Jee Kuna Posibility ya Plagiarism Kwenye Taarifa za Madini?. Taarifa Zitolewe for Public Scrutiny.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,574
Wanabodi

Tangu kutolewa kwa Taarifa zote mbili za kamati za madini zimekuwa zikipata uungwaji mkono mkubwa kutoka kwenye lakini pia kuna baadhi ya criticism.

Kwa vile hizi taarifa zote mbili ni public documents, kwa nini mpaka sasa bado hazijawekwa wazi zaidi ya kusomwa tuu mbele ya public wakati wa kukabidhiwa kwa rais.

Nimesoma mahali kauli hii kuhusu Taarifa ya pili ya madini ya Prof. Nehemia Osoro

"Sijazungumzia bado plagiarism ya taarifa mbali mbali za kiserikali na zisizo za kiserikali katika Taarifa ya Kamati ya Prof. Osoro. Hili nitalisema baadae baada ya kupata soft copy ya Taarifa hiyo"

Jee inawezekana kweli kwa Taarifa hii kuwa na plagiarism?, au ni makuwadi wa mafisadi wanataka kumchafua Prof. wetu baada ya kufanya kazi nzuri?.

Maadam Taarifa zote mbili zilisomwa mbele ya rais na kukabidhiwa rasmi, hii maana yake they are (both) public documents.

Kwa nini mpaka sasa Taarifa hizi mpaka sasa bado hazijawekwa wazi for public scrutiny ili ama zifanyiwe public appraisers za pros na cons zake or wenye uwezo wazifanyie critique ?.

Kwa kawaida professional presentations zinakuwa appraised na wasomi wa calibre hiyo kwa hoja za kisomi, hivyo inapotokea tuhuma za msomi wa level ya Prof. tena anayeheshimika kama Prof. Osoro halafu akaibuka mtu kusema kuna plagiarism! , that is very serious allegations!.

Ili kuwatendea haki Watanzania na kulinda heshima za wasomi walioandika taarifa hizo, natoa wito taarifa hizo ziwekwe wazi hadharani ziwe subjected to public scrutiny ili wenye hoja pinzani ku criticise taarifa hizo walete hoja zao tuzichambue na sio ku dismisses taarifa za kisomi kwa hoja nyepesi.

Jee unaungana nami, kuwa now it's high time, taarifa hizi sasa zitolewe rasmi in public ili wachambuzi wetu wawe huru kutuchambulia kisomi?

Paskali
 
Kwanza kuna tuhuma kwamba hao watuhumiwa wachimba madini hadi sasa hawajakabidhiwa ripoti ya awamu ya kwanza, kitu ambacho wanalalamika imewawia ugumu kujibu tuhuma dhidi yao au kuchukua hatua zozote.

Pili, ule ni utafiti, nilimsikia Prof akisema only in Tanzania, am shocked sijui pesa ingejenga SGR au ingefanya hivi au vile.

Wao walitakiwa walete facts, findings kazi ya kuchambua na kutoa maoni watuachie. Hiyo haikuwa miongoni mwa hadidu rejea. Tayari kulikuwa na dalili za ripoti inayoonyesha uegemeo wa upande mmoja.
 
Back
Top Bottom