Je, yaliyotokea Kenya, Congo, na Uganda ni kushindwa kwa ubepari?

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Kuna documentari moja inatayarishwa na waandishi wa habari wa kiafrika wanaofanya kazi kwenye mashirika makubwa ya habari ya uropa na amerika. Documentari hii ilisimama kwa muda baada ya mmoja wa wataarifu habari (reporter) maarufu kutoka nchi moja ya afrika mashariki kuacha/chishwa kazi katika mazingira yasiyo na kueleweka kabisa.

Katika documentary hii, kumeonyeshwa maisha ya wananchi wa nchi zilizoamua kuwa za kibepari afrika baada ya uhuru ikilinganishwa na zile zilizoamua kuwa za kijamaa (au kutofungamana na upande wowote). Niliguswa sana na clips toka kwa majirani zetu wa Kenya, Uganda, na Congo.

Ilionyeshwa kuwa, Kenya kulikuwa na watoto ombaomba (chokoraa) karibu milioni moja wanaoishi maisha ya kubahatisha. Ilionyeshwa pia kuwa Kuna watu zaidi ya milioni nne wanaoishi katika slums na hali mbaya ya kiafya na kimazingira. Uganda kulionyeshwa maelfu ya watoto wanaotembea kilomita nyingi kila siku kwenda kulala kwenye miji mikubwa kwa sababu hawana pa kulala. Kuna watoto zaidi ya milioni moja Congo wasiokuwa na hakika ya kula mlo mmoja wa siku. Habari imekuwa mbaya kwa Malawi ambayo baa la njaa la miaka michache iliyopita limeacha watu wengi taabuni.

Nchi za kijamaa nazo wameonyesha Ghana, Tanzania, Zambia (sijui ni vigezo gani wametumia) zimepitia matatizo haya haya na hakuna mwenye nafuu kidogo ingawa waandishi hawa wote wanakiri kuwa Slums za Kibera nk za kenya ndizo kubwa kabisa katika nchi yoyote Afrika (sijui bado vigezo). Hii documentary imeonyeshwa kwa wanachama wa chama cha waafrika hapa chuoni kwangu ili kupata mawazo yao kabla haijaanza kusambazwa.

Kilichonishangaza ni kuwa, wengi walioiona hawakupinga kuwa iko biased ila walianza kulaumu ubepari na ujamaa. Wote tunajua kuwa ujamaa wa russia uliporomoka na kushindwa wakati wanaojiita mabepari - marekani wakionekana kufanikiwa. Swali ni je, hali mbaya ya wananchi wa nchi za "kibepari" afrika ni dalili ya kushindwa kwa ubepari Afrika?
 
Swali ni je, hali mbaya ya wananchi wa nchi za "kibepari" afrika ni dalili ya kushindwa kwa ubepari Afrika?

Mkuu MWK,

Heshima mbele, sina uhakika kama mifano ya nchi zilizotajwa kama mifano ya ubepari katika Afrika, zinatimiza matakwa rasmi ya kupewa jina hilo la ubepari. Kwa sababu binafsi ninaaamini kuwa kuna cnhi ambazo zinatimiza matakwa hayo kama Afrika Kusini, Botswana, na Namibia, ambako ubaperi unafanyika in fulll gear na hakuna matatzio kama yaliyopo kwenye nchi ulizozitaja au zilizotajwa kwenye hiyo documentary, ubepari bado kushindwa kuanzia Afrika wala Europe, isipokuwa pale tu ulipojaribishwa bila ya kufuata masharti yake in full.

Argentina, ulikuwa ni mfano mkubwa wa kujaribisha bila kufuata masharti yake in full, mpaka walipokubali kufuata masharti yake yote sasa wameanza kuwa na nafuu na kuona matunda yake. Ubepari siku zote unafuatana na demokrasia, na sidhani kuna any ya hizo nchi zilizotumika kama mfano wa kushindwa kwa demokrasia Afrika, zimashawahi ku-practice angalau hata 1/4 ya true demokrasia.

