Je Zitto Amepoteza Uhalali wa kuwa Kiongozi?

Eric Ongara

Senior Member
Sep 19, 2006
165
8
Wengi wamepongeza baadhi kuhoji na kubeza uamuzi wa Zitto kugombea. Na badae wamebeza uamuzi wa Zitto kujitoa sambamba na kushangazwa na ushauri wa kamati ya wazee waliomshauri Zitto ajitoe katika kinyanganyiro cha uenyekiti wa taifa dhidi ya mwenyekiti wa sasa Freeman Aikael Mbowe( Mtuhuru).

Sikubaliani na waliompinga Zitto kwa msukumo wa mazoea na kukumbatia ukiritimba. Ushindani ni hitaji muhimu katika ustawi wa chama. Ni kweli Zitto alikuwa na haki ya kugombea na anakidhi vigezo vya jumla vya kugombea. Kinachogomba ni wajibu aliojaribu kuupuza wakati anafanya maamuzi ya kugombea. Lazima tukumbuke haki huambatana na wajibu.

Zitto anafahamu kwa sasa CHADEMA haina anasa ya kuchagua kati yake na mtuhuru. Pamoja na ukuaji unaovutia kwa nje,CHADEMA bado haina watu wenye mitaji mikubwa ya kisiasa.Inawahitaji wote(Mtuhurum,slaa na Zitto) kwa pamoja katika timu moja ya kiuongozi.Jaribio lolote la kulazimisha wanachama wachague kati ya mtuhuru,Zitto au slaa ni fikra muhali za kihuni ambazo zinaweza kukijeruhi chama.

Zitto alipaswa kutekeleza vyema wajibu wake kwa kutafakari.Pengine hakujipa mda wa kutosha kutafakari kwani alikamilisha maamuzi yake akiwa uwanja wa ndege. Wengi wanoasukumwa na nadharia zaidi ya uhalisia, walitaka Zitto ashindanishwe na mtuhuru kama kielelezo cha kukidhi matakwa(na sio mahitaji) ya demokrasia kwa tafsiri na matamanio yao.

CHADEMA ina wafuasi wengi lakini ni wachache waliojitokeza mbele katika siasa za moja kwa moja.Hivyo CHADEMA inahitaji majabali haya machache kuendelea kuwemo katika safu moja ili kukiandaa chama kwa ajili ya uchaguzi mkuu.Tayari kulikuwa na wazo la kutumia "utatu mtakatifu" yaani Mtuhuru,Slaa na Zitto katika kuipasua na kiitesa CCM katika uchaguzi mkuu wa mwakani na hatiame kukiandaa vyema chama na mwaka wa “mavuno” mwaka 2015.

Zitto alikuwa ana wajibu wa kutafakari namna ambavyo "haki" yake ya kugombea ingesababisha mnyukano ambao ungeibua athari za muda mrefu kwa chama na wagombea. Hatuwezi kuhujumu demokrasia ndogo kwenda kuathiri demokrasia Pana.Hatuwezi kutetea udhofishaji wa CHADEMA Kwa kiisngizio cha demokrasia na kwa wakati huo tukiua demokrasia pana yani ushindani wa CCM na CHADEMA.

Kugombea kwa Zitto kungefaidisha zaidi CCM zaidi ambavyo ingefaidisha CHADEMA. Kama CCM wangeombwa ushauri basi wangesisitiza Mtuhuru na Zitto washindane. Hivyo uamuzi wa awali wa Zitto kugombea ulikuwa tayari una manufaa kwa wapinzani wa CHADEMA Hususani CCM.

Inalekea kulikuwa na makundi ya muda mrefu ambayo Zitto anayafahamu kwa mujibu wa maandiko yake hapa, na pengine ndio msukumo wake kugombea. Kama ndivyo,Zitto amepwaya kiungozi kwa kuamua kugombea kwa msukumo wa kukuza na kumaliza kundi jingine.Umbea, majungu na husda haviwezi kamwe kufaulu kama kichocheo cha kuwa mwenyekiti wa chama kitaifa.

