Je wanadamu tuna FREE WILL??

Free will tunazo ila hakuna kiumbe kisicho na fomula ,kwamba ukistep nje ya fomula utapata madhara.
Ila pia tuko controled kwa kiasi fulani tangu kuzaliwa kwetu..
Ndio maana kila kitu kina negative na positive.. kila kitu kina kinyume

Ila yale matukio ya zama huwaga yameshaandaliwa katika mfumo huo huo wa + -
Kwahiyo kila litokealo kama sio matokeo hasi basi matokeo chanya.

kwa mfano yuda asingemsaliti angetokea mwingine kwasababu yupo mtu wa aina ya yuda siku zote ,na yeye angali ametumia free will kujitoa katika dhambi.. lakini lile tukio la usaliti liko pale pale... ndio maana katika bible wanasema "ili litimie neno lililonenwa na manabii" kwamba matukio tayari yapo controlled kama Unavyoona Ratiba ya harusi nk ila je nani atayakamilisha ndio inapokuja hio "FREE WILL"
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Free will tunazo ila hakuna kiumbe kisicho na fomula ,kwamba ukistep nje ya fomula utapata madhara.
Ila pia tuko controled kwa kiasi fulani tangu kuzaliwa kwetu..

So nikawaida kabisa
Tuko controlled na nani mkuu?
 
Hakuna kitu inaitwa freewill,always kuna causality somewhere!

Hii Freewill ya kwenye bible ni pure lie na myth tu.

Mwanangu Sam Harris ka-debunk it left and right!

See him here:

Kama hatuna free will basi huu uzi umeujibu kwa kushurutishwa?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Kama hatuna free will basi huu uzi umeujibu kwa kushurutishwa?

Mkuu

Umemsikiliza Sam Harris hapo mkuu?

Ni kwamba mpaka nimeingia humu kujibu hii post yako inajumlisha countless of causers ambazo ni seen and unseen internal and external...mpaka ubongo wangu unakubali kuchapa keyboard yangu hapa kukujibu ni baada ya minyukano ya causes chungu nzima,zilizokua powerful zimeshinda ndio maana nikachapa keyboard hapa..

Msikilize Sam Harris hapo,Free Will imekua debunked kushoto kulia!
 
Mkuu ukisoma Mwanzo 3 yote utaona ni tamaa na uzembe wa binadamu wenyewe tuu kwani Adamu alishaambiwa asile hilo tunda hata kabla ya Hawa kuumbwa toka ubavuni mwake. Soma Mwanzo 2:16-17 "Mwenyezi-Mungu alimwamuru mwanaume huyo, waweza kula matunda ya mti wowote katika bustani lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema usile, maana siku utakapokula matunda ya mti huo hakika utakufa"
Kwa hiyo kwa mujibu wa huo mstari hapo Adamu alikua keshaonywa hata kabla ya kuumbwa kwa Hawa.

Sasa mkuu nani mjinga? nani mwenye makosa? Mungu au Adamu?
...Adamu ndie mwenye makosa kwa sababu hakutii amri ya Mungu badala yake alisikiliza alichoambiwa na Hawa. Soma Mwanzo 3:11-12 "Mwenyezi-Mungu akamwuliza nani aliyekuambia uko uchi? Je umekula tunda la mti nililokuamuru usile? Huyo mwanaume akajibu mwanamke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la mti huo nami nikala"

Sasa mkuu unaanzaje kumlaumu Mungu wakati ni makosa ya Adamu? Tena Adamu ndie mpuuzi kwa sababu alimsikiliza mwanamke badala ya kumsikiliza Mungu wake, so mwanamke kwake alikua ni zaidi ya Mungu! dharau ilioje????

Na uzuri Hawa nae alikua anajua matunda ya mti fulani Mungu kakataza yasiliwe soma Mwanzo 3:2-3

Sasa mkuu kwa kifupi tuko hapa tulipo sababu ya uasi wa binadamu toka mwanzo!
Haya yote yanayotokea hayana budi kutokea. Mungu ni mwema siku zote, binadamu sababu ya tamaa zetu na kutoshika maandiko ndivyo vinatuponza. Ni lazima tujue uwepo wa Mungu, watu wengi wasiposhuhudia matendo makuu ya Mungu huwa hawaamini kwamba Mungu yupo.

Yes bado anatupenda ndio maana alimtoa mwanae wa pekee/Yesu aje kutukomboa lakini pamoja na yote hayo hamna kitu bado binadamu wanazidi kuasi. Soma vitabu vya Daniel na Ufunuo ujue hatma ya huu ulimwengu. Na ni lazima unabii utimie hata Yesu alikuja kutimiza unabii na kutukomboa toka kifungoni mwa shetani.


Nawashangaa sana watu mnaokaa hapa na kuanza kumshushia lawama Mungu wakati ni matokeo ya uasi wetu toka mwanzo.
Huu ndio ukweli.
Hata wanaotengeneza vyombo vya kutumia kama mashine au magari, kuna menu za vyombo hivyo, jinsi ya kuvitumia na kuvitunza.
Binadamu pia ana menu yake inayomwelekeza jinsi ya kujitumia na kuishi.
Mungu kupitia maandiko matakatifu ameeleza kila kitu kuhusu Binadamu aliye muumba, aishi vipi na jirani, ale nini, avae nini, afanye nini, asifanye nini ili aishi vizuri na kujitunza afya yake imavyopasika.
Mambo hayo yako wazi kabisa kwa mfano imeandikwa, usiue, usizini, mpende jirani yako, usiibe, NK.
Sasa wewe unazini na mke wa mtu, au unaiba au unaua, watu wanakukamata wanakuua kwa kukuchinja au kukuchoma moto au kwa kipigo, halafu unaanza kumlaumu Mungu eti haja kulinda.
Unaanza kimsingizia Mungu eti ameumba dunia yenye machafuko ya vita na kadhalika kadhalika.
Umeambiwa kabisa usipotii Neno la Mungu hakika utakufa, sasa kwanini lawama.
Neno la Mungu ndio afya na ulinzi wenyewe.
Amri ambazo Mungu ameziweka ili tuzifuate, zimewekwa kwa manufaa yetu wenyewe ili tustawi hapa duniani na kufurahia maisha.
Tusipo zifuata basi tukubali madhara yatakayotupata, chanzo ni sisi wenyewe.
Ndio maana mtu akipigwa kwa kufumaniwa haendi kushtaki popote, anajua amestahili adhabu hiyo.
Wajibu wa kufanya Wema au Ubaya upo mikononi mwetu.
 
Binadamu ana Free will ya kutenda mema tu.
Kwenye kutenda mabaya Binadamu hana Free will.
Tupo huru kufanya mambo mazuri kama kufanya kazi, kuabudu, kujiburudisha, kusaidia wengine, kula chakula nk.
Katika kufanya uovu Binadamu hana uhuru.
Ukimtukana mtu utashtakiwa na kufungwa jela. Ukibaka utauawa na watu wenye hasira, ndio maana watu wanaogopa kufanya maovu.
Hatupo huru kufanya uovu.
Tupo huru kufanya mambo mema tu.
 
Free wil ni contradiction kwani Mungu mwenye uwezo wote haiwezekani binadam akawa free! Kila anachofanya mtu Mungu anajua ! Hiyo free wil imetoka wapi ?
 
kama tunayo basi itakuwa ni freewill ya mwendokasi 😱😱 maana hiyo freewill haiwezekani niikute wakati nishafika duniani 😳😳 ilitakiwa niipate kabla ya kuja duniani hiyo sio freewill hiyo ni lazima case closed
 
Free will ni uhuru wa mustakabali wako.. Ni nguvu isiyo na uwezo wa kuidhibiti kimwili.. Ni mtazamo wenye asili ya roho na kila mtu huwa nayo utotoni
Lakini kadiri makuzi yanavyoendelea nguvu hiyo huuliwa taratibu na mila desturi imani na elimu
. mila kuna limitations nyingi kwenye mila unaambiwa hairuhusiwi kufanya hili au lile..
. imani unaambiwa kutokana na imani yetu ukisema hivi unakosea
. elimu zetu ni za upande mmoja huku wengi sana wakinyimwa elimu za kiroho utambuzi na ugunduzi
Good summary!!
Mazingira, makuzi, elimu, mila na desturi, n.k zimemuathiri mwanadamu katika free will yake sana.
Safari ya kiroho ni ya upekee kwa maana ya kuwa kila mmoja ameumbwa tofauti kuufikia u yeye wake....spiritual path

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliwahi kuandika thread hapa hapa jukwaani kuhusu usaliti wa yuda kwa yesu kuwa ni tulio/kitendo kklichopangwa kabla ila yuda alikuja kukamilisha script iliyotayali lakini kwa maksudi mods waliufuta ule uzi.Katika suala la free will binadamu na viumbe wengine hicho kitu hatuna bali limewekwa kiimani ili kuhalalisha adhabu ambazo mungu anasema atazitoa kwa wakosefu.Kama mungu kweli ametupa uhuru wa kuchagua mema na mabaya kwanini achikizwe na machaguo yetu,kama alikuwa hataki mabaya yafanyike aliyaumba kwa sababu gani,kwanini alimuumba binadamu ambaye anaweza kutenda mabaya ambayo yeye hayapendi.Hii dhana ya free will naipinga sana sababu ni illogic kabisa hivi kwanini mungu alimuumba shetani kama yeye anachukizwa na vitendo vyake?maswali ni mengi kuliko majibu.......Vitabu vinasema mungu anajuwa yaliyopita yaliyopo na yajayo,kama mwakani wewe au mimi nitafanya zinaa mungu anajuwa kabla hata ya kufanyika kitendo hicho,na kwa kuwa mungu anajuwa ni lazima hilo tendo nilifanye ili kuleta maana ya god is perfection tofauti na hapo mungu hatakuwa na sifa hii.Je kama nitafanya hili tendo huo mwwaka huoni kuwa sikuwa na uhuru wa kuchagua sababu my fate ilikuwa tayari existed.Binadamu hatuna freewill mungu anatuonea kwa kutupa adhabu ambazo yeye ambaye ni perfection angeweza kuziondoa since day one of creation


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Benedict de Spinoza katika kitabu chake cha Tractatus; Theologico-Politicus anasema Deus sive Natura akimaanisha God or Nature chapter three nanukuu "Whether we say...that all things happen according to the laws of nature, or are ordered by the decree and direction of God, we say the same thing.".
Katika chapter 3 na 4 anachotaka kutueleza ni kwamba Mungu na "Nature" acha niite asili (nimekosa kiswahili chake) ni kitu kimoja kwamba kila amuzi unalofanya na unalopitia sio kwamba umeamua kulifanya eti kisa unalipenda bali ni sababu mazingira(nature) yanakushawish ulifanye!
the infant believes that it is by free will that it seeks the breast; the angry boy believes that by free will he wishes vengeance; the timid man thinks it is with free will he seeks flight; the drunkard believes that by a free command of his mind he speaks the things which when sober he wishes he had left unsaid. … All believe that they speak by a free command of the mind, whilst, in truth, they have no power to restrain the impulse which they have to speak.″. kila unachofanya kina ushawish na mazingira uliyopo lasivyo jiulize;
  • unaweza zuia kasirika, lia, cheka?
  • Unaweza zuia kuamua, mawazo?
  • Unaweza zuia hisia zako/ zikaact tofauti na unavyoishi siku zote?
Binadamu hatuna FREE WILL
Mkuu upo sahihi. Hata utatuzi wa jambo utegemea kuelewa kwanza kipi ni chanzo kwa asili.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bro free will tunayo that why tunajua lipi ni jema na lipi ni baya na tuuwezo wa kuchagua na kwa upande wa Yuda alitumia free will kumuuza Yesu na mpango wa Mungu ulikuwa kumkomboa binadamu kwa njia kifo na mateso lakini si mpango wa Mungu kwa Yuda kumsaliti Yesu kilichotokea kwa Yuda ni misuse of our freedom ( free will) ikampelekea Yuda kumuuza Yesu ukitaka ku prove hii Yesu alimlaumu Yuda kwa kitendo chake kwani alimwambia kwa kitendo anachodhamilia kukifanya ni heri asingezaliwa hivyo free will ipo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa upande wangu naweza kusema kuwa free will anayo Mungu sisi tunapewa kama gifts after birth ila sio kwamba u can do each and everything bila sir God kujua kinachoendelea

Sent using Infinix hot 4
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom