MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
Nimejiuliza sana kuhusiana na kile kinaendelea nchini kuhusiana na suala la chanjo za korona!
Yaani kwa ufupi ni kuwa, kama CHADEMA ingekuwa kwa sasa madarakani, chanjo ya korona nchini ingekuwa ni LAZIMA kwa kila mwananchi nchini. Ikumbukwe kuwa, Mbowe wakati akiongea na vyombo vya habari tarehe 19 Julai 2021 alinukuliwa akisema, “serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan iweke utaratibu mzuri wa chanjo kuwa ya LAZIMA kwa Watanzania”
Kama hukumsikia Mbowe akisema, gonga hii LINK kwenye gazeti la viongozi wa upinzani;
Bahati nzuri sana “Mwenyezi Mungu” alituepusha watanzania kuwa na viongozi serikalini wenye mawazo kama ya Freeman Mbowe katika maamuzi ya chanjo za korona.
Kinachoendelea kwa sasa nchini kuhusu chanjo za korona kinaonyesha hata wanachama wengi wa CHADEMA hawakubaliani na fikra za Mwenyekiti wao wa taifa.
Fikiria mpaka sasa ni Watanzania laki tatu na ushee pekee ambao wamejitokeza kwenda kupata chanjo za korona. Ieleweke kuwa kwa sasa ni zaidi ya mwezi mmoja na nusu tokea chanjo milioni 1.5 zianze kutolewa.
Tunaambiwa na viongozi wa CHADEMA kuwa CHADEMA ina wanachama milioni 7.
Ukijiuliza kati ya watu laki tatu na ushee waliojitokeza kwenda kupata chanjo ya korona ni wanachama wangapi wa CHADEMA ambao ni miongoni mwao?
Kinachoendelea katika zoezi la chanjo za korona kinaonyesha wana CHADEMA wengi wamempuuza Mwenyekiti wao wa Taifa kwenya suala la chanjo za korona.
Kama aliyekuwa Rais wa Tanzania, Magufuli aliwatia kasumba(brainwash) watanzania kwenye suala la chanjo za korona kama tunavyoambiwa na baadhi ya watu ina maana hata wana CHADEMA wengi walikubaliana na kasumba hiyo ambayo inadharau fikra za Mwenyekiti wao wa CHADEMA, Freeman Mbowe?
Kwa sasa tunaona baadhi ya viongozi wa CCM na serikali yake wakisaidiwa na bunge wameanza kutafuta “mbuzi wa kafara” baada ya zoezi la chanjo za korona kudoda ili baadaye watuambie zoezi limedoda kwa sababu ya Askofu Gwajima na Polepole kuwatia kasumba(brainwash) wananchi wengi nchini.
Je, Mbowe pia atamtafuta nani kuwa “mbuzi wa kafara” kwenye suala la chanjo ndani ya CHADEMA baada ya wazo lake kukataliwa na wanachama wengi ndani ya chama hasa ikichukuliwa alitueleza mara nyingi kuwa Rais Magufuli hana ushawishi mkubwa nchini achilia mbali kwa wana CHADEMA?
Kiufupi, chanjo za korona zimekataliwa na watanzania wengi nchini kwa sababu wananchi wameonyesha wanajitambua bila kujali wanachokitaka viongozi wao pamoja na kwamba baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa walitaka kulifanya suala la korona kama la kisiasa.
Viongozi wa serikali na vyama vya siasa wamepewa somo ambalo kama wana akili timamu watajifunza.
Juzi wananchi wa Kawe walimwambia Rais Samia “HATUCHANJI” baada ya kuwauliza kama wanachanja au hawachanji.
Yaani kwa ufupi ni kuwa, kama CHADEMA ingekuwa kwa sasa madarakani, chanjo ya korona nchini ingekuwa ni LAZIMA kwa kila mwananchi nchini. Ikumbukwe kuwa, Mbowe wakati akiongea na vyombo vya habari tarehe 19 Julai 2021 alinukuliwa akisema, “serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan iweke utaratibu mzuri wa chanjo kuwa ya LAZIMA kwa Watanzania”
Kama hukumsikia Mbowe akisema, gonga hii LINK kwenye gazeti la viongozi wa upinzani;
Bahati nzuri sana “Mwenyezi Mungu” alituepusha watanzania kuwa na viongozi serikalini wenye mawazo kama ya Freeman Mbowe katika maamuzi ya chanjo za korona.
Kinachoendelea kwa sasa nchini kuhusu chanjo za korona kinaonyesha hata wanachama wengi wa CHADEMA hawakubaliani na fikra za Mwenyekiti wao wa taifa.
Fikiria mpaka sasa ni Watanzania laki tatu na ushee pekee ambao wamejitokeza kwenda kupata chanjo za korona. Ieleweke kuwa kwa sasa ni zaidi ya mwezi mmoja na nusu tokea chanjo milioni 1.5 zianze kutolewa.
Tunaambiwa na viongozi wa CHADEMA kuwa CHADEMA ina wanachama milioni 7.
Ukijiuliza kati ya watu laki tatu na ushee waliojitokeza kwenda kupata chanjo ya korona ni wanachama wangapi wa CHADEMA ambao ni miongoni mwao?
Kinachoendelea katika zoezi la chanjo za korona kinaonyesha wana CHADEMA wengi wamempuuza Mwenyekiti wao wa Taifa kwenya suala la chanjo za korona.
Kama aliyekuwa Rais wa Tanzania, Magufuli aliwatia kasumba(brainwash) watanzania kwenye suala la chanjo za korona kama tunavyoambiwa na baadhi ya watu ina maana hata wana CHADEMA wengi walikubaliana na kasumba hiyo ambayo inadharau fikra za Mwenyekiti wao wa CHADEMA, Freeman Mbowe?
Kwa sasa tunaona baadhi ya viongozi wa CCM na serikali yake wakisaidiwa na bunge wameanza kutafuta “mbuzi wa kafara” baada ya zoezi la chanjo za korona kudoda ili baadaye watuambie zoezi limedoda kwa sababu ya Askofu Gwajima na Polepole kuwatia kasumba(brainwash) wananchi wengi nchini.
Je, Mbowe pia atamtafuta nani kuwa “mbuzi wa kafara” kwenye suala la chanjo ndani ya CHADEMA baada ya wazo lake kukataliwa na wanachama wengi ndani ya chama hasa ikichukuliwa alitueleza mara nyingi kuwa Rais Magufuli hana ushawishi mkubwa nchini achilia mbali kwa wana CHADEMA?
Kiufupi, chanjo za korona zimekataliwa na watanzania wengi nchini kwa sababu wananchi wameonyesha wanajitambua bila kujali wanachokitaka viongozi wao pamoja na kwamba baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa walitaka kulifanya suala la korona kama la kisiasa.
Viongozi wa serikali na vyama vya siasa wamepewa somo ambalo kama wana akili timamu watajifunza.
Juzi wananchi wa Kawe walimwambia Rais Samia “HATUCHANJI” baada ya kuwauliza kama wanachanja au hawachanji.