Zitto anaelewa kanuni, mazoea na taratibu za uendeshaji wa chaguzi zake za ndani. Kama alikuwa na nia njema alipaswa kuwa ameepika michakato hii ili isije ikadhuru nia yake ya kugombea na pengine kuwa na athari hasi kwa taathira ya chama kwa ujumla wake. Uzembe wake katika kutathmini hili ni hujuma za wazi dhidi ya haki yake kama mgombea na ustawi wa chama kwa ujumla wake. Ushauri uliotolewa na kamati ya wazee wa chama ni jambo ambalo Zitto alipaswa kuling’amua hata kabla.Pengine lengo lilikuwa kukivua nguoa chama au kuwashwa na msisimko wa ndani.

Ipo changamoto ya chama ya kuwa na utegemezi usio wa kwaida kwa mtuhuru, slaa na Zitto kutokana na mitaji yao mikubwa ya kisiasa. CHADEMA inao watu wengi wenye weledi wanaoweza kutoa mchango mkubwa katika medani ya siasa, hivyo kunapaswa kuwa na mkakati kambambe wa kuzalisha na kutambulisha kwa umma wanasiasa wengi zaidi.”Utatu mtakatifu “uliapaswa kuwa nyenzo ya kutengeneza mabingwa wapya. Zitto kwa uzembe au kiburi aliamua kupuuza hali halisi ya chama na kuamua liwalo na liwe! Suluhisho lake la mvutano wa ndani lilikuwa ni kusambaratisha wapinzani wake wa ndani na pengine kukisambaratisha kabisa chama kwa ujumla wake.


Maandiko ya Zitto kama majibu ya Tuhuma dhidi zake JF
Hakuna maelezo yoyote yanaoweza kuhalalisha ujinga wa Zitto alioufanya hapa. Kwa maelezo yake amethubitisha maamuzi ya wazee yalikuwa ni sahii juu yake. Ni utovu wa nidhamu usio na kikomo na ni ishara ya kutokuwa na mapenzi yoyote na chama anachokiongoza.

Utetezi kuwa yeye ni binadamu ana nyama na kuwa anaudhika kama binadamu ni upumbavu. Ni sawa na mlevi anaebaka kwa kisingizo cha msukumo wa pombe, kwanini hakuna msukumo wa mlevi mwanaume kulazimisha kulatiwa? Kwa nini bado kuna uangalifu wa kuchagua vitendo?

Ikiwa wabaya wake ni John Mrema na John Mnyika, kwanini ameamua kugombana na chama kizima? Uchaguzi wake makini wa maeneo ya kugusa katika majibu yake ni kielelezo cha mpangalio uliojaa uovu, fikra duni na nia mbaya, mathalan maelezo yanayoibua hisia kama suala la marehemu wangwe ni kielelezo halisi kuwa Zitto ana nia mbaya na CHADEMA. Huwezi kujisaidia katika kisima ambacho unatumia kwa maji ya kunywa na kupikia kisa umekasirishwa na mwanakijiji mmoja.

Ikiwa ni kweli Mrema na Mnyika wamemtuhumu Zitto ni kwa nini kama kama kiongozi ameshindwa kutumia miundo ya chama kutataua? Na mbona amekishambulia chama kwa ujumla wake? Amekihusisha chama na uchaga( ni sawa na kuthibitisha propaganda za CCM au kuunga Mkono msimamo,mkakati na mtazamo wa CCM dhidi ya CHADEMA), maauji na matumizi mabaya ya fedha. Hizi sio tuhuma za kwa watu binafsi! Inaelekea anaowalenga wana mapenzi makubwa kwa chama zaidi yake, hivyo kete yake yeye ni kwa kuumiza kile kinachopendwa na hao maadui zake wa “kubuni”.

Ni kama anatuambia yeye haipendi CHADEMA kihivyo! wakiendelea kumgusa ataua chama! Huu ni ubakaji wa chama na kuibua hofu za kibazazi. Ni kama anawaambia wanaCHADEMA wasimuuzi lasivyo atanyea kisima?! Hatuwezi kuendesha chama kwa hofu na kuwaza ni lini Zitto atakunya katika kisima. Kuna maswala mengi ya kuwaza katika mustakabali wa nchi zaidi ya kunya kwa Zitto.

Kwa makusudi Zitto ameamua kupotosha suala la BAVICHA. Ushindi wa kafulila anauzungumzia anaujaje?. Nilibahatika kushuhudia uchagauzi ule, matokeo hayakutangazwa kutokana na idadi za kura kuzidi idadi ya wapiga kura. Hali ilivyoanza kuwa tete Zitto alitoa kauli tata kuwa vijana leo watatupiana ngumi na kutokomea, yeye kama kiongozi wa kitaifa anaamua kukimbia hali ile ulikuwa ni udhaifu mwingine mkubwa wa kiungozi wa Zitto.

