BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,825
- 287,849
Zichukuliwe hatua Zanzibar isigeuke kisiwa cha ufuska, ulevi
Maulid Ahmed
Daily News; Wednesday,July 09, 2008 @20:01
HIVI karibuni nilikuwa Zanzibar kwa takriban wiki tatu kwa ajili ya shughuli za kikazi. Lakini kutokana na uenyeji wangu kisiwani huko niliona Zanzibar niliyokuwa naifahamu miaka 10 iliyopita sasa si hiyo tena.
Ninaweza kusema kuwa Zanzibar imeharibika nikiangalia upande wa utamaduni na maadili ya watu wake. Leo ni kawaida kukuta baa kila pembe, ni kawaida kukuta ngono ikifanyika hadharani kati ya wanawake na wanawake, wanaume na wanaume na hata wa jinsia hizo mbili.
Hali hiyo si mjini pekee lakini nimeishuhudia zaidi maeneo ya shamba hasa yenye hoteli za kitalii lakini pia kwa kuelezwa na wakazi wa huko.
Katika maeneo yenye kushamiri watalii ndipo uchafu huo hutendeka zaidi na hiyo kwa mawazo yangu naamini inatokana na utalii huo.
Kutokana na hali hiyo ndipo leo tunasikia athari za utalii huo ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ugonjwa wa Ukimwi kisiwani humo kama Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji Samia Suluhu Hassan alivyolieleza Baraza la Wawakilishi kuhusiana na utafiti uliofaywa kutathmini hali ya Ukimwi katika sekta ya utalii.
Nimefurahi kusikia Serikali yenyewe ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imelitambua hilo. Lakini nadhani umefika wakati wa kuchukua hatua kudhibiti hali hiyo.
Kauli kwamba Zanzibar njema atakaye aje ingefaa ifanyiwe tathmini tena licha ya kusudio lake kuwa zuri la kuwakaribisha watu. Ninachosema ni kwamba iangaliwe namna ya kuwakaribisha watu wema na si kuwakaribisha wabaya wanaokwenda kuiharibu.
Elimu ya Ukimwi bado naona ipo chini. wananchi wa kawaida wanahitajika kuelimishwa zaidi ikilinganishwa na eneo kama Dar es Salaam lenye kila aina ya starehe ambako watu wake wengi wanaifahamu elimu hiyo na hawaoni aibu kudai kondomu kwa wale wanaofanya shughuli hiyo ya kujiuza au kufanya ngono ovyo.
Kwa Zanzibar bado aibu ipo! Mtu anaona aibu kumwambia mwanamume avae kondom, anajihisi ataonekana mhuni. Hivi kufanya naye ngono mwanamume wa aina hiyo siyo uhuni? Inanishangaza sana.
Kwa habati mbaya udogo wa kisiwa hicho unafanya mambo yawe hadharani zaidi. Watoto wa kiume wanajiingiza katika mchezo wa kufanya mapenzi na wanaume wenzao kama inavyofahamika ushoga huku wanawake nao wanafanya mapenzi na wenzao tena kwa ufahari bila kujali kama kuna Ukimwi ambao unaendelea kuliteketeza taifa hili.
Licha ya taifa kupata fedha nyingi kutokana na utalii, ni vizuri zaidi iwapo serikali itaanzisha mkakati wa kuzitembelea hoteli hizo za kitalii na kudhibiti ufuska unaoendelea huko na ikiwezekana kuwachukulia hatua wale wanaojiuza ambao kwa sasa kisiwani huko wameingia kwa kasi.
Nimeshawahi kuelezwa kuwa katika hoteli za kitalii, kunarekodiwa sinema za ngono. Ingawa sijashuhudia lakini lisemwalo lipo na kama halipo linakuja, hali hiyo isipuuzwe.
Hizo baa zilizotapakaa kwa wingi si kuwa zinatumika tu kwa ajili ya watu kupata kinywaji kujiburudisha bali zimekuwa vichaka vya ufuska. Zipo baa maarufu za mashoga na hapa nisingependa kuzitaja lakini najua zinafahamika kunapofanyika ufuska waziwazi lakini nashangaa zinaachwa kushamiri badala ya kudhibitiwa.
Zisipofanyika jitihada za makusudi kukinusuru kisiwa hiki chenye wakazi wasiofikia milioni mbili basi Zanzibar yenye maadili, inayothamini utamaduni na watu wake wakarimu waliokuzwa kwa misingi ya dini itageuka na kuwa kisiwa cha ufuska, ulevi na kilichojaa waathirika wa Ukimwi.
