Je, wewe ni Mkristo au Muislamu? je, kalenda unayoitumia unaijua?

Dr Orb

Member
Aug 4, 2019
10
40
Historia kuu inayozingatiwa kuhusu hesabu za miaka ni ile yenye mlengwa wa kidini. ambapo historia hiyo inasema miaka 2019 ilianzia mwaka 1 ambapo Yesu kristo alipozaliwa kwa mujibu wa Dionysius Exiguu.

Hesabu hii haikuwa na uhakika na ilikuwa kimakadirio tu ya bwana Dionyius. Sababu kuu ya yeye kufanya hivi ilikuwa ni kwamba baada ya kifo cha Kristo si vyema kuendelea kuhesabu muda kwa kutumia mifumo ya watu waliomuua mkombozi wao (YESU KRISTO). Hivyo basi, ili kumaanisha alichokusudia ikawa ni vyema kuongeza neno A.D katika miaka, ikimaanisha Ano Domino yaani kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ikiwa na maana hii "baada ya Mkobozi (Yesu)".

kwa hivyo popote uonapo miaka na neno A.D uelewe kuwa inamaanisha ni miaka iliyotajwa baada ya Kuzaliwa Mkombozi(YESU). mfano 1222A.D, maana yake ni miaka 1222 baada ya mkombozi (Yesu). Mfumo huu ulikubaliwa na kupewa kipaumbele na dola la kirumi kwa kuwa uligusa imani ya kikristo ambayo tayari dola ya kirumi ilikuwa imeshaipokea na kuitumia kama imani rasmi.

Katika muendelezo na jitihada za kueneza na kuusambaza ukristo, Baadae miaka ya 1500 ilikuja kukubalika na kuwekwa katika mfumo wa mahesabu ya kalenda uliowekwa na Julian na Gregory(hawa ni warumi), mfumo huu ndio huu tunaoutambua mpaka sasa na upo kimkondo kwamba 2019 ni miaka baada ya kuzaliwa YESU. Mahesabu ya kalenda ya Gregoryndio yanayotajwa kuwa na usahihi mkubwa wa kimahesabu kuliko kalenda yoyote duniani.

Kwa vile mfumo wa mahesabu ya kalenda ya Gregory yana usahihi mkubwa hivyo basi yalirasmishwa duniani kama ndio mfumo maalumu wa mahesabu ya miaka na kutumiwa na jamii nyingi kama zile za kiarabu na kichina,. Uingizwaji wa mfumo wa mahesabu wa Dionyius ulileta shida hasa katika mlengwa wa kiimani hususa ni nchi zisizoamini Ukristo kama Nchi za Asia na Afrika.

Jambo hili lilipelekea vita ya kikalenda kwa kuwa sasa ulijikita kidini zaidi, ilipelekea kila jamii kujikita na kalenda yake katika mlengwa wa imani zao. vita hii ikasababisha kuwapo kwa malekebisho ya uwakilishaji wa miaka kutoka kutumia A.D mpaka B.C.E (Before Common Era). ikiwa na lengo la kupunguza makali ilihali maana bado ni ileile.

Pamoja na mabadiliko hayo lakini bado Jamii nyingi za Ulimwengu haziungu mkono mfumo huu wa Gregory kwa kuwa ni wa kidini zaidi. Jamii kama Waethiopia, Wachina, Wahindi, Waarabu na Wayahudi bado wanaupinga mfumo huu mpaka sasa na wana mifumo yao safi kabisa ya mahesabu ya kalenda ingawa bado yanafuata Mfumo wa kimahesabu wa Gregory lakini si kwa nadharia kwamba huu ni mwaka wa 2019.

Lakini pamoja na yote haya shughuli nyingi za kimataifa zinaendeshwa kwa kutumia mfumo huu wa mahesabu wa Dionyius ambao ni wa kidini zaidi. na nchi hizi zinazopinga mfumo huu hutumia zaidi kalenda zao kwa mambo ya ndani ya nchi lakini katika masualla ya kimataifa wanalazimika kutumia Mfumo huu wa Dionyius.