Ubepari bado haujshindwa, lakini sio siri kuwa American empire iko njiani kuelekea kwenye ku-decline, kwa sababu ya ubepari kukosa mpinzani kwa muda mrefu!
 
No, hali mbaya za watu wa mataifa ya Kiafrika yanayofuata mfumo wa kibepari au mfumo wowote ule (ujima, ujamaa, feudalism, imperialism etc etc) zinasababishwa na jinsi sisi wenyewe tulivyo kiasili (yaani tuna dosari za kiasili). Kwa hiyo kulaumu laumu ubepari au mifumo ya kimagharibi ni moja ya visingizio tu visivyo na kichwa wala miguu. Waafrika Ndiyo Tulivyo.
 
Ubepari wa Marekani hausimami kwa sababu ni Mfumo mzuri, unasimama kwa sababu ni mfumo wa kimumiani.

Ona walivyodhoofisha uchumi wa nchi za America ya kusini kwa kisingizio cha kuzuia Ukomunisti usiingie huko.
Ona wanavyosimamia mzunguko wa fedha Duniani kwa uharamia mkubwa?
Katika Biashara kuna Pazia Zito la kiyoo kutenganisha Bei za kununulia Bidhaa kutoka Dunia ya 3 na bei ya kuziuzia Dunia ya 1.
Kuna Ukiritimba mkubwa unaohusisha umwagaji damu ili kuzuia watu wa ulimwengu wa 3 kuuza moja kwa moja kwenye soko la Dunia kwa uhuru.
Mra utaambiwa kahawa yako chafu au nchi yako ina kipundupindu na kifua kikuu, ukimpasia bidhaa hiyo hiyo jamaa kutoka dunia ya 1 bidha inauzwa bila mkwara na faida anakula yeye.

Demand and Supply ni dhana halisi kwao wenyewe kutoka dunia ya 3 wakiwa wamejifungia kwney Pazia la kioo.

Bei ya kahawa iwe chini ya $1 kwa kilo Tanzania au nchi nyingine ya ulimwengu wa 3 kisha ikifika hapa Marekani Kikombe kimoja cha kahawa kiwe $4?
Ni kil ngapi za kahawa zinatumika kutengenezea hicho kikombe komoja?

Ukipiga Hesabu ya kuweza kukifikisha kiombe cha kahawa $4 hapa Marekani na Kilo 1 ya kahawa kuwa less than $1 kule tanzania unagundua siri ya Pazia la kioo.

Marekani inahusika kwa asilimia 75% katika uharifu wa Kibenki Dunia nzima. Hawa ni Mabingwa wa kitu inaitwa Money Laundering.

http://www.unodc.org/images/odccp/money_laundering_scheme_big.jpg

http://static.howstuffworks.com/gif/money-laundering-4.jpg

Kila mwaka Zinaingia Billions za Dola kutoka fedha chafu za kila Biashhara chafu hapa Duniani.
Uchafu huu ni mkuu kuliko hata uchafu wa Mafia.

Mafanikio ya Marekani yana sura mbili.
Moja ni juhudi za hawa jamaa za kufanya utafiti wa hali ya juu katika kila uwanja wa elimu ya sayansi na jamaii.
uwanja wa pili ni Uharamia wa hali ya juu wa kutumia elimu hiyo hiyo.
 
Kuna documentari moja inatayarishwa na waandishi wa habari wa kiafrika wanaofanya kazi kwenye mashirika makubwa ya habari ya uropa na amerika. Documentari hii ilisimama kwa muda baada ya mmoja wa wataarifu habari (reporter) maarufu kutoka nchi moja ya afrika mashariki kuacha/chishwa kazi katika mazingira yasiyo na kueleweka kabisa.

Katika documentary hii, kumeonyeshwa maisha ya wananchi wa nchi zilizoamua kuwa za kibepari afrika baada ya uhuru ikilinganishwa na zile zilizoamua kuwa za kijamaa (au kutofungamana na upande wowote). Niliguswa sana na clips toka kwa majirani zetu wa Kenya, Uganda, na Congo.

