenga Taifa mwaka mmoja. Maafande wetu wakufunzi karibu wote walikuwa wameishia darasa la saba. Walikuwa wanatutukana kwa kuwa sisi tumesoma zaidi yao na kutupigisha fangfang la kisawasawa! Afande anasema, Kuruta 'njoo hapa!' Piga Pushup ishirini chapchap! Ukimaliza, 'wekamikono kichwani, ruka kichura' Pigamagoti sema 'mimi mjinga'!!!! Unafanya hayo si kwa kuwa ni ya kweli ama unayaamini, lakini kwa mujibu wa sheria. Siku moja Afande akamsulubu rafiki yangu eti kwa nini yeye ni mrefu kuliko afande!! Mioyoni tulikuwa tunawadharau sana. Walikuwa kama katuni fulani au maroboti fulani vile! Lakini kwa nje,.............. du!
 
Paskali umenikumbusha maisha ya kule Jeshini kwa mujibu wa sheria. Tumemaliza kidato cha sita na kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu ilikuwa lazima ulitumikie Jeshi la Kujenga Taifa mwaka mmoja. Maafande wetu wakufunzi karibu wote walikuwa wameishia darasa la saba. Walikuwa wanatutukana kwa kuwa sisi tumesoma zaidi yao na kutupigisha fangfang la kisawasawa! Afande anasema, Kuruta 'njoo hapa!' Piga Pushup ishirini chapchap! Ukimaliza, 'wekamikono kichwani, ruka kichura' Pigamagoti sema 'mimi mjinga'!!!! Unafanya hayo si kwa kuwa ni ya kweli ama unayaamini, lakini kwa mujibu wa sheria. Siku moja Afande akamsulubu rafiki yangu eti kwa nini yeye ni mrefu kuliko afande!! Mioyoni tulikuwa tunawadharau sana. Walikuwa kama katuni fulani au maroboti fulani vile! Lakini kwa nje,.............. du!
umenikumbusha mbali sana ... " wee ulievaa green vest ya kijani kijani kujaa hapa". "wenye green vest za njano mbeleee tembea"
 
Awamu Hii Tutashuhudia Wimbi Kubwa Sana La Watabiri Na Wazee Wa Falsafa
 
Baba wa Taifa huyu aliheshimika sana na Watanzania wengi na anaendelea kuheshimika kutokana na sababu mbali mbali kabla ya kuwa kiongozi wa nchi, alipokuwa kiongozi wa nchi na baada ya kung'atuka madarakani.

Wanabodi,

Hili ni swali tus, "Jee Kuna Uwezekano Viongozi Wetu Tunawaheshimu kwa Machoni Tuu Kutokana na Kuwaogopa kufuatia Nguvu ya Kimamlaka Waliyo Nayo, Lakini Ndani na Mioyoni Mwetu, Tunawadharau?!.

Swali hili limefuatia kusoma mchango wa mwana JF mmoja ambao ni mmoja wa GT wachache wa ukweli humu JF, akichangia uzi fulani humu, amesema maneno mazito kwenye mchango wake ambayo yamenigusa na kupelekea kupandisha bandiko hili.

Hoja ya msingi ya mwanajf huyu ni kuhusu heshima, yaani "respect is earned and not forced!".

Hivyo kufuatia tabia binafsi za baadhi ya viongozi wetu, inawezekana kabisa watu wanakeheshimu machoni tuu lakini moyoni wanawadharau?, yaani respect iliyopo ni nidhamu ya woga tuu? .
Mkuu Nguruvi 3, naunga mkono hoja, respect is earned and not forced, ili kiongozi uweze kuheshimika, kwanza wewe mwenyewe kama kiongozi, lazima kwanza ujiheshimu, na kuwaheshimu wengine ili ile heshima ikurudie na wewe! .

Kujiheshimu huku kwa kiongozi ni lazima uongee kwa heshima na unyenyekevu, onyesha respect kwa watu wote, timiza majukumu yako ya kiuongozi kwa weledi wa hali ya juu huku ukiheshimu katiba na ukifuata sheria, taratibu na kanuni.

Ukionyesha dharau, majigambo, kujisikia wewe ndio wewe, wewe ndio Alfa na Omega, watu watakeheshimu machoni kwa sababu wanakuopa lakini moyoni wanakudharau!.

Namalizia kwa kukumbushia swali la msingi, jee tunawaheshimu viongozi wetu kwa dhati au tunawaheshimu kwa uoga tuu?.

Na kwenu viongozi, naomba mjiulize, jee heshima mnayoipata, inatokana na earning it?. True respect is earned and not forced! .

Paskali
 
Back
Top Bottom