Msiamazi baada ya kutangaza hali halisi ya zoezi la kura, aliwaapa wajumbe nafasi ya kutoa maoni yao ambao wengi walimtuhumu moja kwa moja Zitto pasipo kutafuna maneno kuwa alishiriki kuhujumu uchaguzi ule. Kipindi hicho sio Zitto wale Kafulila waliokuwepo, wagombea wengine walikuwepo na kuzunguma, hatukumsikia hata wakala wa kafulila akilalamikia kudhulumiwa. Ni aibu kwa Zitto kufanya jitihada za kuhalalisha uhuni ule. Ikiwa alibainie jitihada za hujuma dhidi ya Kafulila ni kwanini hakuziwasilisha katika kikao cha jumapili cha kamati kuu?

Kuhoji kamati ya wazee chini ya Mtei kuendelea kusimamia uchaguzi zinaozendelea wakati tayari baraza la wazee limechagua viongozi wake ni kielelezo cha kukosa uwajibikaji wa pamoja. Yeye kama kiongozi hakushiriki katika kuandaa ratiba na mchakato mzima wa uchaguzi? Kwanini anajitenga? Inaelekea Zitto amepoteza Imani na chama chake au amejifungua imani mpya.

Baada ya kikao cha kamati kuu jumapili iliyopita umma ulielezwa kuwa tofauti kati ya Zitto na Mtuhuru zimefutwa. Sasa hapa Zitto anaposema siku wakipatana na Mtuhuru wapambe nuksi watakoma anataka kusema nini? Kwamba walituzuga? Walifanya unafiki?

Kimsingi Zitto amepoteza uhalali wa kuwa kiongozi. Mtuhuru ameandamwa sana na kuandikwa mno lakini hajawai payuka nama hii kwa kisingizo kuwa na yeye ana nyama! Kiongozi lazima uwe na moyo mkubwa. Zitto angekuwa Mwenyekiti (Mungu katuepuesha) angekuwa ndio mlengwa mkuu wa tuhuma toka kwa washindani wake, angetupeleka wapi na mihemko ya aina hii ya kisiasa? Na je ni kwanini amekuwa mkali sana kwenye tuhuma hizi na sio wakati wa Dowans au ule wa mahusiano? Je kuna msukumo wowote wa hatia? Zitto anapaswa kutafakari kwa kina kwa nini nembo/Bango(Brand) yake/lake ya kisiasa imekuwa dhaifu kiasi cha kubeba tuhuma kirahisi hivi na hatime baadhi ya watu kukaribia kuziamini ikiwemo yeye mwenyewe kiasi cha kuweweseka namna hii?

Jitihada za Kuiua CHADEMA ni jambo lisilovumilika kwa hali yoyote ile.Ni ushenzi na laana iliyo kuu. Naami hili ni jaribio la mwisho la CHADEMA kudhihirisha ukomavu wake wa kisiasa na kuwarejeshea matumaini watanzania. Upuuzi na udhaifu wa Zitto unaweza kusahihishwa.
 
Last edited by a moderator:
Zitto alianza hii safari pale alipokubali kujiunga na kamati ya madini ya Kikwete (bila kujadiliana na viongozi wenzake ndani ya chama) na hivyo kuondoa momentum ambayo wapinzani walikuwa wameipata baada ya kuibua skandali ya Buzwagi.

Watu wengi walimpinga hapa na kumuomba abadili mawazo lakini yeye akawakatalia kata kata kwa kudai kuwa anajua anachokifanya. Matokeo yake yanajulikana - suala la Buzwagi na migodi ya madini liliishia kwa mkulu Sinclair na mafisadi wenzake.

Baada ya hapo - na baada ya kupata pesa kibao kwenye kamati na tume za Kikwete - Zitto alibadilika sana kimtizamo na kiutendaji. Haikunishangaza pale alipoanza kuunga mkono mafisadi kuhusu ununuzi wa Dowans.