Ilionyeshwa kuwa, Kenya kulikuwa na watoto ombaomba (chokoraa) karibu milioni moja wanaoishi maisha ya kubahatisha. Ilionyeshwa pia kuwa Kuna watu zaidi ya milioni nne wanaoishi katika slums na hali mbaya ya kiafya na kimazingira. Uganda kulionyeshwa maelfu ya watoto wanaotembea kilomita nyingi kila siku kwenda kulala kwenye miji mikubwa kwa sababu hawana pa kulala. Kuna watoto zaidi ya milioni moja Congo wasiokuwa na hakika ya kula mlo mmoja wa siku. Habari imekuwa mbaya kwa Malawi ambayo baa la njaa la miaka michache iliyopita limeacha watu wengi taabuni.

Nchi za kijamaa nazo wameonyesha Ghana, Tanzania, Zambia (sijui ni vigezo gani wametumia) zimepitia matatizo haya haya na hakuna mwenye nafuu kidogo ingawa waandishi hawa wote wanakiri kuwa Slums za Kibera nk za kenya ndizo kubwa kabisa katika nchi yoyote Afrika (sijui bado vigezo). Hii documentary imeonyeshwa kwa wanachama wa chama cha waafrika hapa chuoni kwangu ili kupata mawazo yao kabla haijaanza kusambazwa.

Kilichonishangaza ni kuwa, wengi walioiona hawakupinga kuwa iko biased ila walianza kulaumu ubepari na ujamaa. Wote tunajua kuwa ujamaa wa russia uliporomoka na kushindwa wakati wanaojiita mabepari - marekani wakionekana kufanikiwa. Swali ni je, hali mbaya ya wananchi wa nchi za "kibepari" afrika ni dalili ya kushindwa kwa ubepari Afrika?

Mwanamke wa Kike:

Hapa itabidi nitafute glove tuanze ngumi. Kwanza inabidi tutofautishe vitu viwili. Ubepari muundo wa kiuchumi na serikali ina-support huo muundo.

Ubepari kama muundo wa uchumi una kanuni zake na moja kubwa kuruhusu ushindani wa uchumi ulio huru na kazi ya serikali ni kuakikisha kuwa hizo za ushindani zinafuatwa.

Uganda, Kenya na Zaire hazikuwa nchi za kibepari. Serikali hazikulinda kanuni za ushindani na walichofanya viongozi ni kujipendelea kama vile unavyoona mafisadi wetu wa sasa.
 
Bin Mariam,
Mojawapo ya mazingaombwe ya ubepari ni ile dhana kwamba unaruhusu ushindani wa uchumi ulio huru. Ubepari misingi yake ni samaki mkubwa kummeza mdogo. Hata Marekani kwenyewe kumekuwepo na mabavu ya big corporates ku"squeeze out" competitions.
 
Ubepari na dhana nzima inayoendana na ubepari (at least ubepari wa US) iko based kwenye ile ile philosophy aliyoitaja Jasusi...Samaki mkubwa kumla mdogo au kwa maneno mengine mkubwa kumnyonya mdogo.

Sasa kibao kinapogeuka, kama inavyokuwa kwa biashara kati ya China na USA, hawa mabepari ambao wamefikia kiwango cha juu cha ubepari (UBEBERU) hufikiria njia za kibeberu katika kubaki juu.

Bahati mbaya hii imeshindikana kwa China na sasa wanazungumzia "Trade Deficit"...yoooote ni spin ya kukimbia ukweli, China sasa ni samaki mkubwa.

Kwa nchi zetu za kiafrika...mmh...Ukifanya kazi sana ukipata pesa kuliko wengine (in other words ukawa samaki mkubwa), kunatokea conflict mbaya sana. Bado akili zetu ziko kwenye ujamaa, kipindi hiki cha Transition (Mpito?) ni kigumu na kinahitaji busara. Pia tunatakiwa tujiulize...tunataka kwenda alipo marekani na mabepari wengine AU tunajenga ubepari wetu..eeh...tuiite nini, UJAPARI?
 
Kila mara nimekuwa nasema kilichotuangusha waafrika kiuchumi na kijamii kwa asilimia 100 ni viongozi wetu. Hakuna cha siasa ya ujamaa wala ubepari. Ni RUSHWA tu, PERIOD. Hebu angalia mwaka mmoja tu tumegundua uwizi wa $130m (minimum) benki kuu. Je miaka 46 ya uhuru ni kiasi gani wameiba hawa viongozi wetu? Je fedha zote hizo zingeingia kwenye uchumi leo hii tungekuwa wapi?

Mbona nchi kama Korea, Malaysia, Singapore, nk. pamoja na ubepari wao miaka ya 60 tulikuwa tumezipita mbali sana kiuchumi? Ni nini kilitokea hadi tukakwama kama sio uwizi na kukosa kuwajibika kwa viongozi wetu?

Kwa kweli kama hawa jamaa (viongozi) wana aibu basi wangepaswa hata kujinyonga na sio kusimama mbele za watu na kutamba kwamba wametuletea maendeleo, umoja na mshikamano.

Sometimes nakubaliana na Freeman kwamba heri wakati wa mkoloni kuliko wakati wowote baada ya uhuru watanzania.
 
Inawezekana context ya filamu yenyewe hii na maudhui yake hayashabihiani. Maana mimi mpaka leo najiuliza, kwa wale wanaosomasoma mambo ya itikadi, hivi kuna nchi Africa inayofuata itikadi yeyote kweli sasa hivi? Sasa ukishakosea context hata conclusion yako ita-flawed. Kusema malaria ni tatizo Africa ni kitu kimoja, lakini kusema yanasababishwa na nini ni swala lingine. Kwa mtindo wa filamu hii sitashangaa kama hawa jamaa wakaishia na hitimisho kwamba malaria yanasababishwa na ngono zembe wakati tunajua siyo! Sasa matatizo hayo wanayoyaeleza kwenye filamu yao ndiyo yapo, lakini itachukua miaka mingi kunishawishi kwamba yanasababishwa na ujamaa au ubepari.
 
Mkuu MWK,

Heshima mbele, sina uhakika kama mifano ya nchi zilizotajwa kama mifano ya ubepari katika Afrika, zinatimiza matakwa rasmi ya kupewa jina hilo la ubepari. Kwa sababu binafsi ninaaamini kuwa kuna cnhi ambazo zinatimiza matakwa hayo kama Afrika Kusini, Botswana, na Namibia, ambako ubaperi unafanyika in fulll gear na hakuna matatzio kama yaliyopo kwenye nchi ulizozitaja au zilizotajwa kwenye hiyo documentary, ubepari bado kushindwa kuanzia Afrika wala Europe, isipokuwa pale tu ulipojaribishwa bila ya kufuata masharti yake in full.

Argentina, ulikuwa ni mfano mkubwa wa kujaribisha bila kufuata masharti yake in full, mpaka walipokubali kufuata masharti yake yote sasa wameanza kuwa na nafuu na kuona matunda yake. Ubepari siku zote unafuatana na demokrasia, na sidhani kuna any ya hizo nchi zilizotumika kama mfano wa kushindwa kwa demokrasia Afrika, zimashawahi ku-practice angalau hata 1/4 ya true demokrasia.

Ubepari bado haujshindwa, lakini sio siri kuwa American empire iko njiani kuelekea kwenye ku-decline, kwa sababu ya ubepari kukosa mpinzani kwa muda mrefu!