Hata hivyo mifumo ya kuhesabu kalenda ni migumu na inatofauti sana kati ya jamii na jamii. ikiwa utapenda kufahamu zaidi link nimeweka hapa chini kwa baadhi ya kalenda maarufu duniani.

 
Kwajina Anaitwa St. Dionysius Exiguus (Dionysius the the humble) tamka Dionisi. Kazaliwa mnamo mwaka 470 na kufariki mwaka 544 A.D, kazaliwa ukanda wa Scythia minor ambapo kwasasa ni Dobruja ipo katikati ya Romania na Burgaria. Alikua ni mtawa Cythian ambapo alikua mtaalamu wa Theology. Mwaka wa 5 alishi Rumi ambapo alijifunza namba za Roman Curia na kuzitafdiri toka kwenye Kigiriki kwenda Kilatini.
Anakumbukwa kwa kugundua Matumizi ya AD baada ya kufanya Calculations kuhusu mwaka aliozaliwa Yesu ambapo inatumika kwenye kalenda ya Gregory (Christian) na julian.

UTANGULIZI
The date of birth of Jesus of Nazareth is not stated in the gospels or in any secular text, but most scholars assume a date of birth between 6 BC and 4 BC.Two main methods have been used to estimate the year of the birth of Jesus: one based on the accounts of his birth in the gospels with reference to King Herod's reign, and another based on subtracting his stated age of "about 30 years" from the time when he began preaching (Luke 3:23) in "the fifteenth year of the preaching

Luka 3:1 Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake kaisari tiberio...
]
Kaisari Tiberio alimfuata kaisari Augusto katika utawala wa kirumi mnamo Tarehe 19/8/14 BK. Mwaka huo wa 15 wa kaisari tiberio ni kitambo toka tarehe 19/8/28 mpaka tarehe 18/8/29. Hivyo Yesu katika mwaka huo wa 15 alikua na miaka therathini

Katitka 3:23 Mwinjili luka aliandika kua Yesu alipoanza kuhubiri alikua na miaka 30 hivyo sasa mnamo karne ya 6 Dioniso alitumia tarakimu hiyo 30 kama msingi wake kua Yesu kipindi iko alikua na miaka 30.
Lakini mwinjili mwenyewe anasema umri wa Yesu ulikua kati ya miaka 30 kwahiyo mwaka aliobuni Dioniso kama mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu amepitwa miaka mitano au zaidi. Herode mkubwa aliyetaka kumwua Yesu amekufa mwaka wa nne kabla ya tarehe ya kuzaliwa Yesu iliyobuniwa na Dioniso. Kwahiyo Yesu kazaliwa kitambo kidogo kabla ya kufa herode , hivyo ukijumlisha miaka hiyo 5 na kitambo hiko kidogo twapata kama miaka 7. Kwahiyo tarehe ya kuzaliwa Yesu ni kati ya miaka 5 hadi 7 kabla ya tarehe iliyobuniwa na Dioniso. Kwaiyo inawezekana pia Yesu aiishi miaka zadi ya 33.

Source: Uzi wa member Da'Vinci
 
Historia kuu inayozingatiwa kuhusu hesabu za miaka ni ile yenye mlengwa wa kidini. ambapo historia hiyo inasema miaka 2019 ilianzia mwaka 1 ambapo Yesu kristo alipozaliwa kwa mujibu wa Dionysius Exiguu.

Hesabu hii haikuwa na uhakika na ilikuwa kimakadirio tu ya bwana Dionyius. Sababu kuu ya yeye kufanya hivi ilikuwa ni kwamba baada ya kifo cha Kristo si vyema kuendelea kuhesabu muda kwa kutumia mifumo ya watu waliomuua mkombozi wao (YESU KRISTO). Hivyo basi, ili kumaanisha alichokusudia ikawa ni vyema kuongeza neno A.D katika miaka, ikimaanisha Ano Domino yaani kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ikiwa na maana hii "baada ya Mkobozi (Yesu)".

kwa hivyo popote uonapo miaka na neno A.D uelewe kuwa inamaanisha ni miaka iliyotajwa baada ya Kuzaliwa Mkombozi(YESU). mfano 1222A.D, maana yake ni miaka 1222 baada ya mkombozi (Yesu). Mfumo huu ulikubaliwa na kupewa kipaumbele na dola la kirumi kwa kuwa uligusa imani ya kikristo ambayo tayari dola ya kirumi ilikuwa imeshaipokea na kuitumia kama imani rasmi.

Katika muendelezo na jitihada za kueneza na kuusambaza ukristo, Baadae miaka ya 1500 ilikuja kukubalika na kuwekwa katika mfumo wa mahesabu ya kalenda uliowekwa na Julian na Gregory(hawa ni warumi), mfumo huu ndio huu tunaoutambua mpaka sasa na upo kimkondo kwamba 2019 ni miaka baada ya kuzaliwa YESU. Mahesabu ya kalenda ya Gregoryndio yanayotajwa kuwa na usahihi mkubwa wa kimahesabu kuliko kalenda yoyote duniani.

Kwa vile mfumo wa mahesabu ya kalenda ya Gregory yana usahihi mkubwa hivyo basi yalirasmishwa duniani kama ndio mfumo maalumu wa mahesabu ya miaka na kutumiwa na jamii nyingi kama zile za kiarabu na kichina,. Uingizwaji wa mfumo wa mahesabu wa Dionyius ulileta shida hasa katika mlengwa wa kiimani hususa ni nchi zisizoamini Ukristo kama Nchi za Asia na Afrika.

Jambo hili lilipelekea vita ya kikalenda kwa kuwa sasa ulijikita kidini zaidi, ilipelekea kila jamii kujikita na kalenda yake katika mlengwa wa imani zao. vita hii ikasababisha kuwapo kwa malekebisho ya uwakilishaji wa miaka kutoka kutumia A.D mpaka B.C.E (Before Common Era). ikiwa na lengo la kupunguza makali ilihali maana bado ni ileile.

Pamoja na mabadiliko hayo lakini bado Jamii nyingi za Ulimwengu haziungu mkono mfumo huu wa Gregory kwa kuwa ni wa kidini zaidi. Jamii kama Waethiopia, Wachina, Wahindi, Waarabu na Wayahudi bado wanaupinga mfumo huu mpaka sasa na wana mifumo yao safi kabisa ya mahesabu ya kalenda ingawa bado yanafuata Mfumo wa kimahesabu wa Gregory lakini si kwa nadharia kwamba huu ni mwaka wa 2019.

Lakini pamoja na yote haya shughuli nyingi za kimataifa zinaendeshwa kwa kutumia mfumo huu wa mahesabu wa Dionyius ambao ni wa kidini zaidi. na nchi hizi zinazopinga mfumo huu hutumia zaidi kalenda zao kwa mambo ya ndani ya nchi lakini katika masualla ya kimataifa wanalazimika kutumia Mfumo huu wa Dionyius.

Hata hivyo mifumo ya kuhesabu kalenda ni migumu na inatofauti sana kati ya jamii na jamii. ikiwa utapenda kufahamu zaidi link nimeweka hapa chini kwa baadhi ya kalenda maarufu duniani.

Pamoja na changamoto zote , niwapongeze wale wenzetu walioamua kuwa na calendar zao ni jambo la kupongezwa sana
 
Historia kuu inayozingatiwa kuhusu hesabu za miaka ni ile yenye mlengwa wa kidini. ambapo historia hiyo inasema miaka 2019 ilianzia mwaka 1 ambapo Yesu kristo alipozaliwa kwa mujibu wa Dionysius Exiguu.

Hesabu hii haikuwa na uhakika na ilikuwa kimakadirio tu ya bwana Dionyius. Sababu kuu ya yeye kufanya hivi ilikuwa ni kwamba baada ya kifo cha Kristo si vyema kuendelea kuhesabu muda kwa kutumia mifumo ya watu waliomuua mkombozi wao (YESU KRISTO). Hivyo basi, ili kumaanisha alichokusudia ikawa ni vyema kuongeza neno A.D katika miaka, ikimaanisha Ano Domino yaani kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ikiwa na maana hii "baada ya Mkobozi (Yesu)".

kwa hivyo popote uonapo miaka na neno A.D uelewe kuwa inamaanisha ni miaka iliyotajwa baada ya Kuzaliwa Mkombozi(YESU). mfano 1222A.D, maana yake ni miaka 1222 baada ya mkombozi (Yesu). Mfumo huu ulikubaliwa na kupewa kipaumbele na dola la kirumi kwa kuwa uligusa imani ya kikristo ambayo tayari dola ya kirumi ilikuwa imeshaipokea na kuitumia kama imani rasmi.

Katika muendelezo na jitihada za kueneza na kuusambaza ukristo, Baadae miaka ya 1500 ilikuja kukubalika na kuwekwa katika mfumo wa mahesabu ya kalenda uliowekwa na Julian na Gregory(hawa ni warumi), mfumo huu ndio huu tunaoutambua mpaka sasa na upo kimkondo kwamba 2019 ni miaka baada ya kuzaliwa YESU. Mahesabu ya kalenda ya Gregoryndio yanayotajwa kuwa na usahihi mkubwa wa kimahesabu kuliko kalenda yoyote duniani.

Kwa vile mfumo wa mahesabu ya kalenda ya Gregory yana usahihi mkubwa hivyo basi yalirasmishwa duniani kama ndio mfumo maalumu wa mahesabu ya miaka na kutumiwa na jamii nyingi kama zile za kiarabu na kichina,. Uingizwaji wa mfumo wa mahesabu wa Dionyius ulileta shida hasa katika mlengwa wa kiimani hususa ni nchi zisizoamini Ukristo kama Nchi za Asia na Afrika.

Jambo hili lilipelekea vita ya kikalenda kwa kuwa sasa ulijikita kidini zaidi, ilipelekea kila jamii kujikita na kalenda yake katika mlengwa wa imani zao. vita hii ikasababisha kuwapo kwa malekebisho ya uwakilishaji wa miaka kutoka kutumia A.D mpaka B.C.E (Before Common Era). ikiwa na lengo la kupunguza makali ilihali maana bado ni ileile.

Pamoja na mabadiliko hayo lakini bado Jamii nyingi za Ulimwengu haziungu mkono mfumo huu wa Gregory kwa kuwa ni wa kidini zaidi. Jamii kama Waethiopia, Wachina, Wahindi, Waarabu na Wayahudi bado wanaupinga mfumo huu mpaka sasa na wana mifumo yao safi kabisa ya mahesabu ya kalenda ingawa bado yanafuata Mfumo wa kimahesabu wa Gregory lakini si kwa nadharia kwamba huu ni mwaka wa 2019.

Lakini pamoja na yote haya shughuli nyingi za kimataifa zinaendeshwa kwa kutumia mfumo huu wa mahesabu wa Dionyius ambao ni wa kidini zaidi. na nchi hizi zinazopinga mfumo huu hutumia zaidi kalenda zao kwa mambo ya ndani ya nchi lakini katika masualla ya kimataifa wanalazimika kutumia Mfumo huu wa Dionyius.

Hata hivyo mifumo ya kuhesabu kalenda ni migumu na inatofauti sana kati ya jamii na jamii. ikiwa utapenda kufahamu zaidi link nimeweka hapa chini kwa baadhi ya kalenda maarufu duniani.

Is it a big deal
 
Mababu zetu afrika walikuwa na kalenda ipi?
Waafrika tulikuwa na mifumo na miongozo ming ya maisha ambayo yalijitosheleza, kwa upande wa kalenda tulitumia mfumo ujulikanao kama ZODIAC system. Huu ulikuwa ni mfumo wa kwanza wa mwanadamu kutambua nyakati lakin pia kutambua mamb mengine mengi ya kimaisha.
 
Sisi kalenda yetu tungeitengeneza tangu tulipopata uhuru natungeenda miezi 12 kwasiku 30 kila mwezi
 
Mababu zetu afrika walikuwa na kalenda ipi?
Walikuwa na kalenda yao ya kuhesabu vipindi vya mvua na joto , sherehe zao n.k , walijitosheleza kwenye hilo ( nyota na mwezi zilikuwepo ) , unauliza maswali gani !!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom