Je, yaliyotokea sekta ya Korosho na Halmashauri kutokea pia kwenye Sekta ya Utalii?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Amani iwe kwenu wadau!

Kwa kumbukumbu zangu kuna mabadiriko ya sheria yaliyohusisha Fedha za zao la korosho na vyama vya ushirika. Mabadiriko yale yalipingwa vikali sana na wabunge wa kusini akiwemo Nape na kupelekea Hawa Ghasia kutumia diplomasia kujiuzuru uwenyekiti wa kamati moja ya Bunge. Serikali kutaka Fedha za korosho ililazimisha, Kilichofuata ni kuharibika kwa soko na biashara ya zao la korosho. Saivi hakuna anayethubutu kusema chochote kuhusu zao hili.

Ilifuata suala la Fedha za halmashauri/ Mapato yake kwenda Serikali Kuu. Kilichofuata ni halmashauri kushindwa kujiendesha na nyingi ziko hoi.

Funga Kazi ni hili la bajeti ya mwaka huu, Fedha za Tanapa, Tawa na Ngorongoro kwenda Serikali kuu. Hii inamaanisha wale jamaa wakitaka hata hela za kurekebisha lodge zao, barabara za Mbugani na mazingira ya mbugani itabidi waombe hela kutoka Serikali kuu na zifuate mchakato uleule kama ofisi zingine za Serikali ambazo zikiombaga hela huwa kama sio zinachelewa kwa miezi basi hazipewi kabisa.

Je, kwa marekebisho haya, Huu ndo mwisho wa kuendelea na kustawi kwa Sekta ya Utalii Tanzania?

Waliopendekeza marekebisho haya hawajajifunza kwenye Halmashauri na Kwenye korosho kusini?

Mwisho naisi kuna mtu anataka aonekane anavunja rekodi ya makusanyo kumbe hakuna lolote. Anachofanya ni kuzielekeza tu Fedha zote ziingie serikali kuu kupitia TRA jambo ambalo nina uhakika hata Kikwete angefanya tena kwa jinsi alivyostawisha uwekezaji, makusanyo kwa mwezi yangekuwa hata Trilioni 3

Ijumaa Kareem!
 
Mapendekezo yangu ni kuwa Tawa, Tanapa na Ngorongoro waachwe wakusanye fedha zao na wazipangie matumizi wenyewe.

Kama kulikuwa na walakini kwenye matumizi wawekewe tu mfumo mzuri kwa kudhibiti matumizi mabaya.

Kenya na Rwanda wataenda kukamata kabisa sekta ya utalii kwa ukanda huu maana ni ukweli usiopingika Hifadhi zetu zitakuwa na miundombinu duni isiyorekebishwa kwa wakati hivyo watalii kushauriwa kutokuja Tanzania. Sekta ya utalii itashuka vibaya sana na pia wanyama wetu walioanza kuongezeka kwa kasi watapungua sana.
 
Sekta ya utalii ndo ilikuwa kiuhalisia ndo sekta inayokuwa kuliko sekta zote nchini na ndo sekta inayoziogopesha nchi tunazoshindana nazo kwa ukanda huu hasa Kenya na Rwanda.

Kilichosababisha sio tu bahati ila Tanapa, Tawa na Ngorongoro walikuwa wanatumia fedha zao kuboresha miondombinu na kuweka teknolojia nzuri kwa ajili ya kuwalinda wanyama na kutengeneza mahusiano mazuri na vijiji jirani ili kupunguza ujangiri kitu kilichopelekea Tanzania kuwa na wanyama wengi kuliko nchi zinazotuzunguka.

Kuwaondolea hawa hela kutawafanya kutokuwa hata na miradi ya ujirani mwema kama kuweka miradi katika vijiji jirani kuzuia wananchi kufanya ujangiri.

Tanzania tunaenda kupotea mazima kwenye utalii maana hata ujangiri utarudi kwa kasi sana.
 
Amani iwe kwenu wadau!

Kwa kumbukumbu zangu kuna mabadiriko ya sheria yaliyohusisha Fedha za zao la korosho na vyama vya ushirika. Mabadiriko yale yalipingwa vikali sana na wabunge wa kusini akiwemo Nape na kupelekea Hawa Ghasia kutumia diplomasia kujiuzuru uwenyekiti wa kamati moja ya Bunge. Serikali kutaka Fedha za korosho ililazimisha, Kilichofuata ni kuharibika kwa soko na biashara ya zao la korosho. Saivi hakuna anayethubutu kusema chochote kuhusu zao hili.

Ilifuata suala la Fedha za halmashauri/ Mapato yake kwenda Serikali Kuu. Kilichofuata ni halmashauri kushindwa kujiendesha na nyingi ziko hoi.

Funga Kazi ni hili la bajeti ya mwaka huu, Fedha za Tanapa, Tawa na Ngorongoro kwenda Serikali kuu. Hii inamaanisha wale jamaa wakitaka hata hela za kurekebisha lodge zao, barabara za Mbugani na mazingira ya mbugani itabidi waombe hela kutoka Serikali kuu na zifuate mchakato uleule kama ofisi zingine za Serikali ambazo zikiombaga hela huwa kama sio zinachelewa kwa miezi basi hazipewi kabisa.

Je, kwa marekebisho haya, Huu ndo mwisho wa kuendelea na kustawi kwa Sekta ya Utalii Tanzania?

Waliopendekeza marekebisho haya hawajajifunza kwenye Halmashauri na Kwenye korosho kusini?

Mwisho naisi kuna mtu anataka aonekane anavunja rekodi ya makusanyo kumbe hakuna lolote. Anachofanya ni kuzielekeza tu Fedha zote ziingie serikali kuu kupitia TRA jambo ambalo nina uhakika hata Kikwete angefanya tena kwa jinsi alivyostawisha uwekezaji, makusanyo kwa mwezi yangekuwa hata Trilioni 3

Ijumaa Kareem!
Ninachojaribu kujua in TRA in wazuri kukusanya mapato kutoka vyanzo ambavyo ni stationed ,fixed ni pre identified ambayo ni rahisi kuyainvoiced lakini kwa mapato ambayo ni unpredictable ni ngumu kukusanywa na TRA,kama mapato ambayo hujui kesho atalipa nani, hivi tayari TRA wanakusanya 100% kodi ya maato?,vat?custom&excise?na n.k
 
Tanapa inapita kwenye hali ngumu,wasaidiwe na serikali hadi pale ongezeko la watalii itarudi hali ya kawaida.
Lakini Ngorongoro crater huwa ikapata misaada mikubwa ya kitafiti na kuhifadhi kutoka vyuo mbali mbali tokea Mataifa tajiri.Pia kuna taasisi nyingi za kigeni zinaleta msaada kwa sekta hii,labda wakati umefika wa kuendesha shughuli hizi kwa uwazi zaidi.
 

Attachments

  • VID-20200611-WA0000.mp4
    2.8 MB
Tanapa inapita kwenye hali ngumu,wasaidiwe na serikali hadi pale ongezeko la watalii itarudi hali ya kawaida.
Lakini Ngorongoro crater huwa ikapata misaada mikubwa ya kitafiti na kuhifadhi kutoka vyuo mbali mbali tokea Mataifa tajiri.Pia kuna taasisi nyingi za kigeni zinaleta msaada kwa sekta hii,labda wakati umefika wa kuendesha shughuli hizi kwa uwazi zaidi.
 
Ninachojaribu kujua in TRA in wazuri kukusanya mapato kutoka vyanzo ambavyo ni stationed ,fixed ni pre identified ambayo ni rahisi kuyainvoiced lakini kwa mapato ambayo ni unpredictable ni ngumu kukusanywa na TRA,kama mapato ambayo hujui kesho atalipa nani, hivi tayari TRA wanakusanya 100% kodi ya maato?,vat?custom&excise?na n.k
Lengo kuu ya mabadiriko haya ni kuwa hela zote zinazolipwa na watalii kwenda Ngorongoro, Tawa na TANAPA ziingie kwanza Serikali Kuu, alafu serikali kuu ndo iwapangie matumizi na wao wawe wanaomba serikali kuu.
Kwa malalamiko yanayotokea toka taasisi za serikali ya kutopewa fedha kwa wakati na wakati mwingine kutopewa kabisa naona hii ndo uuaji wa sekta ya utalii Tanzania. Hifadhi zetu zitakuwa na ari mbaya, miradi ya ujirani mwema ambapo vijiji jirani vilikuwa vinapata miradi na fedha toka kwenye hifadhi ifakufa na wananchi watarudi kwenye ujangiri kwa kiwango kikubwa sana.

Yakianza kutokea haya tutapandisha huu uzi kama kumbukumbu.
 
Tanapa inapita kwenye hali ngumu,wasaidiwe na serikali hadi pale ongezeko la watalii itarudi hali ya kawaida.
Lakini Ngorongoro crater huwa ikapata misaada mikubwa ya kitafiti na kuhifadhi kutoka vyuo mbali mbali tokea Mataifa tajiri.Pia kuna taasisi nyingi za kigeni zinaleta msaada kwa sekta hii,labda wakati umefika wa kuendesha shughuli hizi kwa uwazi zaidi.
Sahihi kabisa. Hali ya utalii ni mbaya saivi kutokana na dunia kukumbwa na mdororo wa uchumi. Je suluhisho ndo hili hela zote zilizokuwa zinakusanywa na hifadhi ziende kwanza Serikali kuu then hifadhi ndo ziombe tena kama taasisi nyingine za serikali???

Sekta ya utalii ni sekta nyeti sana, na ina ushindani sana. Inahitaji fedha kuwepo wakati wote hasa kwa kuboresha miundombinu na hata kufanya matangazo ili watalii waje kwako wasiende uganda, Kenya , Rwanda au Zambia.

Pamoja na changamoto zote ila uelekeo ulianza kuwa mzuri maana TANAPA walianza kujitangaza sana na sasa kusema kweli Tanzania tulikuwa tunaelekea pazuri. Hii ni kutokana na sababu kuwa hizi hela zilikuwa zinatumika kwa wao kujipangia sehemu gani ya kuweka nguvu na kwa wakati gani.

Kwa mabadiriko haya watahitajika nao kuwa wanaomba wizara ya fedha. Ambapo nchi nzima kuna mlolongo wa Taasisi, Idara na wizara zikipeleka maombi. Swali ni je wataweza kuhimili ushindani kwa utaratibu huu mpya ambao unajulikana ulivyo na changamoto maana unapoomba hela serikalini inasemwa huwa haitoki kwa wakati na muda mwingine hupewi kabisa maana mambo ni mengi.

Na kuhusu Ngorongoro, Je wataendelea kupata misaada siku zote???? Na misaada ni fedha za uhakika kupelekea wewe kubadili sheria???
 
Sahihi kabisa. Hali ya utalii ni mbaya saivi kutokana na dunia kukumbwa na mdororo wa uchumi. Je suluhisho ndo hili hela zote zilizokuwa zinakusanywa na hifadhi ziende kwanza Serikali kuu then hifadhi ndo ziombe tena kama taasisi nyingine za serikali???

Sekta ya utalii ni sekta nyeti sana, na ina ushindani sana. Inahitaji fedha kuwepo wakati wote hasa kwa kuboresha miundombinu na hata kufanya matangazo ili watalii waje kwako wasiende uganda, Kenya , Rwanda au Zambia.

Pamoja na changamoto zote ila uelekeo ulianza kuwa mzuri maana TANAPA walianza kujitangaza sana na sasa kusema kweli Tanzania tulikuwa tunaelekea pazuri. Hii ni kutokana na sababu kuwa hizi hela zilikuwa zinatumika kwa wao kujipangia sehemu gani ya kuweka nguvu na kwa wakati gani.

Kwa mabadiriko haya watahitajika nao kuwa wanaomba wizara ya fedha. Ambapo nchi nzima kuna mlolongo wa Taasisi, Idara na wizara zikipeleka maombi. Swali ni je wataweza kuhimili ushindani kwa utaratibu huu mpya ambao unajulikana ulivyo na changamoto maana unapoomba hela serikalini inasemwa huwa haitoki kwa wakati na muda mwingine hupewi kabisa maana mambo ni mengi.

Na kuhusu Ngorongoro, Je wataendelea kupata misaada siku zote???? Na misaada ni fedha za uhakika kupelekea wewe kubadili sheria???
Tatizo ni la kiutawala ,kila mtawala anakuja na yake.Leo Magufuli anaongeza idadi ya National parks,jana Kikwete alikuwa anauza Twiga Dubai,juzi Mkapa aligawa vitalo vya uwindaji kwa watu fulani,na hapo nyuma Mwinyi kampa kipande cha ardhi mfalme wa Emirates Loliondo kwa miaka 99.
Kwa namna hii ni wazi hatuwezi kutoboa,japo tuna vivutio kuliko Kenya na South Africa.
 
Hapa tutegemee sekta hii kuporomoka , kwan sehem zote zinatotumia utaratibu huu uliopangwa na serekali mambo yako hovyo, kwa na huku tutegemee vivyo hivyo
 
Tatizo ni la kiutawala ,kila mtawala anakuja na yake.Leo Magufuli anaongeza idadi ya National parks,jana Kikwete alikuwa anauza Twiga Dubai,juzi Mkapa aligawa vitalo vya uwindaji kwa watu fulani,na hapo nyuma Mwinyi kampa kipande cha ardhi mfalme wa Emirates Loliondo kwa miaka 99.
Kwa namna hii ni wazi hatuwezi kutoboa,japo tuna vivutio kuliko Kenya na South Africa.
Natofautiana na Magufuli maeneo mengi , ila kusema kweli hakukuwa na kosa la kuongeza National Park. Ni uamuzi sahihi.

Ni kweli pia kuwa Tanzania tuna wanyama wengi na vivutio vingi kuliko nchi nyingi zinazotuzunguka, Asante kwa sera nyingi nzuri zikiwemo miradi ya ujirani mwema iliyokuwaikitekelezwa na hifadhi na mapori ambayo ilisaidia sana ku punguza ujangiri.

Sekta ya utalii ni sekta yenye faida sana ila inahitaji kutumia sana fedha ili upate fedha nyingi. Kwa mabadiriko haya ya sheria Nina uhakika sekta hii itashindwa kuhimili ushindani maana watalii wanaitaji ukisasa zaidi na mabadiriko ya mara kwa mara yanayowavutia zaidi.
 
Ushenzi wa kingwangalla kuchota fedha hovyo huko ndio kumepelekea mapalendekezo hayo. Tunaenda kuua hizo taasisi.
 
Back
Top Bottom