Mkuu FMES,

Kuna debate kubwa sana inaendelea hapa kuhusu ubepari na ujamaa. Kuna watu wengi sasa wanaamini kuwa hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kudai kwa hakika kuwa ni ya kijamaa au ya kibepari. Ukiangalia nchi zinazodai kuwa za kibepari kama marekani, kuna sera nyingi tu za kijamaa zinaendeshwa na serikali zao kama ilivyo kwa nchi nyingi zinazodai kuwa za kijamaa zinavyokuwa na mabepari kibao (wengi wao wakiwa viongozi wa serikali).

Ugomvi wangu katika documentary hii haukuwa sana katika nani alaumiwe kwa umasikini wa bongo. Ugomvi wangu ulikuwa katika dhani nzima ya kutengeneza documentary ya kuonyesha mabaya tu katika nchi za afrika (ukichukulia kuwa hii documentary inatengenezwa na reporters ambao asili yao ni Afrika).

Kitu kimoja nimegundua kuwa kuna tatizo kubwa sana Afrika zaidi ya sera zinazoongoza nchi. Hebu angalia hali ya maisha ya South Afrika leo hii. Je unaweza kusema kuwa wananchi wa kawaida kwa asilimia ngapi wanafaidika na mafanikio ya nchi hiyo? Je ni kweli Botswana ni nchi ya kibepari iwapo serikali ya nchi hiyo inafanya biashara na huduma kwa wananchi nyingi zinatolewa na serikali bure (mambo aliyojaribu kufanya nyerere na dunia nzima ikasema huo ni ujamaa)?

Kuna tatizo somewhere zaidi ya ujamaa na ubepari kwa waafrika na kwa sasa ninatafuta kulijua hili tatizo.
 
Mwanamke wa Kike:

Hapa itabidi nitafute glove tuanze ngumi. Kwanza inabidi tutofautishe vitu viwili. Ubepari muundo wa kiuchumi na serikali ina-support huo muundo.

Ubepari kama muundo wa uchumi una kanuni zake na moja kubwa kuruhusu ushindani wa uchumi ulio huru na kazi ya serikali ni kuakikisha kuwa hizo za ushindani zinafuatwa.

Uganda, Kenya na Zaire hazikuwa nchi za kibepari. Serikali hazikulinda kanuni za ushindani na walichofanya viongozi ni kujipendelea kama vile unavyoona mafisadi wetu wa sasa.

Wewe binti wa Maryam,

Bado nasubiri kuona tofauti ya ubepari muundo wa kiuchumi na serikali ina-support huo muundo. Huna sababu ya kuvaa gloves maana hii mada sio confrotational. It rather should be educational, what say you!
 
Bin Mariam,
Mojawapo ya mazingaombwe ya ubepari ni ile dhana kwamba unaruhusu ushindani wa uchumi ulio huru. Ubepari misingi yake ni samaki mkubwa kummeza mdogo. Hata Marekani kwenyewe kumekuwepo na mabavu ya big corporates ku"squeeze out" competitions.

Hakuna kitu perfect ambacho kitakupa faida bila kuwa na hasara. Na moja ya hasara za ushindani huru ni mwenye nguvu kushinda kama ulivyoeleza hapo juu. Hili kupunguza matatizo haya ndio serikali inapoingilia kati na kuweka sheria.

Kwa mfano AT&T lilikuwa ndio shirika pekee la simu Marekani. Na matatizo yaliotokea ni kuwa gharama zilizidi kwa mtumiaji na shirika lilifanya juhudi ndogo katika mambo ya innovation. Mwaka 1982 serikali ilishtaki AT&T na matokeo ya mashtaka haya kuligawa shirika hili katika makundi madogo madogo.

Ku-squeeze out competitions ni nature. Kabla mbwa wa kike ajakubali kutoa uroda ni lazima mbwa wa kiume washindane. Shaka Zulu aliunda Zulu Empire kwa ku-squeeze out competitions. The warlord Mirambo ali-squeeze out competitions kuanzisha Empire ya wanyamwezi. Mfumo wa chama kimoja cha siasa ni ku-squeeze out competitions za kifikra.

Hivyo hatuwezi ku-avoid ushindani. Lakini hili ushindani uwe na maana ni lazima sheria ziwepo hili ushindani ulete faida kwa jamii inayoitumikia (creative destruction).

