Je, Zanzibar Ni Sehemu Salama Kwa Uwekezaji?

Rich Dad

JF-Expert Member
Dec 15, 2010
748
133
Wana JF naombeni Tujadili!
Kutokana na kushamiri kwa matukio ya hivi karibuni ya uchomaji wa biashara za watu na hasa zinazomilikiwa na watu wasio wazanzibari. Baa zimekuwa zikichomwa moto karibuni kila siku, inasemekana jeshi la polisi na mahakama halioneshi ushirikiano unaotakiwa kuwawajibisha watu wanaokula njama na kufanya vitendo hivyo.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba vitendo hivi wanafanyiwa wafanyabiashara wenye mitaji midogo, wachomaji hawa hawafiki hoteli kubwa ambako kimsingi watu ndo wanakuwa huru zaidi kufanya yale wayapendayo ( kuanzia kwenye kuvaa mavazi yanayoacha sehemu kubwa ya mwili wazi hadi kwenye unywaji wa pombe). Na mfano mzuri ni hoteli ya Zanzibar Beach Resort ambayo nilifikia juzi, nenda huko kajionee mwenyewe usisubiri kusimuliwa.

Vitendo hivi vikiendelea kufumbiwa macho bila vyombo vya usalama kuchukua hatua stahiki, nina mashaka na huko twendako. Je, Zanzibar imekuwa declared ni taifa la Kiislam? Na kama ni hivyo kwanini Zanzibar bado ni part ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania?

Tafadhali kama unaweza, toa maoni yako kuhusu nini kifanyike ili kuweka mambo sawa ndani ya Zanzibar.
 
Ukitaka poteza assets zako nenda kawekeze zanzibar kwenye issue za bar au pub.
 
zanzibar kila siku panazidi kuwa sehemu hatari kwa wawekezaje-haswa wa tanganyika-maana kuna Islamist hardliners wanaorise zanzibar ambao kwa mtazamo wangu polisi wameshindwa kuwazuia-hawa hardliners hawana tofauti na boko haram wale wa nigeria,wao kazi yao ni kuchoma bar za wawekezaji kila siku,nina imani siku bar zikiwewa zimeisha au zinakaribua kwisha watahamia kwenye biashara nyingine,na nyingine tena,
SO ZANZIBAR SI SEHEMU YA KUWEKEZA
 
Back
Top Bottom