Je, wananchi wanayo mamlaka haya kweli? au ni changa la macho tu!!

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Jamani watanzania wenzangu sidhani kuna asiyefahamu kwamba katiba hii tunayoendelea kuitumia si mali ya serikali au ya bunge au ya mahakam au ya wanasheria au wanasiasa, au ya wanaharakati au ya vitu mfano wa hivyo, hapana!

Katiba hii ya mwka 1977 ni mali ya wananchi wanaounda jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mantiki hii wao ndio wenye mali hiyo (katiba) japokuwa wametapakaa sehemu mbalimbali, mjini na mavueni. Wakulima, wafanyakazi, wafanyabiasha, wajasiliamali, wavuvi. wachimbaji wadogo wadogo nk.
Leo narudia kuwakumbusha kuwa; nyinyi wananchi ndiyo wenye katiba hii, japo iwe nzuri au mbaya.

Ni kwa sababu hiyo sasa, naomba mrejee pamoja nami katika sura ya kwanza, ibara ya 8 ibara ndogo ya (1) kipengere (b) cha katiba yetu hii ambacho kinasema hivi, nanukuu.

"Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wanachi kwa mujibu wa katiba hii"

Hebu tujaribu kutafakari polepole.

Kwamba wananchi sisi ndio msingi wa mamlaka yote! Na tena eti kwamba serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa katiba hiyo.

Yaani kwa rugha nyepesi ni kwamba; sisi wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho kuhusu mamlaka, kwamba yupi tunampa mamlaka na yupi hatumpi mamlaka.

Ni hii inabainisha wazi kuwa ni sisi wananchi wenye maamuzi juu ya chama kipi kiunde serikali na kipi kiwe cha upinzani.
Ni sisi laia na wala si taasisi yoyote yenye mamlaka hiyo!

Vyombo vyote vya ulinzi na usalama, vilivyopokea mamlaka yao kutoka kwa wananchi, kwa mujibu wa katiba hii, vinapaswa kulisimamia, kulinda, na kutetea mamlaka ya wananchi.

SASA SWALI LANGU NI HILI.

Je kwa hali ilivyo hapa kwetu, wananchi wanayo mamlaka haya kweli?

Kwa mfano.
Mwaka 2020 endapo wananchi, kwa mamlaka waliyonayo kwa mujibu wa kifungu hicho juu watataka kukiondoa chama tawala madarakani; wakati huo huo bila kusahau mazingira ya chaguzi zilizopita, je wanayo hayo mamlaka ya kukinyang'anya chama hicho mamlaka waliyokipa?

Je katiba kweli katiba hii imeweka mazingira ya kutumika mamlaka na uwezo huu wa wananchi? au hili ni bado ni changa la macho tu!

Karibuni
 
Jamani watanzania wenzangu sidhani kuna asiyefahamu kwamba katiba hii tunayoendelea kuitumia si mali ya serikali au ya bunge au ya mahakam au ya wanasheria au wanasiasa, au ya wanaharakati au ya vitu mfano wa hivyo, hapana!

Katiba hii ya mwka 1977 ni mali ya wananchi wanaounda jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mantiki hii wao ndio wenye mali hiyo (katiba) japokuwa wametapakaa sehemu mbalimbali, mjini na mavueni. Wakulima, wafanyakazi, wafanyabiasha, wajasiliamali, wavuvi. wachimbaji wadogo wadogo nk.
Leo narudia kuwakumbusha kuwa; nyinyi wananchi ndiyo wenye katiba hii, japo iwe nzuri au mbaya.

Ni kwa sababu hiyo sasa, naomba mrejee pamoja nami katika sura ya kwanza, ibara ya 8 ibara ndogo ya (1) kipengere (b) cha katiba yetu hii ambacho kinasema hivi, nanukuu.

"Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wanachi kwa mujibu wa katiba hii"

Hebu tujaribu kutafakari polepole.

Kwamba wananchi sisi ndio msingi wa mamlaka yote! Na tena eti kwamba serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa katiba hiyo.

Yaani kwa rugha nyepesi ni kwamba; sisi wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho kuhusu mamlaka, kwamba yupi tunampa mamlaka na yupi hatumpi mamlaka.

Ni hii inabainisha wazi kuwa ni sisi wananchi wenye maamuzi juu ya chama kipi kiunde serikali na kipi kiwe cha upinzani.
Ni sisi laia na wala si taasisi yoyote yenye mamlaka hiyo!

Vyombo vyote vya ulinzi na usalama, vilivyopokea mamlaka yao kutoka kwa wananchi, kwa mujibu wa katiba hii, vinapaswa kulisimamia, kulinda, na kutetea mamlaka ya wananchi.

SASA SWALI LANGU NI HILI.

Je kwa hali ilivyo hapa kwetu, wananchi wanayo mamlaka haya kweli?

Kwa mfano.
Mwaka 2020 endapo wananchi, kwa mamlaka waliyonayo kwa mujibu wa kifungu hicho juu watataka kukiondoa chama tawala madarakani; wakati huo huo bila kusahau mazingira ya chaguzi zilizopita, je wanayo hayo mamlaka ya kukinyang'anya chama hicho mamlaka waliyokipa?

Je katiba kweli katiba hii imeweka mazingira ya kutumika mamlaka na uwezo huu wa wananchi? au hili ni bado ni changa la macho tu!

Karibuni
Mamlaka hayo yaliyo ainishwwa katika katiba wananchi walisha yatekeleza kwa kuiweka madarakani serikali iliyopo na si vinginevyo.
 
Mamlaka hayo yaliyo ainishwwa katika katiba wananchi walisha yatekeleza kwa kuiweka madarakani serikali iliyopo na si vinginevyo.
Kkimondoa, jaribu kuelewa swali.

Swali ni kwamba; Wananchi, wakitaka kukiondoa chama tawala madarakani, bila kujali ni ccm au ni cuf, je katiba hiyo-hiyo imejenga mazingira mazuri yatakayowafanya wawe na uwezo wa kutumia mamlaka waliyonayo kikatiba?
 
Kkimondoa, jaribu kuelewa swali.

Swali ni kwamba; Wananchi, wakitaka kukiondoa chama tawala madarakani, bila kujali ni ccm au ni cuf, je katiba hiyo-hiyo imejenga mazingira mazuri yatakayowafanya wawe na uwezo wa kutumia mamlaka waliyonayo kikatiba?
Nimekuelewa vyema sana na nina kujibu kwa mujibu wa namna katiba yetu inavyo tekelezeka katika kifungu hicho,

Mamlaka ya kuiondoa ccm madarakan wananchi wamepewa kwa mujibu wa kifungu hicho na wana kitekeleza kifungu hicho kila baada ya miaka mitano tatizo ni kifungu kingine cha katiba hiyo hiyo ambacho kinahusiana na tume ya uchaguzi na mamlaka zake na uhusiano wake na serikali

Lakin kipengere hicho ulicho leta mkuu kinatekelezwa sana kupitia sanduku la kura kila baada ya miaka mitano ndio maana vyama vyote hushiriki na husimamisha wagombea kwa ngazi zote na wananchi ndio wanao fanya maamuzi nani atoke nani abaki kwa njia ya kidemokrasia na huo ndio utekelezaji wenyewe wa kifungu hicho ,na wala sio kwenda kuwafukuza Ccm ikulu kwa mapanga na mashoka.
 
Yaani kwa rugha nyepesi ni kwamba; sisi wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho kuhusu mamlaka, kwamba yupi tunampa mamlaka na yupi hatumpi mamlaka.


Mamlaka wanapeana wao, kumbuka kilisemwa nini wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa flyover ya ubungo hivi karibuni... sitaki kunukuu
 
Nimekuelewa vyema sana na nina kujibu kwa mujibu wa namna katiba yetu inavyo tekelezeka katika kifungu hicho,

Mamlaka ya kuiondoa ccm madarakan wananchi wamepewa kwa mujibu wa kifungu hicho na wana kitekeleza kifungu hicho kila baada ya miaka mitano tatizo ni kifungu kingine cha katiba hiyo hiyo ambacho kinahusiana na tume ya uchaguzi na mamlaka zake na uhusiano wake na serikali

Lakin kipengere hicho ulicho leta mkuu kinatekelezwa sana kupitia sanduku la kura kila baada ya miaka mitano ndio maana vyama vyote hushiriki na husimamisha wagombea kwa ngazi zote na wananchi ndio wanao fanya maamuzi nani atoke nani abaki kwa njia ya kidemokrasia na huo ndio utekelezaji wenyewe wa kifungu hicho ,na wala sio kwenda kuwafukuza Ccm ikulu kwa mapanga na mashoka.
Kwa hiyo unakiri kuwa kuna kifungu kingine kinachoweka kauzibe fulani kwa wananchi pindi wanapotaka kutumia mamlaka yao kwa mujibu wa katiba.
Hivi ni kusema kwamba katiba yetu hii inatoa mamlaka kwa wananchi kwa mkono wa kushoto na kuwapokonya kwa mkono wa kulia!
 
Kwa hiyo unakiri kuwa kuna kifungu kingine kinachoweka kauzibe fulani kwa wananchi pindi wanapotaka kutumia mamlaka yao kwa mujibu wa katiba.
Hivi ni kusema kwamba katiba yetu hii inatoa mamlaka kwa wananchi kwa mkono wa kushoto na kuwapokonya kwa mkono wa kulia!
Wananchi wenyewe wanatekeleza matakwa ya katiba kama inavyo takiwa swala la mapungufu ya katiba kuhusu tume ya uchaguzi hilo ni swala lingine mkuu lakin kipengere hicho nimekijibu kulingana na swali lako
 
Jamani watanzania wenzangu sidhani kuna asiyefahamu kwamba katiba hii tunayoendelea kuitumia si mali ya serikali au ya bunge au ya mahakam au ya wanasheria au wanasiasa, au ya wanaharakati au ya vitu mfano wa hivyo, hapana!

Katiba hii ya mwka 1977 ni mali ya wananchi wanaounda jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mantiki hii wao ndio wenye mali hiyo (katiba) japokuwa wametapakaa sehemu mbalimbali, mjini na mavueni. Wakulima, wafanyakazi, wafanyabiasha, wajasiliamali, wavuvi. wachimbaji wadogo wadogo nk.
Leo narudia kuwakumbusha kuwa; nyinyi wananchi ndiyo wenye katiba hii, japo iwe nzuri au mbaya.

Ni kwa sababu hiyo sasa, naomba mrejee pamoja nami katika sura ya kwanza, ibara ya 8 ibara ndogo ya (1) kipengere (b) cha katiba yetu hii ambacho kinasema hivi, nanukuu.

"Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wanachi kwa mujibu wa katiba hii"

Hebu tujaribu kutafakari polepole.

Kwamba wananchi sisi ndio msingi wa mamlaka yote! Na tena eti kwamba serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa katiba hiyo.

Yaani kwa rugha nyepesi ni kwamba; sisi wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho kuhusu mamlaka, kwamba yupi tunampa mamlaka na yupi hatumpi mamlaka.

Ni hii inabainisha wazi kuwa ni sisi wananchi wenye maamuzi juu ya chama kipi kiunde serikali na kipi kiwe cha upinzani.
Ni sisi laia na wala si taasisi yoyote yenye mamlaka hiyo!

Vyombo vyote vya ulinzi na usalama, vilivyopokea mamlaka yao kutoka kwa wananchi, kwa mujibu wa katiba hii, vinapaswa kulisimamia, kulinda, na kutetea mamlaka ya wananchi.

SASA SWALI LANGU NI HILI.

Je kwa hali ilivyo hapa kwetu, wananchi wanayo mamlaka haya kweli?

Kwa mfano.
Mwaka 2020 endapo wananchi, kwa mamlaka waliyonayo kwa mujibu wa kifungu hicho juu watataka kukiondoa chama tawala madarakani; wakati huo huo bila kusahau mazingira ya chaguzi zilizopita, je wanayo hayo mamlaka ya kukinyang'anya chama hicho mamlaka waliyokipa?

Je katiba kweli katiba hii imeweka mazingira ya kutumika mamlaka na uwezo huu wa wananchi? au hili ni bado ni changa la macho tu!

Karibuni
Mkuu: hoja yako ni nzuri ila umesahau kitu kimoja. Mamlaka huenda na WAJIBU na hutumika kwa kuzingatia TARARATIBU. Kubadilisha serkali au "kukitoa" chama tawala si kszi ndogo kama kubadilisha viatu na soksi, ni lazima nchi iwe na vitu vya kudumu (TRA, BoT, Polisi, Baraza la Maaskofu, NBAA, Magereza, JWTZ, nk). Huwezi kuvifuta na kuvianzisha hivihivi. Hii ndiyo shida yako, unsfikiri ni maskhara.

Ungekumbuka haya wala usingeumiza kichwa chako, pale pale ungeelewa kuwa "wananchi" si kitu kimoja, ni watu milioni 50. Ili uwe na kitu hadi ukiite MATASHI YA WANANCHI, itabidi upigishe kura, watakaoshinda ndiyo watayekeleza MATAKWA yao.

Unataka CCM itoke? No problem, jenga hoja kwa wananchi; wakikuelewa CCM itatoka automatically mara utakapopata ridhaa yao kwa kura. CUF wanataka kuvunja Muungano ili tuwe na EU ya mkataba - bado wanajitaheed lakini kura hazijatosha. CHADEMA walitaka dola ya familia moja, baadaye wakataka kabila moja, baadaye wakataka ya kanda moja; bafo wanajitaheed lakini kura hazijatosha. Ni kujebga hoja tu.

Kosa jingine unafanya ni kuiomba CCM ikusaidie kuitoa madarakani. Unataka Kamati ya Warioba kiulaini tu ituletee serkali 3 mezani huku wapiga kura walishasema tangu 1964 wanataka serkali mbili kwa kukipa ushindi CCM yenye sera hiyo na kuikataa NCCR Mageuzi yenye sera ya serkali 3.

Naam, madaraka yote yako kwa wananchi, wanachotaka lazima kifanyike. Kwa hivi sasa wanataka CCM.
 
Back
Top Bottom