Zitto wa leo sio yule ambayo wazee wa CHADEMA walimpa issue ya Buzwagi ili ajijenge kisiasa. Ukaribu wa Zitto na Kikwete ni mkubwa sana kiasi cha kufunika juhudi binafsi ndani ya chadema kama chama chenye mpango wa kuingoa serikali ya Kikwete.

Safari ya Zitto kujiunga na Kikwete ilianza pale alipokubali uteuzi kwenye kamati ya madini. Yaliyobaki ni historia.
 
Ndugu yangu Eric Ongara,

Umechambua vema kabisa hali halisi inayoendelea CHADEMA, lakini nakuomba ukomee hapo maana nionavyo unaipenda CHADEMA kama nilivyo mimi. Uloyasema ni kweli lakini ukiendelea utakuwa sawa na "kuchafua kisima".

Tunaihitaji CHADEMA na pia CCM inaihitaji CHADEMA. Watu wema ndani ya CCM wametuambia kuwa kukua kwa CHADEMA ni salama kwao na hasa ndani maana siku hizi hawatishani kama zamani kwa hofu kuwa mtu akitishwa ataenda CHADEMA. Ili CCM ipone inahitaji CHADEMA yenye nguvu na mshikamano. Naamani Zitto amejifunza na hatarudia tena.
 
RAIA MWEMA ya leo:

NILIIPOKEA vizuri taarifa ya uamuzi wa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe (Mb) kuchukua fomu ya kugombea uenyekiti wa chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika leo Jumtano.

Nilimwuunga mkono Zitto kwa moyo wangu wote, kumpongeza, na kumwombea dua apambane vyema na Mwenyekiti wa sasa, Freeman Mbowe katika kinyang'anyilo hicho. Najua si mimi peke yangu, bali na Watanzania wengine kadhaa walifurahia uamuzi huo adimu wa Zitto; ingawa wapo pia waliouona kama usio sawa sawa.

Binafsi nilimuunga mkono Zitto kwa sababu kuu nne. Kwanza, nilijua kwamba uamuzi wake ungeleta msisimko mkubwa katika siasa za Tanzania kwa mwaka huu, msisimko wenye mwelekeo tofauti na msisimko wa muda mrefu katika siasa za Tanzania kwa kipindi cha miaka miwili sasa.
 
RAIA MWEMA ya leo:

NILIIPOKEA vizuri taarifa ya uamuzi wa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe (Mb) kuchukua fomu ya kugombea uenyekiti wa chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika leo Jumtano.

.....!

Ukisikia flooding basi ndiyo hii. Unabandika kitu kwenye thread mbili tofauti (wakati kitu hicho tayari kina thread inayojitegemea).

Umeishiwa hoja nini?!
 
Lakini uamuzi wowote wa kilegelege kama huu wa ‘ushauri wa wazee' unawaponda wengi mioyo na kuwakatisha tamaa. Uamuzi wa ‘ushauri wa wazee' aliochukua Zitto umetia doa rekodi ya demokrasia ya CHADEMA.


- Ngoja tujaribu kuchambua hoja nzito za hii ishu, naona hapa Raia Mwema wamejaribu kutusaidia na hoja zaidi.

Respect.

FMEs!
 
- Ngoja tujaribu kuchambua hoja nzito za hii ishu, naona hapa Raia Mwema wamejaribu kutusaidia na hoja zaidi.

Respect.

FMEs!

We Field Marshal
Mbona tena unataka kutuvuruga? Thread hii umeituma mara mbili, na zaidi unaonekana kushabikia anguko la CHADEMA wakati mimi nakuaminia kwa kuwa objective. Usinitie majaribuni kuacha kukuheshimu.
 
Eric baba, hayo mawazo yako wala usifikiri kila mtu anawaza kama wewe!

Kwangu mimi Zito mpiganaji na kiongozi mzuri, andika weeeeeeeee jaza hata thread zote kwangu mimi ni hivyo hiyo haitabadilika; sijamjua leo wala jana!

Pili, weka dhamana au insuarance kuwa wengine woote wapiganaji hawawezi kuhudhiwa na kubadilika; ama sivyo kutakuwa hakuna mpiganaji !

swala la kuwa huyu jamaa atakufa kisiasa pia ni theory is not practical, na wote wanaosema hivyo ni kujaribu kutabiri kama akina Yahaya!

Tukiwa wakali kuwalinda wale wapiganaji wetu tutawaokoa wengi, tukiwa waandika nakala kama wewe tutaua wengi mwishowe utabaki wewe peke yako maana wooote watachukuliwa na upepo.

Uwazi wa Zito ni mzuri ndugu , ni picha tunapata kuwa ni jinsi gani vyama vinavyojiita mbadala vinaishi, Zito angekuwa wa kujikomba angekaa kimya!

KWA NAKALA YAKO UNAPROVE PIA KUWA ZITO YUKO JUU SANA ZAIDI YA CHADEMA, CCM huwa hawafanyi ujinga huu, angekuwa mdogo; why all this unconvicing articles!

Mwambie Mtei na Chadema wote kuwa habari zenu tumezipata na mnavyoishi humo, hamna tofauti na CUF, NCCR, TLP.

Shida ilikuwa nini si angeachwa ashindwe kwenye kibox cha kura, wewe hili hufikirii??

swali la kumalizia, tunawalindaje hawa wapiganaji?? maana juzi tu ulikuwa unampenda Zito , leo humtaki, kesho utamkacha Slaa, maana tuhuma zipo tu, na tusivyopenda vithibitisho!

why are we not believing in them, when then we will belive them as true dream leaders??

Mtu gani mkweli atakayeingia kwenye siasa na kuishi namna hii??

ETI KULINDA CHAMA THIS IS POPPYCOCK !!!, AKILINDE KISHA WAJE KUCHUKUA NCHI, SI KAMA YA KENYA YA KUMUONDOA MOI, THEN WAO HAWATAKI KUTOKA, THUBUTU !!! better this what is CHADEMA ANYWAY , mjinga sana wewe!!

Upumbavu huu anaouvumbua Zitto badala ya kufurahia ndio mnasema kulinda chama, TOFAUTI YA HII NA CCM ni nini then

Kwa wataka mabadiliko tusio na makundi this was good movies, kuona kumbe hakuna cha CHADEMA wala CCM, wala CUF , TLP, NCCR, we are long way to true revolution, lets think another way!

ETI KULINDA CHAMA!!! huu ujinga hausameheki, NDIO MNAISHI NA WANAWAKE WAZINZI ETI KULINDA NDOA!

mchaga nini wewe!!!!!!!!!!
 
Swali kwa Eric, au nikimgusa mchaga mmoja ndio nimegusa wooote, siku hizi wachaga kama waarabu. hata CUF na kanzu zao hawako hivi!

Ukileta chuki za kikabila hapa utajibiwa na yeyote yule hapa JF. Kama ulikuwa na swali binafsi kwa Eric ungetumia kitu inaitwa PM. Hizo chuki zako za kikabila zipeleke huko kwenu mkuu.
 
Eric...ina maana wajumbe wa Chadema ni wajinga?..au wana akili za Kushikiwa? kiasi ambacho wanashindwa kutofautisha Mchango wa Zitto na Mchango wa Mbowe ktk Chadema?...!!!

Kwa Jinsi mnavyomtetea Mbowe kiasi Hiki...kama hawezi kusimama na Zitto ktk Uchaguzi wa Ndani, Je anaweza simama na Mgombea wa CCM ktk Kuchukua Mamlaka Makubwa ya Nchi...?
 
Eric...ina maana wajumbe wa Chadema ni wajinga?..au wana akili za Kushikiwa? kiasi ambacho wanashindwa kutofautisha Mchango wa Zitto na Mchango wa Mbowe ktk Chadema?...!!!

Kwa Jinsi mnavyomtetea Mbowe kiasi Hiki...kama hawezi kusimama na Zitto ktk Uchaguzi wa Ndani, Je anaweza simama na Mgombea wa CCM ktk Kuchukua Mamlaka Makubwa ya Nchi...?

Wewe maoni yako ni yapi?
 


Tukiwa wakali kuwalinda wale wapiganaji wetu tutawaokoa wengi, tukiwa waandika nakala kama wewe tutaua wengi mwishowe utabaki wewe peke yako maana wooote watachukuliwa na upepo.

Uwazi wa Zito ni mzuri ndugu , ni picha tunapata kuwa ni jinsi gani vyama vinavyojiita mbadala vinaishi, Zito angekuwa wa kujikomba angekaa kimya!

KWA NAKALA YAKO UNAPROVE PIA KUWA ZITO YUKO JUU SANA ZAIDI YA CHADEMA, CCM huwa hawafanyi ujinga huu, angekuwa mdogo; why all this unconvicing articles!

Mwambie Mtei na Chadema wote kuwa habari zenu tumezipata na mnavyoishi humo, hamna tofauti na CUF, NCCR, TLP.

Shida ilikuwa nini si angeachwa ashindwe kwenye kibox cha kura, wewe hili hufikirii??

swali la kumalizia, tunawalindaje hawa wapiganaji?? maana juzi tu ulikuwa unampenda Zito , leo humtaki, kesho utamkacha Slaa, maana tuhuma zipo tu, na tusivyopenda vithibitisho!

why are we not believing in them, when then we will belive them as true dream leaders??

Mtu gani mkweli atakayeingia kwenye siasa na kuishi namna hii??

ETI KULINDA CHAMA THIS IS POPPYCOCK !!!, AKILINDE KISHA WAJE KUCHUKUA NCHI, SI KAMA YA KENYA YA KUMUONDOA MOI, THEN WAO HAWATAKI KUTOKA, THUBUTU !!! better this what is CHADEMA ANYWAY , mjinga sana wewe!!

Upumbavu huu anaouvumbua Zitto badala ya kufurahia ndio mnasema kulinda chama, TOFAUTI YA HII NA CCM ni nini then

Kwa wataka mabadiliko tusio na makundi this was good movies, kuona kumbe hakuna cha CHADEMA wala CCM, wala CUF , TLP, NCCR, we are long way to true revolution, lets think another way!

ETI KULINDA CHAMA!!! huu ujinga hausameheki, NDIO MNAISHI NA WANAWAKE WAZINZI ETI KULINDA NDOA!

mchaga nini wewe!!!!!!!!!!

Waberoya mkuu, i always respect you na kweli leo umekasirika!! punguza kidogo tu jazba mkuu...

You have said it all na its better that you have given this other side of the story; kama ukichunguza sana hizi threads za Zitto, zinaonyesha wazi kwamba hakuna utaifa, ila kuna itikadi za kichama na ku-confirm kwamba siasa huku kwetu ni biashara...

Nilimwuliza Kibanda, haoni kwamba wanaji-expose na kuwa kama wale watu wanaooga kando ya barabara?? na ukienda ndani zaidi utakuta wooooote wako hivyohivyo!!! Yaani siasa za bongo zimekuwa kama mashindano ya kuvuana nguo chamani, yet they all claim kwamba wanaipenda nchi!!!!

Its a high time we have wagombea huru ili kuondoa hizi collectivity zisizo na tija!!!!!!!!!!! Zitto is young, ambitious etc. so is Mnyika ... and so is Kitila, and you can clearly read that they may not forma a great team because of their vogor and ambitions!!! this is for all politicians in this country expecially young gees!!!

Jana tumeona na youth wing yenu inavyolumbana kama tofali la barafu kwenye fence!!!

Yamekuwa kama mashindano ya kuwekana uchi humu jamvini jamani CHADEMA, just one of you call for truce and you go bakc and dress yourself

The bottom line, dont let your dirty laundry destroy you [both Zitto and the rest of CHADEMA]
 
Swali kwa Eric, au nikimgusa mchaga mmoja ndio nimegusa wooote, siku hizi wachaga kama waarabu. hata CUF na kanzu zao hawako hivi!

Just delete that "mchagga thing" inatugawa na haina mantiki katika undugu wetu wa kitaifa!!
 
hii inatisha sasa hivi.

Utadhani kama wachaga hawatakiwi kusema au kufanya chochote Tanzania!


....kuna juhudi ya dhati ya kubagua section ya watanzania..huu ni ubaguzi...wewe fikiria imefikia mahali watu wanaoogopa vivuli ..viongozi wakubwa kabisa wamefikia mahali ..wanapita baadhi ya maeneo hasa ya pwani wakiwahuburia wazee wao wasiwauzie watanzania wenzao ardhi au tuseme kuzuia kuwakaribisha....kinyume cha katiba ya nchi waliyoapa kuilinda inayosema kuwa watanzania wana freedom of movement....chuki hii inaazia juu....hawa ni wafuasi tu kwa kile kilichojificha kwa wanaowatuma...kwa kujuwa au kutojuwa!!
 
Back
Top Bottom