Tukirudi kwenye mada Congo na Kenya sio mfano wa ubepari. Na sababu kubwa ya Tanzania na Zambia kutokuwa na slum nyingi zinatokana na ukweli wa mfumo wa utawala wa mwingereza ambao ulifanya nchi fulani kuwa za makazi ya wazungu na nchi zingine kuwa za uzalishaji.

Katika nchi za Afrika mashariki: Kenya, Uganda na Tanzania. Kenya ilikuwa ni nchi ya makazi. Tanzania na Uganda zilikuwa wazalishaji tu. Faida ya makazi ni kwamba wakoloni walijenga miundo mbinu lakini wazawa walinyang'anywa ardhi. Faida ya nchi za uzalishaji, wazawa walibakia na vipande vyao vya ardhi.

katika nchi za Afrika ya kati (Rhodesia): Zambia na Malawi walikuwa wazalishaji wakati Zimbabwe yalikuwa ni wazawa walinyang'anywa vipande vya ardhi.
 
Wewe binti wa Maryam,

Bado nasubiri kuona tofauti ya ubepari muundo wa kiuchumi na serikali ina-support huo muundo. Huna sababu ya kuvaa gloves maana hii mada sio confrotational. It rather should be educational, what say you!

Kuna tofauti kubwa kati Bin na Binti. Na kwa sisi wenye asili ya kihabeshi Maryam ni jina la Kiume, remember !!!.
 
Kuna tofauti kubwa kati Bin na Binti. Na kwa sisi wenye asili ya kihabeshi Maryam ni jina la Kiume, remember !!!.

Ingawa sijui sana unamaanisha nini hapa lakini ngoja niachane nayo maana si sehemu ya mada labda ueleze kidogo kuhusu tofauti ya maneno uliyotaka kuhusiana na ubepari!
 
Ingawa sijui sana unamaanisha nini hapa lakini ngoja niachane nayo maana si sehemu ya mada labda ueleze kidogo kuhusu tofauti ya maneno uliyotaka kuhusiana na ubepari!

Ubepari: Ni muundo wa maisha ambao uzalishaji na usambaji huko kwa sehemu kubwa chini ya mikono ya watu au mashirika binafsi kwa kufuata misingi ya soko huru.

Serikali ya kibepari ni inayoakikisha kuwa misingi ya masoko huru inafuatwa na vile vile watu wana haki ya kumiliki ya kile walichozalisha. Kwa msingi huu serikali sio mzalishaji ni regulator.

Serikali za kiafrika zilizofuata au ambazo sasa hivi zinaingia katika mfumo huu (Tanzania) hazifanyi juhudi yoyote kuhakikisha misingi ya masoko huru inafuatwa.

Kwa mfano: Wachimbaji wa Tanzanite Mererani waligundua madini hayo bila msaada wa serikali. Kwa maana nyingine walionyesha jitihada zao za uwekezaji na utafutaji ambazo ni muhimu katika ubepari au ushindani. Na serikali ya Tanzania kwenda kuwanyang'anya wananchi hawa kitu walichokivumbua ni kukiuka misingi ya ubepari.
 
Kila mara nimekuwa nasema kilichotuangusha waafrika kiuchumi na kijamii kwa asilimia 100 ni viongozi wetu. Hakuna cha siasa ya ujamaa wala ubepari. Ni RUSHWA tu, PERIOD. Hebu angalia mwaka mmoja tu tumegundua uwizi wa $130m (minimum) benki kuu. Je miaka 46 ya uhuru ni kiasi gani wameiba hawa viongozi wetu? Je fedha zote hizo zingeingia kwenye uchumi leo hii tungekuwa wapi?

Mbona nchi kama Korea, Malaysia, Singapore, nk. pamoja na ubepari wao miaka ya 60 tulikuwa tumezipita mbali sana kiuchumi? Ni nini kilitokea hadi tukakwama kama sio uwizi na kukosa kuwajibika kwa viongozi wetu?

Kwa kweli kama hawa jamaa (viongozi) wana aibu basi wangepaswa hata kujinyonga na sio kusimama mbele za watu na kutamba kwamba wametuletea maendeleo, umoja na mshikamano.

Sometimes nakubaliana na Freeman kwamba heri wakati wa mkoloni kuliko wakati wowote baada ya uhuru watanzania.

This is a good analysis. Thank you!

FMES:

Matatizo ya dunia ya nne kwa sasa tunahitaji kukaa na kureflect tunatoka wapi na tunakwenda wapi. Kama nilivyosema awali, tunaishi kwenye very hostile world ambayo its everybody for himself and GOD for us all. Ujamaa na ubepari mifumo yote naona haijatusaidia (au masharti yake yametushinda) especially waafrica, nadhani its high time tuwe INNOVATIVE kutafuta mfumo mwingine! Mimi na wewe hatujui lakini hakika tunaweza kutafuta mfumo ambao unaangalia tulikotoka na tunakotaka kwenda. Kwa sasa HATUJITAMBUI ndo maana JK akienda China ataongea ujmaa na ukomunist na Premier wa China akienda Capitol Hill kwa Bush atacheza mdundiko wa ubepari! Bila kuangalia consequences kwa wananchi wake. Kifupi we dont know what we want and worse even our Moses (JK) doesnt know! Yes he admitted that!!!

Hatuwezi kuulaumu Ubepari wala ujamaa wa kujiangalia na kujisuta ni sisi: mfano kama mmoja alivyosema, katika mwaka mmoja tumegundua 130$$M zilizoibwa na akina Balali, je kabla ya hapo waliiba ngapi? Idrisa alichukua ngapi, Mramba, Msuya, Mkapa, Sumaye and on and on....is it the fault of ubepari? I say no its our culture of corruption. na kama ulivyoandika, Ubepari masharti yake ni magumu hatuyawezi kwa hiyo tunalazimisha unworkable ideals.

In Africa from my personal views hakuna economic system ambayo imefanikiwa iwe South Africa, Nigeria or else where, because we were just coopted by our colleagues in the west (and east!) to implement things which we were/are not honest about and yet we are not prepared to say no to such policies. Whose fault is that??
 
This is a good analysis. Thank you!

FMES:

Matatizo ya dunia ya nne kwa sasa tunahitaji kukaa na kureflect tunatoka wapi na tunakwenda wapi. Kama nilivyosema awali, tunaishi kwenye very hostile world ambayo its everybody for himself and GOD for us all. Ujamaa na ubepari mifumo yote naona haijatusaidia (au masharti yake yametushinda) especially waafrica, nadhani its high time tuwe INNOVATIVE kutafuta mfumo mwingine! Mimi na wewe hatujui lakini hakika tunaweza kutafuta mfumo ambao unaangalia tulikotoka na tunakotaka kwenda. Kwa sasa HATUJITAMBUI ndo maana JK akienda China ataongea ujmaa na ukomunist na Premier wa China akienda Capitol Hill kwa Bush atacheza mdundiko wa ubepari! Bila kuangalia consequences kwa wananchi wake. Kifupi we dont know what we want and worse even our Moses (JK) doesnt know! Yes he admitted that!!!

Hatuwezi kuulaumu Ubepari wala ujamaa wa kujiangalia na kujisuta ni sisi: mfano kama mmoja alivyosema, katika mwaka mmoja tumegundua 130$$M zilizoibwa na akina Balali, je kabla ya hapo waliiba ngapi? Idrisa alichukua ngapi, Mramba, Msuya, Mkapa, Sumaye and on and on....is it the fault of ubepari? I say no its our culture of corruption. na kama ulivyoandika, Ubepari masharti yake ni magumu hatuyawezi kwa hiyo tunalazimisha unworkable ideals.

In Africa from my personal views hakuna economic system ambayo imefanikiwa iwe South Africa, Nigeria or else where, because we were just coopted by our colleagues in the west (and east!) to implement things which we were/are not honest about and yet we are not prepared to say no to such policies. Whose fault is that??

Masanja:

Suala la Afrika kuja na mfumo mpya sio jipya. Ujamaa wa Nyerere ulitoka kwenye principal za ujamaa za wanafalsafa wa Ulaya na kuingiza mazingira ya kiafrika lakini matokeo yake katuacha machizi.

Kama tunakubali usawa wa binadamu ni lazima tukubali kuwa uchumi nao una-principal zake na hizo ni principal ni universal.

Kushindwa kwetu hakutokani na ubepari au Ujamaa. Kunatokana sisi kushindwa ku-connect dots.

Ukitembelea China leo na kuona maendeleo ya vijiji vya vya ujamaa, kesho usikurupuke na kutaka watanzania nao wawe na vijiji vya ujamaa.
 
Swali ni je, hali mbaya ya wananchi wa nchi za "kibepari" afrika ni dalili ya kushindwa kwa ubepari Afrika?
Nakubaliana na; Sio kushindwa, bali upo kwenye mpito!

Viongozi wetu ndio wanatumia vibaya dhana hii ya ubepari-kwa kutumia nguvu za dola(Access rahisi kwenye mabenki nakadhalika) kwa kigezo cha kuleta haki na usawa-badala yake wanageuka na wao kuwa bourgeoise, sio mbaya lakini the wealth is not redisrtributed. Hii itaendelea mpaka pale demokrasia katika uchumi kupatikana na kuchochea zaidi demokrasia kisiasa. Inakuja taratibu.

Ubepari: Ni azma ya kuondokana umasikini kwa kufanya kazi kwa nguvu ili kukusanya utajiri(jasho lako mwenyewe) kama wa sociologist wanavyodai- ni sawa na dini, dini hii yaamini kufanya kazi kwa nguvu ili kukusanya utajiri na utajiri huu utawezesha kuleta maendeleo ya kibepari. Matajiri tunaotengeneza Afrika ni matajiri wa kutanua, wengi wao ni wa circumstances, ni viongozi wa wananchi-sio wakufanya biashara-wengi wa matajiri ambao tunawajua wanapeleka hela zao nje-wanaondoa hii capital kwetu na badala yake wanarudisha kwa waliobobea. Hapa natumia neno tajiri kumaanisha hususan, viongozi mabilionea kwa jina lingine Mabepari wa Kiafrika, wengi wao walipata bila jasho.


Viongozi wetu au mabepari nyakati hizo walikuwa wanaficha hizi hela. Hizi hela wanazozificha wangerudisha kufanya kama capital…waafrika tungwekuwa mbali, leo hii hali hiyo inabadilika….Nitatoa mfano mmoja, Mkapa na wenzake wanafanya hivi…Pamoja na kwamba wametumia nguvu ya dola hawakufikia mahali pa kuziweka huko ulaya na wao huko ulaya kula interest ya pesa ya mlalahoi, badala yake wamerudisha hizi hela kama capital tena kwa kitu kikubwa kama uzalishaji wa umeme ambayo ni moja yapo nguzo za kuleta maendeleo. Azma ya huyu mkuu ya kibepari ni nzuri. Kuna mengi yataweza kufanyika kuleta maendeleo kwa kutumia hiyo capital aliyoiweka.....

Individualism inaondoka taratibu.

Hivyo basi sio kushindwa ni mlolongo wa mpito wa kibepari hususan Ubepari Afrika:From Dictatorship to Individualism, Man-Fraud-O-Vandalism! And back to realsm. After the Individual realms play its part, then are we to succumb more onto Capitalism and hopefully state of the art Capitalism and have more of kina Mkapa, who if in great numbers might be able kuondoa hali mbaya ya mwananchi, na kufafanua zaidi ubepari wa kiafrika.

Source:International Business(Competeing in the Global Marketplace)C.W.L Hill
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom