GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,518
- 108,793
1. Je, wale 'Washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua kuwa aliyeshindwa huko BET siyo tu Msanii Diamond Platinumz pekee bali hata Watanzania wote tumeshindwa?
2. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua kuwa Kitendo cha Diamond Platinumz Kuikosa hii Tuzo ya BET kuna Fursa kadha wa kadha Tanzania inaenda Kuzikosa?
3. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua kuwa Kitendo cbetu cha Kiswahili na Uswahili wetu wa Kumshambulia ( Kumsagia Kunguni ) Diamond Platinumz huko nje ( katika Mataifa mengine ) kimetufanya tuonekane ni Wapumbavu wakubwa?
4. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tulijiongeza kabla ili kujua kuwa 'Music Industry' ya Tanzania ambayo pia ingechochea Ajira kwa Watanzania ingefanikiwa zaidi kama Msanii Diamond Platinumz angefanya vyema katika Tuzo za BET?
5. Je, wale 'washadadiaji'wa Mitandaoni tunajua kuwa katika hili la Kumuunga mkono Msanii wetu Diamond Platinumz tulipaswa tuweke pembeni Chuki zetu nae kwa muda ili afanikiwe na atungarishe vyema Watanzania Kimataifa na huenda angekuwa pia ni Kivutio kikubwa cha Wageni ambao wangemiminika Tanzania na hata Kukuza Uchumi wetu kwa namna moja au nyingine?
6. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua ya kwamba pamoja na Roho Mbaya zetu 'zilizotukuka' za Kumchafua na Kumfitinisha Msanii wetu Diamond Platinumz bado Yeye ( Nasib Abdul ) anaendelea kubakia Bilionea na Utajiri wake huku Sisi Umasikini wetu na Shida zetu za Kimaisha zikizidi tu Kulundikana kama si Kujilimbikiza kwa Baraka zake Shetani ambaye muda mwingine huwa anatushangaa Watanzania?
7. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni mna habari kuwa hata huyu Msanii Mshindi wa hizi Tuzo za BET nae huko nchini Kwake anasakamwa mno na Watesi ( Critics ) wake hadi Kupigwa 'Madongo' ila katika Kipindi cha Kumpigia Kura huko waliweka tofauti zao pembeni na hata huko ( humu ) Mitandaoni walihakikisha hawamchafui ili Mataifa mengine tujue 'Mapungufu' yake?
Nami GENTAMYCINE namalizia kwa kusema ya kwamba ifike muda Watanzania tuacheni kuwa Washsmba na wenye Roho za Kishetani na Kichawi kama tulizozionyesha katika Kumchafua na Kumfitinisha Msanii Nasib Abdul ( Diamond Platinumz ) na tutambue kuwa Kitendo tulichokifanya ni cha Kipopoma ( Kipumbavu ) mno na tusikirudie tena kwa Msanii mwingine hata kama ni mwana CCM au mwana CHADEMA au ni 'Pro Government' pia.
Kama mpenda Burudani nimeumia mno.
2. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua kuwa Kitendo cha Diamond Platinumz Kuikosa hii Tuzo ya BET kuna Fursa kadha wa kadha Tanzania inaenda Kuzikosa?
3. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua kuwa Kitendo cbetu cha Kiswahili na Uswahili wetu wa Kumshambulia ( Kumsagia Kunguni ) Diamond Platinumz huko nje ( katika Mataifa mengine ) kimetufanya tuonekane ni Wapumbavu wakubwa?
4. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tulijiongeza kabla ili kujua kuwa 'Music Industry' ya Tanzania ambayo pia ingechochea Ajira kwa Watanzania ingefanikiwa zaidi kama Msanii Diamond Platinumz angefanya vyema katika Tuzo za BET?
5. Je, wale 'washadadiaji'wa Mitandaoni tunajua kuwa katika hili la Kumuunga mkono Msanii wetu Diamond Platinumz tulipaswa tuweke pembeni Chuki zetu nae kwa muda ili afanikiwe na atungarishe vyema Watanzania Kimataifa na huenda angekuwa pia ni Kivutio kikubwa cha Wageni ambao wangemiminika Tanzania na hata Kukuza Uchumi wetu kwa namna moja au nyingine?
6. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni tunajua ya kwamba pamoja na Roho Mbaya zetu 'zilizotukuka' za Kumchafua na Kumfitinisha Msanii wetu Diamond Platinumz bado Yeye ( Nasib Abdul ) anaendelea kubakia Bilionea na Utajiri wake huku Sisi Umasikini wetu na Shida zetu za Kimaisha zikizidi tu Kulundikana kama si Kujilimbikiza kwa Baraka zake Shetani ambaye muda mwingine huwa anatushangaa Watanzania?
7. Je, wale 'washadadiaji' wa Mitandaoni mna habari kuwa hata huyu Msanii Mshindi wa hizi Tuzo za BET nae huko nchini Kwake anasakamwa mno na Watesi ( Critics ) wake hadi Kupigwa 'Madongo' ila katika Kipindi cha Kumpigia Kura huko waliweka tofauti zao pembeni na hata huko ( humu ) Mitandaoni walihakikisha hawamchafui ili Mataifa mengine tujue 'Mapungufu' yake?
Nami GENTAMYCINE namalizia kwa kusema ya kwamba ifike muda Watanzania tuacheni kuwa Washsmba na wenye Roho za Kishetani na Kichawi kama tulizozionyesha katika Kumchafua na Kumfitinisha Msanii Nasib Abdul ( Diamond Platinumz ) na tutambue kuwa Kitendo tulichokifanya ni cha Kipopoma ( Kipumbavu ) mno na tusikirudie tena kwa Msanii mwingine hata kama ni mwana CCM au mwana CHADEMA au ni 'Pro Government' pia.
Kama mpenda Burudani nimeumia mno.