Je, wanaodai katiba mpya hawaoni kero ya umeme na maji kwa wananchi?

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Apr 19, 2021
1,502
4,408
Ningekuwa ni mpinzani wa kweli ningesema kweli daima kwamba wananchi hawahitaji katiba mpya sasa zaidi ya wanavyohitaji maji, umeme na huduma bora za afya na elimu.

Nikiwa kama mpigakura sihitaji mgombea anipe ahadi ya katiba mpya sasa, nitahitaji aniambie ni namna gani atapambana na hali yangu ya ukosefu wa ajira, nitahitaji aniambie ni fursa zipi nitazipata kutokana na bomba la mafuta au mradi wa gesi ya mtwara.

Umefika wakati muafaka wanasiasa kuangalia vipaumbele vya wananchi wao kuliko matumbo yao. Katiba mpya ni muhimu lakini sio sasa ambapo nchi inahitaji kujenga uchumi ulioathiriwa na Corona. Nchi inahitaji kutatua tatizo la ajira.

Licha ya mengi wananchi wanayopitia, Je suala la katiba mpya sasa si ni dhihaka? Kwa sasa hekima ya hali ya juu inahitajika hususani kwa mambo yanayohusu maisha ya watu ambayo hata wanaodai katiba mpya hawawezi kusema katiba mpya ni miongoni kama wakihitajika kufanya hivyo.
 
Tatizo la Paka wa Lumumba mkikaririrshwa huko huwa mnakuja kumwaga uharo wanu humu bila kufirkiria!
 
Ile tu kutegemea wengine wakupe ahadi ya maji, umeme n.k ni kielelezo muhimu kuwa Katiba Mpya inahitajika kwa haraka sana!
Jiulize hizo ahadi ushapewa ngapi? Mara ngapi? Je, hadi sasa utekelezaji wake ukoje? Hao wanao kupa ahadi wasipotekeleza unawachukulia hatua gani??
 
Ungejua nini maana ya Katiba wala usingeandika huu upuuzi wako!
Katiba ni sheria mama au sheria kuu. Katiba mpya haitamhakikishia mwananchi upatikanaji wa maji au umeme hivyo wananchi tunaona hamna umuhimu huo sasa.
 
... kwanini kuna kero ya umeme na maji kwa wananchi? Ni kwa sababu hizi;

Katiba ya sasa imeacha mianya ya kupata viongozi wasio na uwezo wa kupanga vipaumbele na rasilimali za taifa - mambo ya teuzi kwa kujuana au uchama.

Katiba ya sasa imeacha mianya ya kuwalinda viongozi mafisadi; kile ambacho kingeenda kuboresha maisha ya wananchi including maji na umeme kinaishia matumboni mwa walafi wachache halafu wananchi hawana cha kuwafanya.

Kwa hayo machache unaweza kuona jinsi Katiba bora ilivyo muhimu kwa maendeleo na ustawi wa wananchi na taifa kwa ujumla. Hata kama haibebi ugali mkononi kukuletea mezani kama wajinga wachache wanavyopotosha, ikiweka mifumo bora ni suluhisho la matatizo ya nchi hii kwa sehemu kubwa.

By the way, kwani nchi hii imewahi kukumbwa na tatizo la Corona?
 
Katiba ni sheria mama au sheria kuu. Katiba mpya haitamhakikishia mwananchi upatikanaji wa maji au umeme hivyo wananchi tunaona hamna umuhimu huo sasa.
Sheria mama inaweka madaraka mikononi mwa wananchi. Hivyo Katiba inapaswa kuweka misingi ya kuwajibishana. Katiba inapaswa kuondoa tabaka la wanyonge na wanyongaji (watawala).
Maji, umeme na huduma nyingine muhimu za kijamii hazitakiwi kuwa ahadi. Hizo ni haki za raia.
#Pevuka
 
... kwanini kuna kero ya umeme na maji kwa wananchi? Ni kwa sababu hizi;

Katiba ya sasa imeacha mianya ya kupata viongozi wasio na uwezo wa kupanga vipaumbele na rasilimali za taifa - mambo ya teuzi kwa kujuana au uchama.

Katiba ya sasa imeacha mianya ya kuwalinda viongozi mafisadi; kile ambacho kingeenda kuboresha maisha ya wananchi including maji na umeme kinaishia matumboni mwa walafi wachache halafu wananchi hawana cha kuwafanya.

Kwa hayo machache unaweza kuona jinsi Katiba bora ilivyo muhimu kwa maendeleo na ustawi wa wananchi na taifa kwa ujumla. Hata kama haibebi ugali mkononi kukuletea mezani kama wajinga wachache wanavyopotosha, ikiweka mifumo bora ni suluhisho la matatizo ya nchi hii kwa sehemu kubwa.

By the way, kwani nchi hii imewahi kukumbwa na tatizo la Corona?
Marekebisho yanayofanyika Mara kwa Mara ya katiba ya sasa ni kuifanya iendane na wakati. Kama tunahitaji kubadili katiba nzima kwa baadhi ya vipengele kupitwa na wakati je tutahitaji tena katiba mpya miaka 50 ijayo?
 
Ningekuwa ni mpinzani wa kweli ningesema kweli daima kwamba wananchi hawahitaji katiba mpya sasa zaidi ya wanavyohitaji maji, umeme na huduma bora za afya na elimu.

Nikiwa kama mpigakura sihitaji mgombea anipe ahadi ya katiba mpya sasa, nitahitaji aniambie ni namna gani atapambana na hali yangu ya ukosefu wa ajira, nitahitaji aniambie ni fursa zipi nitazipata kutokana na bomba la mafuta au mradi wa gesi ya mtwara.

Umefika wakati muafaka wanasiasa kuangalia vipaumbele vya wananchi wao kuliko matumbo yao. Katiba mpya ni muhimu lakini sio sasa ambapo nchi inahitaji kujenga uchumi ulioathiriwa na Corona. Nchi inahitaji kutatua tatizo la ajira.

Licha ya mengi wananchi wanayopitia, Je suala la katiba mpya sasa si ni dhihaka? Kwa sasa hekima ya hali ya juu inahitajika hususani kwa mambo yanayohusu maisha ya watu ambayo hata wanaodai katiba mpya hawawezi kusema katiba mpya ni miongoni kama wakihitajika kufanya hivyo.
Mpuuzi wewe bila kuwa na mifumo wa kuwajibika maendeleo utaendelea kuyaona kwenye TV
 
La kutumikia
Katiba ni sheria mama au sheria kuu. Katiba mpya haitamhakikishia mwananchi upatikanaji wa maji au umeme hivyo wananchi tunaona hamna umuhimu huo sasa.
Ujinga ni shida sana...
Makalio Yako acha yakufanyie kazi yaliuopewa usiyapew kazi kufikiri!
 
kuitafuta katiba mpya kinaathiri vp kupatikana kwa maji na umeme vijijini
 
Sheria mama inaweka madaraka mikononi mwa wananchi. Na inapaswa kuweka misingi ya kuwajibishana.
Maji, umeme na huduma nyingine muhimu za kijamii hazitakiwi kuwa ahadi. Hizo ni haki za raia.
#PevukaHakKKa
Uwajibikaji unakuja na usimamizi mzuri hata katiba ya sasa ina misingi yote labda kilichokosekana ni usimamizi mzuri. Mfumo(katiba) na usimamizi( mtu) vinatakiwa viende sambamba
 
Back
Top Bottom