Maulid Ahmed
Daily News; Wednesday,July 09, 2008 @20:01
HIVI karibuni nilikuwa Zanzibar kwa takriban wiki tatu kwa ajili ya shughuli za kikazi. Lakini kutokana na uenyeji wangu kisiwani huko niliona Zanzibar niliyokuwa naifahamu miaka 10 iliyopita sasa si hiyo tena.
Ninaweza kusema kuwa Zanzibar imeharibika nikiangalia upande wa utamaduni na maadili ya watu wake. Leo ni kawaida kukuta baa kila pembe, ni kawaida kukuta ngono ikifanyika hadharani kati ya wanawake na wanawake, wanaume na wanaume na hata wa jinsia hizo mbili.
Hali hiyo si mjini pekee lakini nimeishuhudia zaidi maeneo ya shamba hasa yenye hoteli za kitalii lakini pia kwa kuelezwa na wakazi wa huko.
Katika maeneo yenye kushamiri watalii ndipo uchafu huo hutendeka zaidi na hiyo kwa mawazo yangu naamini inatokana na utalii huo.
Kutokana na hali hiyo ndipo leo tunasikia athari za utalii huo ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ugonjwa wa Ukimwi kisiwani humo kama Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji Samia Suluhu Hassan alivyolieleza Baraza la Wawakilishi kuhusiana na utafiti uliofaywa kutathmini hali ya Ukimwi katika sekta ya utalii.
Nimefurahi kusikia Serikali yenyewe ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imelitambua hilo. Lakini nadhani umefika wakati wa kuchukua hatua kudhibiti hali hiyo.
Kauli kwamba Zanzibar njema atakaye aje ingefaa ifanyiwe tathmini tena licha ya kusudio lake kuwa zuri la kuwakaribisha watu. Ninachosema ni kwamba iangaliwe namna ya kuwakaribisha watu wema na si kuwakaribisha wabaya wanaokwenda kuiharibu.
Elimu ya Ukimwi bado naona ipo chini. wananchi wa kawaida wanahitajika kuelimishwa zaidi ikilinganishwa na eneo kama Dar es Salaam lenye kila aina ya starehe ambako watu wake wengi wanaifahamu elimu hiyo na hawaoni aibu kudai kondomu kwa wale wanaofanya shughuli hiyo ya kujiuza au kufanya ngono ovyo.
Kwa Zanzibar bado aibu ipo! Mtu anaona aibu kumwambia mwanamume avae kondom, anajihisi ataonekana mhuni. Hivi kufanya naye ngono mwanamume wa aina hiyo siyo uhuni? Inanishangaza sana.
Kwa habati mbaya udogo wa kisiwa hicho unafanya mambo yawe hadharani zaidi. Watoto wa kiume wanajiingiza katika mchezo wa kufanya mapenzi na wanaume wenzao kama inavyofahamika ushoga huku wanawake nao wanafanya mapenzi na wenzao tena kwa ufahari bila kujali kama kuna Ukimwi ambao unaendelea kuliteketeza taifa hili.
Licha ya taifa kupata fedha nyingi kutokana na utalii, ni vizuri zaidi iwapo serikali itaanzisha mkakati wa kuzitembelea hoteli hizo za kitalii na kudhibiti ufuska unaoendelea huko na ikiwezekana kuwachukulia hatua wale wanaojiuza ambao kwa sasa kisiwani huko wameingia kwa kasi.
Nimeshawahi kuelezwa kuwa katika hoteli za kitalii, kunarekodiwa sinema za ngono. Ingawa sijashuhudia lakini lisemwalo lipo na kama halipo linakuja, hali hiyo isipuuzwe.
Hizo baa zilizotapakaa kwa wingi si kuwa zinatumika tu kwa ajili ya watu kupata kinywaji kujiburudisha bali zimekuwa vichaka vya ufuska. Zipo baa maarufu za mashoga na hapa nisingependa kuzitaja lakini najua zinafahamika kunapofanyika ufuska waziwazi lakini nashangaa zinaachwa kushamiri badala ya kudhibitiwa.
Zisipofanyika jitihada za makusudi kukinusuru kisiwa hiki chenye wakazi wasiofikia milioni mbili basi Zanzibar yenye maadili, inayothamini utamaduni na watu wake wakarimu waliokuzwa kwa misingi ya dini itageuka na kuwa kisiwa cha ufuska, ulevi na kilichojaa waathirika wa Ukimwi.