Je wewe uko katika kundi lipi kati ya haya?

Rubi

JF-Expert Member
Oct 5, 2009
1,615
326
Wandugu tumejadili mengi sana kuhusu suala la ufisadi mpaka ikatokea baadhi ya watu kuitwa mafisadi nyangumi, papa, na vidagaa. Nia nzuri ya mijadala hii ya kifisadi ni kutaka kukomeshwa kwa vitendo vya rushwa, kupata viongozi bora na waadilifu, wasio wabinafsi na tamaa ya madaraka na wenye uzalendo na nchi yetu, kufanya kizazi kijacho kiwe ni taifa bora lenye elimu isiyo ya kughushi taifa lenye viongozi walio na uzalendo na nchi yao, elimu bora na mazingira salama ya kuishi. Kutokomeza umimi na tamaa ya kujilimbikizia mali isiyo halali.

Je kwa karne hii tunayoenda nayo ni kweli kunawezekana kutokomeza ufisadi au ndio itakuwa kila siku ufisadi kama hadithi za pwagu na pwaguzi. kama jibu ni hapana sioni mantiki ya kuendelea kujadili mijadala ya kifisadi ambayo hatuwezi kubadilisha kile kinachoonekana kuwa ni ufisadi.

Na kama jibu ni ndio tufanyaje? pengine itapidi kila mtu ajiulize kuwa anaitakia nini nchi yake? kama anitakia mema na mazuri kwa vizazi vya sasa na vijavyo afanyaje? pengine inawezekana na wewe ni mmoja wapo wa anayepinga na kupambana na ufisadi je ni ufisadi upi unaupinga?

Je kwa upande wako wewe sio fisadi?

Inawezekana na wewe ni fisadi lakini hujijui kuwa na wewe ni fisadi lakini uko mstari wa mbele kupinga ufisadi? Hivyo toa boriti kwenye jicho lako ili uone kibanzi kwenye jicho la mwenzio.

kama ni mmoja katika ufisadi jaribu kujirekebisha bado hujachelewa.

FISADI WA ELIMU
pengine ni mmoja wa unayechangia katika kulikisha mitihani ili watoto wako na wengineo wanaokupatia fedha waweze kufaulu bila kujisomea.

pengine wewe ni fataki unayechangia kuharibu watoto wa shule na wa mwezio kwa kuwadanganya kwa lifti na vijisenti na hatimaye kuwaharibia future yao wakati huohuo hujui kuwa na wa kwako nao wataharibiwa na mafataki wengine.

pengine wewe ni mmoja wao unayechangia kupatikana kwa vyeti bandia hivyo kuzidi kudumaza elimu bora inayohitajika kwa maendeleo ya taifa letu. hivyo kupelekea kuwa na madaktari feki, wahandisi feki, wanasheria feki wasiojua kulinda hata mkataba ya masilahi ya nchi yetu, walimu vihiyo, n.k wa kadhaa.

au ni mmoja wao unayewanyima watoto wako haki yao ya msingi ya kusoma hata kama una uwezo wa kuwasomesha

FISADI WA AMANI
pengine wewe ni mmoja wao unayepandikiza chuki za kidini au kikabila katika jamii hivyo kupelekea uhasama wa kidini au kukashifiana katika dini hivyo kutokea kwa uvunjifu wa amani, au kupandikiza chuki za kikabila hivyo kupelekea baadhi ya koo kuanza kupigana na kuuana kitu ambacho hakikuwa cha kawaida katika nchi yetu.

Au ni mmoja wapo unayetumia dini kuwahadaa wengine lakini moyoni mwako ni mbwa mwitu unayesubiri kurarua na kumeza

au ni mmoja wao unayetumia njia zisizo halali kujipatia mali au kwa wizi wa aina zote, udhulumaji, uongo, uhujumu uchumi wa nchi n.k kuvyo kupelekea jamii kukosa imani wanapotembea au kulala majumbani mwao kwa hofu ya kuvamiwa na majambazi, au kukosekana kwa amani makazini kati ya mabosi na wafanyakazi wao wa chini kwa kuwadhulumu haki zao, au kupelekea uchumi wa taifa kuyumba au mashirika ya umma kufa kwa ajili ya kuhujumiwa na mikataba mibovu isiyo na tija kwa taifa letu.

FISADI WA MAPENZI

pengine wewe ni mmoja wapo usiyemwaminifu katika ndoa yako hivyo kupelekea ndoa yako kuwa na migogoro isiyokwisha au ni mmoja wapo uliyechanzo cha ndoa ya mwingine kuvunjika.

au wewe ni yule uliyeingia katika mahusiano kwa sababu maalumu au kwa kufata mali alizo nazo mpenzi wako bila kuwa na mapenzi ya kweli?

au wewe ni yule unayependa kujirusha na vya uswazi au wa geti kali bila kuwa na msimamo then ukiambiwa matunda ya kujirusha unachomoa na kuhama mji au ni mmoja wa wabakaji mambo ambayo pengine hupelekea kuwa na watoto wa mitaani wengi sana au kutolewa mimba/viumbe visivyo na hatia.

FISADI WA UTU.
utu ni hali ya kibinadamu ya kumjali, kumpenda, kumthamini mwenzio kama nafsi yako yaani unavyojipenda mwenyewe. Pengine wewe ni mmoja kati ya wale wanaoingiza madawa ya kulevya na kuharibu vijana na watoto wa wenzio bila kujua kuwa tunaharibu taifa la kesho.

pengine wewe ni mmoja wao unayefanya au kushirikia kwa njia moja au nyingine katika vitendo vya kinyama i.e ngono kwa watoto wadogo, ndugu zako wa damu, ngono kwa wanyama, mauaji ya albino, na mengineyo yafananayo na hayo kwa imani za kishirikina ili kujipatia mali au manufaa yako binafsi.

Au ni mmoja wao unayependa vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike ili hali ukijua madhara ya unachowafanyajia.

Naamini ufisadi ni mwingi kwa upande mwingine lakini je wewe uko kwenye kundi lipi? je nini ufanye kwa upande wako ili pale unapopiga vita ufisadi ujue na wewe ni safi kwa manufaa ya nchi yetu, watoto wetu na vizazi vijavyo viishi katika Taifa lililo na uadilifu, lililo na na elimu bora, afya njema, usalama na uongozi bora
 
Na wewe mkubwa tuambie kwanza upo kundi lipi?
ahahahahaa ndio najichuguza ili nijue niko wapi nitoke ila nilikuwa kwenye kundi la mwoga ambao sijalitaja. sasa naona bora kuwa muwazi. ukiona kibaya kemea, ukiona kizuri sifia.
 
Ni kweli kabisa, tukijichunguza vizuri tutagundua kuwa sote tuna ka-element fulani ka ufisadi uwe ni wa mapenzi, amani, elimu, uchumi n.k tena kwa jinsi mambo yanavyokwenda hapa Bongo.,ile kuona watu wengine wanafaidi jasho la wengine kupita kiasi basi wengi wetu tuna li-element la ufisadi tena ule wa kiuchumi kama wa waheshimiwa sema tu hatujapata avenue ya kuuweka kwenye vitendo.
 
Back
Top Bottom