GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,002
- 107,344
Kuna Mmoja wa hao ‘ Maprofesa ‘ ndani ya hilo Jopo lao ( sasa Naibu Waziri wa Wizara ambayo nimeisahau kwa sasa ila nikiikumbuka nitaitaja ) nakumbuka baada tu ya Kufanikiwa ‘ Kuikomboa ‘ Kisheria Mbung’o / Ndege yetu huko kwa Waafrika Wenzetu Afrika Kusini alipohojiwa alikuwa akiongea kwa Mikogo yote huku ‘ akijimwambafai ‘ kwa kusema kuwa ingekuwa ni ngumu kwa Watu wenye ‘ PhD’s ‘ za uhakika kama Wao Kushindwa ‘ Kuikomboa ‘ Ndege yetu na kututaka Watanzania tuwaamini kwani hawakuenda Vyuo Vikuu Kupoteza muda bali walienda Kuelimika hasa.
Sasa GENTAMYCINE nauliza kama kweli Wao ( hilo Jopo la Maprofesa Wabobezi wa Sheria ) wameiva na walimuweza Mkulima kule nchini Afrika Kusini kwa Waafrika Wenzetu inakuwaje leo Jasho linawatoka kwa Mkulima aliyehamia kwa Wazungu nchini Canada? Na kwanini hivi sasa Watanzania hatupewi tena ‘ Updates ‘ za ‘ Kujimwambafai ‘ Kwao kama walivyokuwa wakitupa mara kwa mara walipokuwa Bondeni?
Huu ni Ushauri wangu tu binafsi Mimi GENTAMYCINE Kwao hilo Jopo la hao ‘ Maprofesa wa Kujimwambafai ‘ kuwa najua wana hizo ‘ PhD’s ‘ zao nzuri tu ila wasione Aibu kuomba Msaada kwa ‘ Genius ‘ wa Masuala ya Kisheria ambaye hana ‘ PhD’s ‘ kama Wao ila IQ yake tu Kubwa aliyonayo ni sawasawa na IQ’s zao wote hao Wanne na anaijua Sheria ‘ Kindakindaki ‘ kuliko Wao ‘ Mtani ‘ wangu wa Kinyiramba Ndugu Tundu Antipasi Lissu.
Nahisi kama tungeondoa ‘ Chuki ‘ Kwake Tundu Lissu na tukamshirikisha vyema kabisa katika hilo Jopo basi huyu Mkulima wala asingethubutu tena ‘ Kutusumbua ‘ Watanzania mara kwa mara na Kutufanya ‘ Mazuzu / Majuha ‘ namna hii. Acheni Siasa zenu na msione Aibu Kumuomba Tundu Lissu ‘ Kolabo ‘ nae ya Kisheria ili mfanikiwe vinginevyo huyu Mkulima atawanyimeni mno Usingizi na huenda hata baadhi yenu ikapelekea Kutoaminiwa na aliyewateua na mkazipoteza nafasi zenu za Kimamlaka / Kiuteuzi.
Sasa GENTAMYCINE nauliza kama kweli Wao ( hilo Jopo la Maprofesa Wabobezi wa Sheria ) wameiva na walimuweza Mkulima kule nchini Afrika Kusini kwa Waafrika Wenzetu inakuwaje leo Jasho linawatoka kwa Mkulima aliyehamia kwa Wazungu nchini Canada? Na kwanini hivi sasa Watanzania hatupewi tena ‘ Updates ‘ za ‘ Kujimwambafai ‘ Kwao kama walivyokuwa wakitupa mara kwa mara walipokuwa Bondeni?
Huu ni Ushauri wangu tu binafsi Mimi GENTAMYCINE Kwao hilo Jopo la hao ‘ Maprofesa wa Kujimwambafai ‘ kuwa najua wana hizo ‘ PhD’s ‘ zao nzuri tu ila wasione Aibu kuomba Msaada kwa ‘ Genius ‘ wa Masuala ya Kisheria ambaye hana ‘ PhD’s ‘ kama Wao ila IQ yake tu Kubwa aliyonayo ni sawasawa na IQ’s zao wote hao Wanne na anaijua Sheria ‘ Kindakindaki ‘ kuliko Wao ‘ Mtani ‘ wangu wa Kinyiramba Ndugu Tundu Antipasi Lissu.
Nahisi kama tungeondoa ‘ Chuki ‘ Kwake Tundu Lissu na tukamshirikisha vyema kabisa katika hilo Jopo basi huyu Mkulima wala asingethubutu tena ‘ Kutusumbua ‘ Watanzania mara kwa mara na Kutufanya ‘ Mazuzu / Majuha ‘ namna hii. Acheni Siasa zenu na msione Aibu Kumuomba Tundu Lissu ‘ Kolabo ‘ nae ya Kisheria ili mfanikiwe vinginevyo huyu Mkulima atawanyimeni mno Usingizi na huenda hata baadhi yenu ikapelekea Kutoaminiwa na aliyewateua na mkazipoteza nafasi zenu za Kimamlaka / Kiuteuzi.