SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Kila ninaposikiliza redio au kutazama TV nshtushwa mtamshi yasiyo sahihi ya baadhi ya maneno. Tatizo hili wengi mtasema linatokana na lugha asili za watangazaji hao lakini kwa upande wangu naona kama tatizo lipo zaidi kwa watangazaji hao kuwa wavivu wa kujisahihisha. Sijapata kwa mfano, kumsikia mtangazaji akitamka sahihi neno 'malaria'. Mara nyingi nimesikia ' marelia' Kama huyu mtangazaji anaweza kutamka 'r' na 'l' sawasawa , kwa nini anashindwa kuweka 'r' mahali pake na 'l' mahali pake?. Kwa hiyo kwenye sentenso 'Mgonjwa wa malaria amepanda lori' utasikia 'Mgonjwa wa marelia amepanda roli' Kwanini watangazaji wanakuwa wavivu kiasi hiki? Inaudhi sana! Hasa wa Star TV.