Je, wanasiasa kutembelea sana Wanasiasa Wastaafu ni Utaratibu tu au nchi imewashinda na Majukumu ni mazito kuliko walivyotarajia?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Nahisi Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar sasa Viti ni vya Moto na imebidi Wanasiasa wa Zanzibar na Kigoma tubuni Mbinu, tugawane Majukumu na kuamzisha Utaratibu wa ghafla wa Kuwatembelea Wastaafu waliotutangulia tulipo sasa maeneo ya Masaki.

Tumeingia Machi na sasa ni Novemba tayari tunaenda Kuwatembelea Wastaafu mara Kumi Kumi sijajua mpaka mwaka 2025 tutakuwa tumewatembelea mara ngapi na huenda hata Wao oia wakatuchoka Sisi Wanasiasa wa saaa anbao wengi Wetu tulijitapa kabisa kuwa Tanzania tunaiweza na tuna Uzoefu nayo kuanzia Zanzibar mpaka Kigoma ila imekuwa ni tofauti.

Kuna uwezekano pia Wanasiasa wa Zanzibar na Kigoma wakikinaiwa na Wastaafu kwa Kuwatembelea Kwao Kutwa au kwa Kuwashtukiza wakaanza sasa Utaratibu wa Kutembelea na Makaburi yote ya Wastaafu Waandamizi na ikiwezekana hata Kuyatambikia Makaburi yao ili Tanzania isonge mbele kwa msaada wa Mizimu yao ambayo imeshakasirika kwa Wanasiasa wa leo kwenda Kinyume na walivyokuwa wanefanya wao.

Chamwino na Magogoni hakulaliki.
 
Back
Top Bottom